• Wasiliana Nasi |
    • Malalamiko |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
    • Blog |
Singida Regional Website

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Tovuti ya Mkoa wa Singida

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na dhima
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Ikungi
      • HISTORIA
    • Iramba
    • Manyoni
    • Mkalama
    • Singida
  • Halmashauri
    • H/W Ikungi
    • H/W Iramba
    • H/W Itigi
    • H/W Manyoni
    • H/W Mkalama
    • H/W Singida
    • H/M Singida
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Viwanda na Biashara
    • Madini
  • Huduma Zetu
    • Afya
      • Madaktari Bingwa
      • Huduma za Tiba
      • Huduma za Kinga
      • Ustawi wa Jamii
      • Afya ya Mazingira
      • Lishe
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba Wa Huduma Kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
    • Investment Guide
  • Kituo Cha Habari
    • Picha
    • Video
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma

RAS Singida atoa wiki moja kuweka vyumba vya madarasa sakafu.

Posted on: February 15th, 2023

Katibu Tawala Mkoa wa Singida Mwl. Dorothy Mwaluko  ametoa muda wa siku saba  (wiki moja ) kwa Afisa Elimu Kata, Mtendaji na kamati za shule  kuhakikisha vyumba vyote vya madarasa katika Shule ya Msingi Kilimatinde iliyopo kata ya Kilimatinde Wilaya ya Manyoni vinawekwa sakafu.

Maelekezo hayo ameyatoa leo baada ya uwekaji wa jiwe la msingi katika jengo la ofisi ya Afisa Tarafa wa Tarafa husika ambapo pamoja na mambo mengine alitaka kupata taarifa ya shule hiyo ya msingi ikiwemo uwepo wa vyoo, madarasa na madawati.

Katibu Tawala Mkoa wa Singida Mwl. Dorothy Mwaluko (kulia) akisisitiza jambo kwa Afisa Elimu wa Kata hiyo Laura Athanas wakati wa ziara hiyo Wilayani Manyoni.

Mwaluko alisema kwamba ni Mpango wa Serikali kuhakikisha kwamba kila shule inapata ruzuku ya elimu bure (Capitation grant ) ambapo alifafanua kwamba Mwalimu Mkuu pamoja na Afisa elimu wangeweza kuilekeza katika ujenzi wa sakafu hizo na kuwaondolea wanafunzi changamoto ya kusoma kwenye madarasa yenye vumbi.

"Mnapopata capitation msikimbilie kununua chaki angalieni namna itakavyowezekana ndani ya siku saba vyumba hivyo viwe vimewekewa sakafu, Afisa Elimu na Mtendaji shirikianeni muwashawishi wazazi na mafundi wajitolee nguvu kazi hiyo ikamilike" alisema.

Hata hivyo Afisa Elimu wa Kata hiyo Laura Athanas, alieleza kwamba katika shule hiyo wana jumla ya wanafunzi Mia nne (400) hivyo kupata ruzuku ndogo ikilinganishwa na shule nyinge jambo ambalo RAS alikataa vikali kwa mifano kwamba zipo shule zinapata fedha kidogo lakini bado wanaweza kufanya na kusimamia mipango ikakaa vizuri.

Aidha, RAS huyo alianzisha harambee ya kuchangia mifuko ya saruji ambapo alitoa mifuko mitano, Afisa Elimu naye akatoa mifuko miwili, huku Menejimenti ya Mkoa huo ilitoa jumla ya mifuko 10 kwa ajili ya uwekaji wa sakafu katika vyumba hivyo.

Ziara hiyo ilihusisha Menejiment ya Mkoa huo na walitembelea Ujenzi wa nyumba ya Afisa Tarafa kata ya Nkonko na Kilimatinde pamoja na ukaguzi wa Ujenzi wa shule ya Sekondari ya Wasichana Solya na Hospitali ya Wilaya ya Manyoni.

MATUKIO KATIKA PICHA

Ukaguzi wa Ujenzi wa shule ya Sekondari ya Wasichana Solya Wilayani Manyoni.

Ukaguzi Hospitali ya Wilaya ya Manyoni

Matangazo

  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2022_2023 SINGIDA RS July 01, 2022
  • MAJINA YA WALIOCHANGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA - 2023, MKOA WA SINGIDA December 14, 2022
  • TAARIFA YA MAPOKEZI YA FEDHA KWA KIPINDI CHA KUANZIA JULAI HADI OCTOBA, 2023 KWA AJILI YA UTEKELEZAJI WA SHUGHULI ZA MAENDELEO November 01, 2023
  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2021/2022 SINGIDA RS - GPN 2021 - 2022 July 01, 2021
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • DKT.MGANGA ASISITIZA MADAKTARI BINGWA KUTOA HUDUMA BORA

    May 05, 2025
  • WATUMISHI NA WAAJIRI HODARI MKOANI SINGIDA WAPOKEA TUZO

    May 02, 2025
  • KUELEKEA MEIMOSI,RC DENDEGO ATANGAZA FURSA ZA UWEKEZAJI

    April 25, 2025
  • MADAKTARI BINGWA WA DKT.SAMIA WABISHA HODI SINGIDA

    April 23, 2025
  • Angalia Zote

Video

Mkoa wa Singida waja na Mikakati ya Kuboresha Elimu
Video zaidi

Viungio vya Haraka

  • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
  • Mwongozo wa Matumizi ya TEHAMA Serikalini
  • Fomu ya Maombi ya Kusafiri Nje ya Nchi
  • MPANGO WA MANUNUZI MKOA WA SINGIDA
  • KUONA AJIRA ZA WAALIMU WA SAYANSI NA MAFUNDI SANIFU

Tovuti Muhimu

  • UTUMISHI
  • TAMISEMI
  • IKULU
  • WIZARA YA ELIMU
  • NECTA
  • WIZARA YA AFYA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Ramani ya Mkoa

Wasiliana Nasi

    SINGIDA

    Anuani: P O BOX 5 SINGIDA

    Simu: 2502170, 2502089

    Simu: 2502170, 2502089

    Barua Pepe: info@singida.go.tz ras@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Usiri
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

Copyright ©2023 Singida Regional Commisioner' Office . All rights reserved.