• Wasiliana Nasi |
    • Malalamiko |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
    • Blog |
Singida Regional Website

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Tovuti ya Mkoa wa Singida

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na dhima
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Ikungi
      • HISTORIA
    • Iramba
    • Manyoni
    • Mkalama
    • Singida
  • Halmashauri
    • H/W Ikungi
    • H/W Iramba
    • H/W Itigi
    • H/W Manyoni
    • H/W Mkalama
    • H/W Singida
    • H/M Singida
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Viwanda na Biashara
    • Madini
  • Huduma Zetu
    • Afya
      • Madaktari Bingwa
      • Huduma za Tiba
      • Huduma za Kinga
      • Ustawi wa Jamii
      • Afya ya Mazingira
      • Lishe
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba Wa Huduma Kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
    • Investment Guide
  • Kituo Cha Habari
    • Picha
    • Video
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma

RC DENDEGO AONGOZA VIONGOZI NA WANANCHI KUSHIRIKI UJENZI

Posted on: March 4th, 2025

Katika kuonyesha kuwa wanawake wanaweza,Mkuu wa Mkoa wa Singida, Halima Dendego, leo (Machi 4, 2025) amewaongoza wanawake wa Wilaya ya Singida kushiriki ujenzi wa shule ya amali ya Mkoa wa Singida inayojengwa kata ya Unyambwa Manispaa ya Singida kwa gharama ya Sh.bilioni 1.6 ikiwa ni mwendelezo wa maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani.

Akizungumza na wanawake waliojitokeza kushiriki ujenzi huo amesema kwamba Halmashauri zote za Mkoa huo zimepewa fedha kwa ajili ya ujenzi wa shule ya Amali ambayo  watachaguliwa kujiunga wanafunzi wenye vipaji.

.         "Tunamshukru Rais Dk.Samia Suluhu Hassan,tumeona dhamira yake ya kweli kwa Watanzania ya kuweza kuwakwamua kiuchumi,shule hii ya Amali inayojengwa kata ya Unyambwa tutawachagua wenye vipaji ndio wajiunge ili watuletee mageuzi ya kiuchumi,alisema Mhe.Dendego

               Mhe.Dendego amesema nchi yetu imezindua sera mpya ya elimu inayokwenda kuangalia vitendo na elimu ya nadharia lengo ili mwanafunzi anapohitimu masomo aweze kujiajiri au kuajiriwa akiwa tayari ana ujuzi mkubwa.

Aidha,Mkuu wa Mkoa wa Singida amezipongeza wilaya zote wa mkoa huu kwa kutekeleza maelekezo ya serikali katika kuadhimisha siku ya wanawake dunia kuanzia ngazi ya Kata hadi Mkoa ambayo yamewashirikisha wanawake kwa kufanya shughuli mbalimbali za maendeleo.

                   Awali Mhandisi wa Manispaa ya Singida amesema serikali  imetoa Sh.Bilioni.1.6 kwa ajili ya ujenzi wa shule ya amali ya Mkoa wa Singida ambayo itakapokamilika katika awamu ya kwanza itachukua wanafunzi takribani 400 wenye vipaji watakaofundishwa ufundi wa aina mbalimbali.

Akitoa taarifa kwa Mkuu wa Mkoa wa Singida,Ameongoza mamia ya wanawake wa Wilaya ya Singida kushiriki ujenzi wa shule hiyo ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya siku ya wanawake duniani ambayo kilele chake ni Machi 8, 2025.

Amesema katika awamu ya kwanza ujenzi ambao unatarajia kukamilika Mei 29, 2025 majengo 22 yatajengwa yakiwamo madarasa nane,maabara 2,mabweni 4,karakana ya ujenzi na ufundi uashi na karakana ya ufundi magari na kuchomelea.

Matangazo

  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2022_2023 SINGIDA RS July 01, 2022
  • MAJINA YA WALIOCHANGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA - 2023, MKOA WA SINGIDA December 14, 2022
  • TAARIFA YA MAPOKEZI YA FEDHA KWA KIPINDI CHA KUANZIA JULAI HADI OCTOBA, 2023 KWA AJILI YA UTEKELEZAJI WA SHUGHULI ZA MAENDELEO November 01, 2023
  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2021/2022 SINGIDA RS - GPN 2021 - 2022 July 01, 2021
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • DKT.MGANGA ASISITIZA MADAKTARI BINGWA KUTOA HUDUMA BORA

    May 05, 2025
  • WATUMISHI NA WAAJIRI HODARI MKOANI SINGIDA WAPOKEA TUZO

    May 02, 2025
  • KUELEKEA MEIMOSI,RC DENDEGO ATANGAZA FURSA ZA UWEKEZAJI

    April 25, 2025
  • MADAKTARI BINGWA WA DKT.SAMIA WABISHA HODI SINGIDA

    April 23, 2025
  • Angalia Zote

Video

Mkoa wa Singida waja na Mikakati ya Kuboresha Elimu
Video zaidi

Viungio vya Haraka

  • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
  • Mwongozo wa Matumizi ya TEHAMA Serikalini
  • Fomu ya Maombi ya Kusafiri Nje ya Nchi
  • MPANGO WA MANUNUZI MKOA WA SINGIDA
  • KUONA AJIRA ZA WAALIMU WA SAYANSI NA MAFUNDI SANIFU

Tovuti Muhimu

  • UTUMISHI
  • TAMISEMI
  • IKULU
  • WIZARA YA ELIMU
  • NECTA
  • WIZARA YA AFYA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Ramani ya Mkoa

Wasiliana Nasi

    SINGIDA

    Anuani: P O BOX 5 SINGIDA

    Simu: 2502170, 2502089

    Simu: 2502170, 2502089

    Barua Pepe: info@singida.go.tz ras@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Usiri
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

Copyright ©2023 Singida Regional Commisioner' Office . All rights reserved.