• Wasiliana Nasi |
    • Malalamiko |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
    • Blog |
Singida Regional Website

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Tovuti ya Mkoa wa Singida

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na dhima
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Ikungi
      • HISTORIA
    • Iramba
    • Manyoni
    • Mkalama
    • Singida
  • Halmashauri
    • H/W Ikungi
    • H/W Iramba
    • H/W Itigi
    • H/W Manyoni
    • H/W Mkalama
    • H/W Singida
    • H/M Singida
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Viwanda na Biashara
    • Madini
  • Huduma Zetu
    • Afya
      • Madaktari Bingwa
      • Huduma za Tiba
      • Huduma za Kinga
      • Ustawi wa Jamii
      • Afya ya Mazingira
      • Lishe
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba Wa Huduma Kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
    • Investment Guide
  • Kituo Cha Habari
    • Picha
    • Video
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma

RC MAHENGE ATOA MAAGIZO MAZITO KWA WATENDAJI MANISPAA YA SINGIDA

Posted on: October 19th, 2021

Mkuu wa Mkoa wa Singida Dkt. Binilith Saatano Mahenge amefanya ziara ya kikazi ya kukagua miradi mbalimbali ya maendeleo na tathimini ya hali ya uwajibikaji kwa watumishi ndani ya manispaa ya Singida.

Akiwa kwenye Manispaa hiyo Oktoba 18,2021 alibaini kuna uzembe mkubwa unaofanywa na baadhi ya watendaji kwa kuto ekeleza kwa maksudi takwa la kisheria la kuhakikisha wanatenga asilimia kumi ya mapato wanayokusanya kila mwezi kwa ajili ya makundi ya wanawake , vijana na wenye ulemavu.

"Nakuagiza Mkurugenzi kufikia mwezi huu mwishoni nataka fedha zote za asilimia kumi ziwe zimetengwa hata kama mnakusanya mapato kidogo. Hii haimwepeki ukikwepa ni sawa na kuichelewesha na kuilimbikiza ", alisema Mahenge.

Akiwa kwenye Machinjio kuu ya Manispaa hiyo iliyopo katika kata ya Mughanga, baada ya kupokea taarifa za kero mbalimbali zinazotokana na uchakavu wa miundombinu ya machinjio hiyo, Mkuu wa Mkoa aligiza kuhamisha machinjio hiyo na kuipeleka eneo la Ng'aida kata ya Kisaki ili kupisha makazi ya watu.

Machinjio hiyo ambayo huchinja wastani wa ng'ombe 40 na mbuzi 20 kwa siku ilijengwa miaka ya 70 iliyopita kwa sasa imekosa ubora kutokana na kukithiri kwa kasoro mbalimbali zinazotokana na uchakavu wa miundombinu yake ikiwemo kero ya utiririshaji wa maji taka na mbolea kwenye makazi ya watu hasa kipindi cha mvua.

Aidha akiwa Stendi Kuu ya Mabasi ya Abiria Misuna aliagiza kuundwa kwa kamati ndogo ya tathimini ambayo itajumuisha madiwani wasiopungua watatu na wataalamu ili kufanya 'stadi' ya je mapato yanayokusanywa ni halali au la.

"Tengenezeni kikundi cha watu watatu waje washinde hapa muda wote kuanzia asubuhi mbaka jioni kufanya 'analysis ' ya kina na watalamu kubaini chanzo hiki kinaweza kikatoa shilingi ngapi wakati wa 'pick ' na usio 'pick'; "alisema Mahenge".

Hata hivyo badala ya kukusanya takribani Milioni 45 kwenye chanzo hicho bado kumekuwa na hali ya kusuasua kwenye makusanyo kutokana na kile kilichoelezwa na viongozi wa Manispaaa kuwa kuna baadhi ya watumishi wasio waaminifu wanakwamisha jitihada hizo.

Pia Mkuu wa Mkoa alitembelea Maziwa ya asili ya Kindai na Munangi na kuagiza zoezi la kusafisha fukwe pembezoni mwa maziwa hayo yote ikiwemo lile na singidani kuanza mara moja na atarudi kwa ukaguzi ndani ya mwezi mmoja kuanzia sasa.

"Katika vitu ambavyo Mwenyezi Mungu ameijalia Singida ni pamoja na haya Maziwa. Huu ni utajiri na urithi wa pekee sana ili urithi huu tuweze kuufaidi ni lazima tutengeneze mazingira mazuri kwa watalii kuanza kufika na kutazama vivutio hivi,"alisema Mahenge".

Mkuu wa Mkoa wa Singida Dkt Binilith Saatano Mahenge akizungumza na watumishi wa Halmashauri ya Manispaa ya Singida katika eneo la Machinjio kuu ya Manispaa wakati wa ziara yake ya kikazi.

Kikao kikiendelea

Mkurugenzi wa Manispaa ya Singida Zefrin Lubuva akitoa maelekezo ya namna stendi kuu ya Misuna inavokusanya mapato

Viongozi wa Chama na Serikali wakiongozwa na Mkuu wa Mkoa wa Singida Dkt. Binilith Saatano Mahenge (watatu kutoka kulia) wakikagua Stendi ya mabasi Misuna mkoani Singida

Matangazo

  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2022_2023 SINGIDA RS July 01, 2022
  • MAJINA YA WALIOCHANGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA - 2023, MKOA WA SINGIDA December 14, 2022
  • TAARIFA YA MAPOKEZI YA FEDHA KWA KIPINDI CHA KUANZIA JULAI HADI OCTOBA, 2023 KWA AJILI YA UTEKELEZAJI WA SHUGHULI ZA MAENDELEO November 01, 2023
  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2021/2022 SINGIDA RS - GPN 2021 - 2022 July 01, 2021
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • IKUNGI YAPEPERUSHA BENDERA KWA MIRADI YA KIMKAKATI.

    May 08, 2025
  • DKT.MGANGA ASISITIZA MADAKTARI BINGWA KUTOA HUDUMA BORA

    May 05, 2025
  • WATUMISHI NA WAAJIRI HODARI MKOANI SINGIDA WAPOKEA TUZO

    May 02, 2025
  • KUELEKEA MEIMOSI,RC DENDEGO ATANGAZA FURSA ZA UWEKEZAJI

    April 25, 2025
  • Angalia Zote

Video

Mkoa wa Singida waja na Mikakati ya Kuboresha Elimu
Video zaidi

Viungio vya Haraka

  • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
  • Mwongozo wa Matumizi ya TEHAMA Serikalini
  • Fomu ya Maombi ya Kusafiri Nje ya Nchi
  • MPANGO WA MANUNUZI MKOA WA SINGIDA
  • KUONA AJIRA ZA WAALIMU WA SAYANSI NA MAFUNDI SANIFU

Tovuti Muhimu

  • UTUMISHI
  • TAMISEMI
  • IKULU
  • WIZARA YA ELIMU
  • NECTA
  • WIZARA YA AFYA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Ramani ya Mkoa

Wasiliana Nasi

    SINGIDA

    Anuani: P O BOX 5 SINGIDA

    Simu: 2502170, 2502089

    Simu: 2502170, 2502089

    Barua Pepe: info@singida.go.tz ras@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Usiri
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

Copyright ©2023 Singida Regional Commisioner' Office . All rights reserved.