• Wasiliana Nasi |
    • Malalamiko |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
    • Blog |
Singida Regional Website

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Tovuti ya Mkoa wa Singida

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na dhima
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Ikungi
      • HISTORIA
    • Iramba
    • Manyoni
    • Mkalama
    • Singida
  • Halmashauri
    • H/W Ikungi
    • H/W Iramba
    • H/W Itigi
    • H/W Manyoni
    • H/W Mkalama
    • H/W Singida
    • H/M Singida
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Viwanda na Biashara
    • Madini
  • Huduma Zetu
    • Afya
      • Madaktari Bingwa
      • Huduma za Tiba
      • Huduma za Kinga
      • Ustawi wa Jamii
      • Afya ya Mazingira
      • Lishe
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba Wa Huduma Kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
    • Investment Guide
  • Kituo Cha Habari
    • Picha
    • Video
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma

RC Serukamba ahimiza miradi inayotekelezwa Iramba ikamilike kabla Juni 10, mwaka huu

Posted on: May 16th, 2023

MKUU wa Mkoa wa Singida, Peter Serukamba, ameanza ziara ya siku 13 ya kutembelea na kukagua miradi ya maendeleo inayotekelezwa katika Halmashauri za mkoa huu ambapo leo (Mei 16, 2023) ameanzia katika Halmashauri ya Wilaya ya Iramba.

Katika miradi aliyoitembelea na kuikagua katika Halmashauri ya Wilaya ya Iramba, Serukamba amewagiza Watendaji kuhakikisha wanaisimamia ili iweze kukamilika kabla ya Juni 10, mwaka huu.

Miradi aliyoitembelea ni pamoja na ujenzi wa barabara ya Mugungia-Kaselya, ujenzi madarasa na vyoo katika Shule ya Msingi Muungano, ujenzi wa Zahanati ya Mugungia, ujenzi wa darasa moja katika Shule ya Msingi Mbelekese na ujenzi wa hosteli katika Shule ya Sekondari Mbelekese.

Miradi mingine ni ujenzi wa vyoo, jengo la mtoto, uzazi na miundombinu ya kuvunia maji ya kunawa mikono katika Zahanati ya Usure, ujenzi wa madarasa na vyoo katika Shule ya Msingi Luzilukulu, ujenzi wa bwalo la chakula na hosteli katika Shule ya Sekondari Ndago, kukagua ujenzi wa barabara ya Songambele-Misuna na ujenzi wa nyumba ya Afisa Tarafa ya Ndago.

Serukamba alihitimisha ziara yake siku ya kwanza katika Wilaya hiyo kwa kukagua ujenzi wa nyumba ya mwalimu katika Shule ya Msingi Ulyang’ombe, ujenzi wa shule mpya ya mikondo miwili ya Ng’anguli, ujenzi wa vyumba viwili vya madarasa katika Shule ya sekondari Kinampanda, ujenzi wa nyumba ya Afisa Tarafa Kinampanda, ujenzi wa madarasa na vyoo katika Shule ya Msingi Kitukutu na ujenzi wa zahanati ya Ulemo.

Akiwa katika mradi wa ujenzi wa shule mpya ya Ng’anguli, Mkuu wa Mkoa alisema hajaridhishwa na kasi ya utekelezaji wa mradi huo na kumwagiza Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya hiyo kuhakikisha anafuatilia kwa karibu mradi huo ili uweze kukamilika kabla ya Juni 10, mwaka huu.

Serukamba alimwambia Mwalimu Mkuu wa Shule hiyo, Juvena Sebastian kama hawezi kusimamia ujenzi wa mradi huo na kukamilika haraka kabla ya Juni 10 amweleze Mkurugenzi mapema ili nafasi hiyo apewe mtu mwingine atakayeweza kusimamia ukamilike kwa haraka.


 

 

Matangazo

  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2022_2023 SINGIDA RS July 01, 2022
  • MAJINA YA WALIOCHANGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA - 2023, MKOA WA SINGIDA December 14, 2022
  • TAARIFA YA MAPOKEZI YA FEDHA KWA KIPINDI CHA KUANZIA JULAI HADI OCTOBA, 2023 KWA AJILI YA UTEKELEZAJI WA SHUGHULI ZA MAENDELEO November 01, 2023
  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2021/2022 SINGIDA RS - GPN 2021 - 2022 July 01, 2021
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • DKT.MGANGA ASISITIZA MADAKTARI BINGWA KUTOA HUDUMA BORA

    May 05, 2025
  • WATUMISHI NA WAAJIRI HODARI MKOANI SINGIDA WAPOKEA TUZO

    May 02, 2025
  • KUELEKEA MEIMOSI,RC DENDEGO ATANGAZA FURSA ZA UWEKEZAJI

    April 25, 2025
  • MADAKTARI BINGWA WA DKT.SAMIA WABISHA HODI SINGIDA

    April 23, 2025
  • Angalia Zote

Video

Mkoa wa Singida waja na Mikakati ya Kuboresha Elimu
Video zaidi

Viungio vya Haraka

  • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
  • Mwongozo wa Matumizi ya TEHAMA Serikalini
  • Fomu ya Maombi ya Kusafiri Nje ya Nchi
  • MPANGO WA MANUNUZI MKOA WA SINGIDA
  • KUONA AJIRA ZA WAALIMU WA SAYANSI NA MAFUNDI SANIFU

Tovuti Muhimu

  • UTUMISHI
  • TAMISEMI
  • IKULU
  • WIZARA YA ELIMU
  • NECTA
  • WIZARA YA AFYA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Ramani ya Mkoa

Wasiliana Nasi

    SINGIDA

    Anuani: P O BOX 5 SINGIDA

    Simu: 2502170, 2502089

    Simu: 2502170, 2502089

    Barua Pepe: info@singida.go.tz ras@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Usiri
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

Copyright ©2023 Singida Regional Commisioner' Office . All rights reserved.