• Wasiliana Nasi |
    • Malalamiko |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
    • Blog |
Singida Regional Website

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Tovuti ya Mkoa wa Singida

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na dhima
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Ikungi
      • HISTORIA
    • Iramba
    • Manyoni
    • Mkalama
    • Singida
  • Halmashauri
    • H/W Ikungi
    • H/W Iramba
    • H/W Itigi
    • H/W Manyoni
    • H/W Mkalama
    • H/W Singida
    • H/M Singida
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Viwanda na Biashara
    • Madini
  • Huduma Zetu
    • Afya
      • Madaktari Bingwa
      • Huduma za Tiba
      • Huduma za Kinga
      • Ustawi wa Jamii
      • Afya ya Mazingira
      • Lishe
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba Wa Huduma Kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
    • Investment Guide
  • Kituo Cha Habari
    • Picha
    • Video
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma

Singida waaswa kuendeleza mapambano dhidi ya Ugonjwa wa Kifua Kikuu

Posted on: March 24th, 2023

Wananchi mkoani Singida wametakiwa kuendeleza mapambano dhidi ya ugonjwa wa Kifua Kikuu ili kuweza kuutokomeza na kuwa na afya bora ambapo imeelezwa kuwa mwaka 2021 walingundulika wagonjwa wapya 2597 na mwaka 2022 wagonjwa 2724 sawa na asilimia 93.19 ya lengo la ugunduzi wa wagonjwa 2923 ambalo Mkoa ulipewa na Mpango wa Taifa wa kudhibiti Kifua Kikuu na Ukoma kwa kushirikiana na Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (OR-TAMISEMI).

Wito huo umetolewa leo na Mkuu wa Wilaya ya Ikungi Thomas Apson, wakati akisoma hotuba kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Singida Peter Serukamba katika maadhimisho ya siku ya Kifua Kikuu duniani yaliyofanyika kimkoa kijiji cha Ilongero Halmashauri ya Wilaya ya Singida.

DC Apson amesema ugonjwa wa Kifua Kikuu bado ni changamoto la kijamii hivyo kuna umuhimu wa kuchukua hatua madhubuti katika mapambano dhidi yake huku akifafanua kuwa endapo jamii itahusika  kikamilifu katika mapambano hayo ugonjwa huo utakwisha.

Aidha DC amefafanua kuwa takwimu hizo zinamaanisha kwamba katika kila watu mia moja (100) watu ishirini na moja (21) wanaugua Kifua Kikuu ndio maana jamii inahitajika kutilia mkazo hamasa ya kupambana na ugonjwa huu na namna ya kujikinga.

Akiendelea na hotuba yake amesema katika kuadhimisha siku ya Kifua Kikuu duniani wananchi wa Mkoa wa Singida wanapaswa kuelewa na kuzingatia kuwa ugonjwa huo unasababishwa na bakteria na huenezwa kwa njia ya hewa kutoka kwa mgonjwa ambaye hajaanza matibabu na siyo kwa kulogwa wala kurithi kama inavyoaminika kwa baadhi ya watu.  

Pia amesisitiza kuwa uchunguzi wa tiba ya Kifua Kikuu hufanyika bila malipo katika Vituo vya Huduma za Afya vya Serikali na Bisafsi hivyo jamii imehaswa kutokuwa na hofu ya gharama wala woga wa kwenda hospitali kwaajili ya kupima na kupatiwa matibabu.

Mkuu huyo wa Wilaya amewahimiza wananchi wa mkoa huo kuhakikisha kuwa nyumba wanazoishi zina mzunguko wa hewa na mwanga wa jua wa kutosha ili kuepusha maambukizo ya Kifua Kikuu.

Ameeleza kuwa watoto wenye umri chini ya miaka mitano (5) wanaoishi kwenye kaya yenye mgonjwa wa Kifua Kikuu wanatakiwa kufanya uchunguzi mapema kwani wapo katika hatari ya kuambukizwa. Pia ni muhimu kwa wazazi au walezi kuwapa taarifa walimu wa afya au walezi wa shule kuhusu matibabu ya Kifua Kikuu ya watoto wao.

“Kumbuka si kila mgonjwa wa Kifua Kikuu ana VVU na si kila anayeishi na VVU ana Kifua Kikuu.  Chukua hatua, kapime afya” Amesisitiza Dc Apson

Akizungumzia kuhusu lishe kwa mgonjwa wa Kifua Kikuu Dc Apson, amesisitiza kuwa mgonjwa huyo anahitaji kupatiwa lishe bora ili kuimarisha afya yake pamoja na kupata ushauri kuhusu lishe kutoka kwa mtoa huduma.

 “Kifua Kikuu kinatibika na kupona kabisa; hivyo kuacha kunywa dawa za Kifua Kikuu kikamilifu kunaweza kusababisha vimelea kuwa sugu na hivyo kuambukiza Kifua Kikuu sugu watu wa karibu yako”. Amefafanua DC Apson

Maadhimisho ya siku ya Kifua Kikuu duniani huadhimishwa kila mwaka ifikapo tarehe 24 mwezi Machi. Kauli mbiu; KWA PAMOJA TUNAWEZA KUTOKOMEZA KIFUA KIKUU NCHINI TANZANIA.

Matangazo

  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2022_2023 SINGIDA RS July 01, 2022
  • MAJINA YA WALIOCHANGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA - 2023, MKOA WA SINGIDA December 14, 2022
  • TAARIFA YA MAPOKEZI YA FEDHA KWA KIPINDI CHA KUANZIA JULAI HADI OCTOBA, 2023 KWA AJILI YA UTEKELEZAJI WA SHUGHULI ZA MAENDELEO November 01, 2023
  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2021/2022 SINGIDA RS - GPN 2021 - 2022 July 01, 2021
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • HUDUMA ZA KIBINGWA ZAWAFIKIA WAGONJWA ZAIDI YA 3000 SINGIDA.

    May 09, 2025
  • IKUNGI YAPEPERUSHA BENDERA KWA MIRADI YA KIMKAKATI.

    May 08, 2025
  • DKT.MGANGA ASISITIZA MADAKTARI BINGWA KUTOA HUDUMA BORA

    May 05, 2025
  • WATUMISHI NA WAAJIRI HODARI MKOANI SINGIDA WAPOKEA TUZO

    May 02, 2025
  • Angalia Zote

Video

Mkoa wa Singida waja na Mikakati ya Kuboresha Elimu
Video zaidi

Viungio vya Haraka

  • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
  • Mwongozo wa Matumizi ya TEHAMA Serikalini
  • Fomu ya Maombi ya Kusafiri Nje ya Nchi
  • MPANGO WA MANUNUZI MKOA WA SINGIDA
  • KUONA AJIRA ZA WAALIMU WA SAYANSI NA MAFUNDI SANIFU

Tovuti Muhimu

  • UTUMISHI
  • TAMISEMI
  • IKULU
  • WIZARA YA ELIMU
  • NECTA
  • WIZARA YA AFYA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Ramani ya Mkoa

Wasiliana Nasi

    SINGIDA

    Anuani: P O BOX 5 SINGIDA

    Simu: 2502170, 2502089

    Simu: 2502170, 2502089

    Barua Pepe: info@singida.go.tz ras@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Usiri
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

Copyright ©2023 Singida Regional Commisioner' Office . All rights reserved.