• Wasiliana Nasi |
    • Malalamiko |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
    • Blog |
Singida Regional Website

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Tovuti ya Mkoa wa Singida

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na dhima
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Ikungi
      • HISTORIA
    • Iramba
    • Manyoni
    • Mkalama
    • Singida
  • Halmashauri
    • H/W Ikungi
    • H/W Iramba
    • H/W Itigi
    • H/W Manyoni
    • H/W Mkalama
    • H/W Singida
    • H/M Singida
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Viwanda na Biashara
    • Madini
  • Huduma Zetu
    • Afya
      • Madaktari Bingwa
      • Huduma za Tiba
      • Huduma za Kinga
      • Ustawi wa Jamii
      • Afya ya Mazingira
      • Lishe
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba Wa Huduma Kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
    • Investment Guide
  • Kituo Cha Habari
    • Picha
    • Video
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma

UFADHILI MAFUNZO YA UFUNDI STADI,KUWAINUA VIJANA KATIKA KILIMO

Posted on: January 27th, 2026

Serikali kwa kushirikiana na Tanzania Agricultural Modernization Association (TAMA) na Mamlaka ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi (VETA) leo imetambulisha rasmi Mradi wa YEFFA ambapo ni mradi wenye lengo la kuwawezesha vijana kushiriki kikamilifu katika kilimo cha kisasa kupitia mafunzo ya ufundi stadi, ajira na ujasiriamali. Mradi huu, unatekelezwa na Tanzania Agricultural Modernization Association (TAMA) kwa kushirikiana na Mamlaka ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi (VETA) na kufadhiliwa na Shirika la AGRA.

Hayo yamejiri wakati wa kikao maalum cha kuutambulisha mradi huo kilichofanyika katika Ukumbi wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Singida Januari 27,2026 na kuwashirikisha wadau mbali mbali wakiwemo Viongozi wa Dini,Maafisa Mipango, wadau wa elimu na wengineo kwa lengo la Kwenda kuwa mabalozi wa kuutambulisha mradi huo kwa jamii.

Akizungumza wakati akitoa wasilisho katika  kikao hicho, Bw. Frank Shinge ambaye ni  Afisa Ufuatiliaji na Tathmini mradi wa YEFFA ,amesema kuwa mradi huo unalenga kuwajengea uwezo vijana kupitia mafunzo ya ufundi stadi katika uendeshaji na matengenezo ya mitambo ya kilimo, mifumo ya umwagiliaji pamoja na usindikaji wa mazao.

“ Mradi huu unatekelezwa katika mikoa ya Singida, Tabora, Dodoma na Manyara, na unafadhiliwa na Shirika la AGRA huku Utekelezaji wake ulianza mwezi Novemba 2025 na unatarajiwa kukamilika mwezi Oktoba 2027.’’

Kupitia mradi huu, jumla ya vijana 1,525 watanufaika moja kwa moja na mafunzo ya kiufundi, ambapo asilimia 70 wanatarajiwa kuwa wanawake, huku vijana 130 wenye mahitaji maalumu wakijumuishwa kikamilifu katika mpango huu. Kupitia vijana hawa, zaidi ya wakulima wadogo 32,500 watanufaika kwa kupata huduma za mitambo ya kilimo, hali itakayoongeza uzalishaji, ufanisi na ubora wa shughuli za kilimo.

Bw.Frank alisema kuwa YEFFA ni chachu ya mabadiliko katika sekta ya kilimo kwa kuwa itawapa vijana ujuzi wa vitendo unaohitajika katika soko la ajira na kuwawezesha kujiajiri au kuajiriwa. Aliongeza kuwa mradi huu unakuja wakati muafaka wa kuimarisha kilimo cha kisasa na chenye tija katika mkoa wa Singida na maeneo ya jirani.

Kadhalika Katika kuhakikisha mradi unakuwa jumuishi na unaowafikia vijana wote, waandaaji wa YEFFA wamesema kuwa  wamejipanga  vizuri zaidi kuwapokea vijana wenye mahitaji maalumu kwa kuwaandalia mazingira rafiki ya ujifunzaji. Ambapo wameweka mikakati ya kuhakikisha upatikanaji wa nukta nundu kwa wasioona, njia zinazopitika kwa walemavu wa viungo pamoja na matumizi ya lugha ya alama kwa wanafunzi wasiosikia na wasioweza kuzungumza, ili kila kijana apate fursa sawa ya kushiriki kikamilifu katika mafunzo.

Akizungumzia katika suala la  utekelezaji, Bw.Bura chepa Mratibu wa Mradi wa YEFFA kwa upande wa VETA,amesema kuwa VETA itakuwa na jukumu la kutoa mafunzo ya kiufundi kwa vijana, huku TAMA ikisimamia uratibu wa mradi, ufuatiliaji na tathmini pamoja na kuwaunganisha wahitimu na fursa za ajira na ujasiriamali katika sekta ya kilimo cha kisasa.

Mradi wa YEFFA pia unatarajiwa kusaidia kuanzishwa kwa biashara 600 zinazoendeshwa na vijana, kutoa fursa 600 za mafunzo ya vitendo pamoja na kuwezesha takribani vijana 6,500 kupata ajira au kujiajiri kupitia mbinu ya mafunzo ya wawezeshaji kwa wenzao. Kupitia jitihada hizi, YEFFA unatarajiwa kuwa chachu ya maendeleo ya kilimo chenye tija, ushindani na ujumuishi nchini Tanzania.

Mgeni rasmi wa hafla hiyo,Bw.Somboi Harold ambaye  ni Afisa Kilimo wa Mkoa wa Singida Amezungumza wakati wa kufunga kikao akiwasisitiza washiriki wa kikao hicho kuhakikisha wanakwenda kuwa mabalozi wazuri kwa jamii katika kuhakikisha wanapeleka taarifa hizi njema kwa walengwa ili waweze kunufaika na fursa hiyo ambayo itakwenda kuwa chachu ya maendeleo kwa vijana,wanawake na watu wenye mahitaji maalumu kwa kupata mafunzo bora.

Alisisitiza kuwa mradi huo ni hatua muhimu katika kubadili taswira ya kilimo kwa vijana na kuongeza ajira katika Ukanda wa Kati wa Tanzania.

Matangazo

  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2022_2023 SINGIDA RS July 01, 2022
  • MAJINA YA WALIOCHANGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA - 2023, MKOA WA SINGIDA December 14, 2022
  • TAARIFA YA MAPOKEZI YA FEDHA KWA KIPINDI CHA KUANZIA JULAI HADI OCTOBA, 2023 KWA AJILI YA UTEKELEZAJI WA SHUGHULI ZA MAENDELEO November 01, 2023
  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2021/2022 SINGIDA RS - GPN 2021 - 2022 July 01, 2021
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • RAS DKT.MGANGA AAGIZA MIRADI KUKAMILISHWA KWA WAKATI.

    January 26, 2026
  • UFADHILI MAFUNZO YA UFUNDI STADI,KUWAINUA VIJANA KATIKA KILIMO

    January 27, 2026
  • MALIGHAFI ZAIDI ZAHITAJIKA ILI KUINUA VIWANDA MKOANI SINGIDA

    January 22, 2026
  • MADIWANI WATAKIWA KUSIMAMIA MIRADI,MAPATO NA NIDHAMU KWA WATUMISHI

    January 15, 2026
  • Angalia Zote

Video

Mkoa wa Singida waja na Mikakati ya Kuboresha Elimu
Video zaidi

Viungio vya Haraka

  • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
  • Mwongozo wa Matumizi ya TEHAMA Serikalini
  • Fomu ya Maombi ya Kusafiri Nje ya Nchi
  • MPANGO WA MANUNUZI MKOA WA SINGIDA
  • KUONA AJIRA ZA WAALIMU WA SAYANSI NA MAFUNDI SANIFU

Tovuti Muhimu

  • UTUMISHI
  • TAMISEMI
  • IKULU
  • WIZARA YA ELIMU
  • NECTA
  • WIZARA YA AFYA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Ramani ya Mkoa

Wasiliana Nasi

    SINGIDA

    Anuani: P O BOX 5 SINGIDA

    Simu: 2502170, 2502089

    Simu: 2502170, 2502089

    Barua Pepe: info@singida.go.tz ras@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Usiri
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

Copyright ©2023 Singida Regional Commisioner' Office . All rights reserved.