• Wasiliana Nasi |
    • Malalamiko |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
    • Blog |
Singida Regional Website

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Tovuti ya Mkoa wa Singida

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na dhima
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Ikungi
      • HISTORIA
    • Iramba
    • Manyoni
    • Mkalama
    • Singida
  • Halmashauri
    • H/W Ikungi
    • H/W Iramba
    • H/W Itigi
    • H/W Manyoni
    • H/W Mkalama
    • H/W Singida
    • H/M Singida
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Viwanda na Biashara
    • Madini
  • Huduma Zetu
    • Afya
      • Madaktari Bingwa
      • Huduma za Tiba
      • Huduma za Kinga
      • Ustawi wa Jamii
      • Afya ya Mazingira
      • Lishe
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba Wa Huduma Kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
    • Investment Guide
  • Kituo Cha Habari
    • Picha
    • Video
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma

RAS DKT.MGANGA AAGIZA MIRADI KUKAMILISHWA KWA WAKATI.

Posted on: January 26th, 2026

Katibu Tawala wa Mkoa wa Singida, Dkt. Fatuma Mganga, ameongoza timu ya ukaguzi wa miradi ya maendeleo kufanya ziara ya kikazi katika Halmashauri ya Wilaya ya Itigi leo tarehe 26 Januari 2026, kwa lengo la kukagua utekelezaji wa miradi ya elimu na afya na kuhakikisha matumizi sahihi ya fedha za umma.

Katika ziara hiyo, Dkt. Mganga alikagua miradi mbalimbali ikiwemo ujenzi wa Zahanati ya Kitongoji cha Mlongoji, unaotekelezwa kwa ushirikiano kati ya Serikali na wananchi. Serikali Kuu imetoa Tsh 50,000,000 kwa ajili ya umaliziaji wa zahanati hiyo, huku wananchi wakichangia Tsh 2,614,000, wadau Tsh 2,750,000 na nguvu kazi yenye thamani ya Tsh 1,250,000. Aidha, Mfuko wa Jimbo ulitoa Tsh 10,000,000. Hadi sasa, jumla ya Tsh 13,437,815.51 tayari imetumika.

Ziara hiyo pia ilihusisha ukaguzi wa miradi ya elimu ikiwemo ujenzi wa vyumba vinne vya madarasa katika Shule ya Msingi Kitaraka unaofadhiliwa kupitia Programu ya BOOST kwa gharama ya Tsh 92,000,000, ambapo hadi sasa Tsh 69,055,299 tayari zimetumika. Mradi huo unatarajiwa kunufaisha wanafunzi 667. Katika Shule ya Msingi Kazikazi, kamati ilikagua ujenzi wa madarasa ya awali na msingi pamoja na matundu ya vyoo, mradi unaogharimu Tsh 120,000,000 kupitia Programu ya BOOST.

Ukaguzi huo ulihitimishwa katika mradi wa ujenzi wa Shule mpya ya Msingi ya Kijobolo iliyopo Kitongoji cha Milumbi, unaotekelezwa kwa ushirikiano wa Serikali na wananchi. Mradi huo umefadhiliwa na michango ya wananchi, Mfuko wa Jimbo, Halmashauri ya Wilaya ya Itigi na Programu ya BOOST kwa jumla ya zaidi ya Tsh 300,000,000, ambapo hadi sasa zaidi ya Tsh 214,000,000 tayari zimetumika.

Akizungumza wakati wa ziara hiyo, Dkt. Fatuma Mganga aliwataka wazazi na viongozi wa maeneo husika kuhakikisha watoto wote wanapata haki yao ya msingi ya elimu na kushiriki kikamilifu katika programu za lishe shuleni. Alisisitiza umuhimu wa ufuatiliaji wa karibu wa miradi ili kuhakikisha inakamilika kwa wakati, kwa viwango vinavyokubalika na kwa kuzingatia thamani ya fedha.

Ziara hiyo ni sehemu ya mkakati wa Mkoa wa Singida wa kufuatilia utekelezaji wa miradi ya maendeleo na kuboresha utoaji wa huduma za kijamii kwa wananchi.

Matangazo

  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2022_2023 SINGIDA RS July 01, 2022
  • MAJINA YA WALIOCHANGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA - 2023, MKOA WA SINGIDA December 14, 2022
  • TAARIFA YA MAPOKEZI YA FEDHA KWA KIPINDI CHA KUANZIA JULAI HADI OCTOBA, 2023 KWA AJILI YA UTEKELEZAJI WA SHUGHULI ZA MAENDELEO November 01, 2023
  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2021/2022 SINGIDA RS - GPN 2021 - 2022 July 01, 2021
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • RAS DKT.MGANGA AAGIZA MIRADI KUKAMILISHWA KWA WAKATI.

    January 26, 2026
  • UFADHILI MAFUNZO YA UFUNDI STADI,KUWAINUA VIJANA KATIKA KILIMO

    January 27, 2026
  • MALIGHAFI ZAIDI ZAHITAJIKA ILI KUINUA VIWANDA MKOANI SINGIDA

    January 22, 2026
  • MADIWANI WATAKIWA KUSIMAMIA MIRADI,MAPATO NA NIDHAMU KWA WATUMISHI

    January 15, 2026
  • Angalia Zote

Video

Mkoa wa Singida waja na Mikakati ya Kuboresha Elimu
Video zaidi

Viungio vya Haraka

  • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
  • Mwongozo wa Matumizi ya TEHAMA Serikalini
  • Fomu ya Maombi ya Kusafiri Nje ya Nchi
  • MPANGO WA MANUNUZI MKOA WA SINGIDA
  • KUONA AJIRA ZA WAALIMU WA SAYANSI NA MAFUNDI SANIFU

Tovuti Muhimu

  • UTUMISHI
  • TAMISEMI
  • IKULU
  • WIZARA YA ELIMU
  • NECTA
  • WIZARA YA AFYA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Ramani ya Mkoa

Wasiliana Nasi

    SINGIDA

    Anuani: P O BOX 5 SINGIDA

    Simu: 2502170, 2502089

    Simu: 2502170, 2502089

    Barua Pepe: info@singida.go.tz ras@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Usiri
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

Copyright ©2023 Singida Regional Commisioner' Office . All rights reserved.