• Wasiliana Nasi |
    • Malalamiko |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
    • Blog |
Singida Regional Website

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Tovuti ya Mkoa wa Singida

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na dhima
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Ikungi
      • HISTORIA
    • Iramba
    • Manyoni
    • Mkalama
    • Singida
  • Halmashauri
    • H/W Ikungi
    • H/W Iramba
    • H/W Itigi
    • H/W Manyoni
    • H/W Mkalama
    • H/W Singida
    • H/M Singida
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Viwanda na Biashara
    • Madini
  • Huduma Zetu
    • Afya
      • Madaktari Bingwa
      • Huduma za Tiba
      • Huduma za Kinga
      • Ustawi wa Jamii
      • Afya ya Mazingira
      • Lishe
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba Wa Huduma Kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
    • Investment Guide
  • Kituo Cha Habari
    • Picha
    • Video
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma

CHANGAMOTO ZA KIFEDHA KUTAFUTIWA UTATUZI SINGIDA*

Posted on: December 2nd, 2024

Benki Kuu ya Tanzania (BoT) imesema asilimia 10 tu ya watu wazima mkoani Singida ndio wanaotumia huduma za benki kiwango ambacho kipo chini ukilinganisha na kiwango cha kitaifa ambacho ni asilimia 22.

Kaimu Meneja msaidizi sera na chambuzi za huduma za kifedha kutoka BoT, Edmund Mbokosi alisena hayo Leo katika kikao cha kujadili changamoto za kifedha na utatuzi wake Mkoa wa Singida ambacho kimewashirikisha Wakuu wa Wilaya, Wakurugenzi wa Halmashauri na mameneja wa benki zinazotoa huduma za kifedha mkoani hapa.

Amesema katika huduma za kifedha Mkoa wa Singida wanatumia asilimia 50 wakati wastani wa kitaifa ni asilimia 72,bima ni asilimia 5,huduma za vyama vya kuweka na kukopa (SACCOS) Singida ni asilimia 7 wakati lengo la kitaifa ni asilimia 12.

Mbokosi amesema kutokana na changamoto hiyo BoT imemua kuja kutoa elimu ili kuangalia namna ya kuweza kupandisha kiwango cha matumizi ya huduma za kifedha katika mkoa wa Singida kwa lengo la kuufanya mkoa kupanda kiuchumi na kuondoka katika nafasi ya tatu kutoka mwisho.

Naye Mkuu wa Mkoa wa Singida,Halima Dendego, amesema mkoa utajitathimini kwenye sensa kwa kupita kwenye maeneo mbalimbali kama kwa wanafunzi mashuleni na vyuo vilivyopo mkoani hapa ili kupandisha kiwango cha huduma za benki.

"Tuna vyuo vingi na taasisi nyingi na karibia kila mtu anatakiwa kulipwa pesa kupitia benki na hivi sasa kuna huduma mpya mfano ya mfumo wa stakabadhi ghalani kwa hiyo nina imani kiwango acha asilimia 72 cha huduma za kifedha tutakifikia," alisema. Ok Google

Awali Mchambuzi Maswala ya fedha kutoka BoT, Michael Mwaituka, alisema BoT imejipanga kuwasaidia wajasiriamali nchini kupitia Mfuko wa Udhamini wa Mikopo kwa ajili ya Mauzo Nje ya Nchi (ECGS) pamoja Mfuko wa Udhamini wa Mikopo kwa Wajasiriamali Wadogo na wa Kati (SME-CGS).

Amesema lengo la kuwezesha sekta binafsi wenye miradi mizuri kuweza kupata mitaji kutoka kwenye mabenki na taasisi za fedha zilizosajiliwa chini na Sheria ya Benki na Taasisi za Fedha 2006, pale wanapokuwa na upungufu wa dhamana.

Mwaituka amesema  kuwa BoT wanasimamia Mfuko wa Udhamini wa Mkopo kwa niaba ya serikali ili kuwasaidia watanzania kupata mitaji kuongeza uzalishaji, ajira, fedha za kigeni na pato la Taifa kwa ujumla.

Amesema  kuwa Mfuko wa Udhamini wa Mikopo kwa Wajasiriamali Wadogo na wa kati una lengo la kuwawezesha wajasiriamali wadogo na wa kati wenye miradi mizuri lakini wana upungufu wa dhamana, kuweza kupata mitaji kutoka kwenye mabenki na taasisi za fedha zinazosimamiwa na Benki Kuu.






Matangazo

  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2022_2023 SINGIDA RS July 01, 2022
  • MAJINA YA WALIOCHANGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA - 2023, MKOA WA SINGIDA December 14, 2022
  • TAARIFA YA MAPOKEZI YA FEDHA KWA KIPINDI CHA KUANZIA JULAI HADI OCTOBA, 2023 KWA AJILI YA UTEKELEZAJI WA SHUGHULI ZA MAENDELEO November 01, 2023
  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2021/2022 SINGIDA RS - GPN 2021 - 2022 July 01, 2021
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • IKUNGI YAPEPERUSHA BENDERA KWA MIRADI YA KIMKAKATI.

    May 08, 2025
  • DKT.MGANGA ASISITIZA MADAKTARI BINGWA KUTOA HUDUMA BORA

    May 05, 2025
  • WATUMISHI NA WAAJIRI HODARI MKOANI SINGIDA WAPOKEA TUZO

    May 02, 2025
  • KUELEKEA MEIMOSI,RC DENDEGO ATANGAZA FURSA ZA UWEKEZAJI

    April 25, 2025
  • Angalia Zote

Video

Mkoa wa Singida waja na Mikakati ya Kuboresha Elimu
Video zaidi

Viungio vya Haraka

  • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
  • Mwongozo wa Matumizi ya TEHAMA Serikalini
  • Fomu ya Maombi ya Kusafiri Nje ya Nchi
  • MPANGO WA MANUNUZI MKOA WA SINGIDA
  • KUONA AJIRA ZA WAALIMU WA SAYANSI NA MAFUNDI SANIFU

Tovuti Muhimu

  • UTUMISHI
  • TAMISEMI
  • IKULU
  • WIZARA YA ELIMU
  • NECTA
  • WIZARA YA AFYA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Ramani ya Mkoa

Wasiliana Nasi

    SINGIDA

    Anuani: P O BOX 5 SINGIDA

    Simu: 2502170, 2502089

    Simu: 2502170, 2502089

    Barua Pepe: info@singida.go.tz ras@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Usiri
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

Copyright ©2023 Singida Regional Commisioner' Office . All rights reserved.