• Wasiliana Nasi |
    • Malalamiko |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
    • Blog |
Singida Regional Website

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Tovuti ya Mkoa wa Singida

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na dhima
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Ikungi
      • HISTORIA
    • Iramba
    • Manyoni
    • Mkalama
    • Singida
  • Halmashauri
    • H/W Ikungi
    • H/W Iramba
    • H/W Itigi
    • H/W Manyoni
    • H/W Mkalama
    • H/W Singida
    • H/M Singida
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Viwanda na Biashara
    • Madini
  • Huduma Zetu
    • Afya
      • Madaktari Bingwa
      • Huduma za Tiba
      • Huduma za Kinga
      • Ustawi wa Jamii
      • Afya ya Mazingira
      • Lishe
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba Wa Huduma Kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
    • Investment Guide
  • Kituo Cha Habari
    • Picha
    • Video
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma

"Endeleeni kuandaa mashamba mbolea inakuja"- Serukamba.

Posted on: November 28th, 2022

Mkuu wa Mkoa wa Singida Peter Serukamba amewataka Wakulima Mkoani Singida kuendelee kuandaa mashamba kwa ajili ya kilimo wakati Serikali ikiendelea na mchakato wa kuleta mbolea ya kutosha katika Wilaya mbalimbali.

Kauli hiyo ameitoa leo katika Kikao kilichofanyika katika ukumbi wa mikutano wa Ofisi hiyo ambacho  kiliwakutanisha Wakuu wa Wilaya, Wakurungenzi na Maafisa kilimo wa Halmashauri zote Mkoani lengo likiwa ni kujadili changamoto mbalimbali ikiwemo upatikanaji wa mbolea, Maandalizi ya mashamba darasa na mashamba darasa pamoja na changamoto za wadaiwa.  

RC Serukamba amewataka wakulima kuendelea na maandalizi ya msimu wa kilimo kwa kuwa swala la upatikanaji wa mbolea linashughulikiwa na viongozi wa Serikali kuhakikisha mbolea inamfikia kila mkulima huku akiwataka Wakuu wa Wilaya kuendelea kuwakumbusha wahusika mara kwa mara.

Awali akichangia mada juu ya hali ya upatikanaji wa mbolea Mkuu wa Wilaya ya Singida Mhandisi Paskasi Muragili amesema Wakulima wa Wilaya yake wana uhitaji mkubwa wa mbolea kwa ajili ya Kilimo hivyo zifanyike juhudi mbalimbali kuhakikisha Mawakala wanaleta mbolea ya kutosha kwa wakati.

Aidha Muragili ameeleza kwamba uwezo wa Mawakala kununua kiasi kikubwa cha mbolea ni mdogo jambo ambalo limesababisha hofu kwa Wakulima kukosa mbolea wakati msimu ukiwa umekaribia.

Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya ya Ikungi Jerry Muro, ameeleza kwamba Wilaya hiyo mpaka sasa hakuna mbolea iliyoingia jambo ambalo limekuwa likilalamikiwa na Wakulima.

Jerry ameeleza kwamba Wakulima Wilayani hapo walishakamilisha maandalizi ya msimu wa kilimo kwa kupata mbegu na kusafisha mashamba jambo lililobaki ni kuwa na uhakika wa mbolea tu alieleza.

Mkuu wa Wilaya ya Iramba Suleimani Mwenda, akizungumza wakati wa kikao hicho.

Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya ya Iramba Suleimani Mwenda, amesema wao wameweza kupata mbolea kwa kiasi kikubwa kwa sababu wakulima walikuwa tayari wameshachanga fedha hivyo kuwafanya wa mawakala wa mbolea kupata kushawishika zaidi.

Amesema kununua Mawakala wengi hawana mtaji mkubwa hivyo wakihakikishiwa fedha wanaweza kuleta eneo lolote ili waweze kupata fedha na kuagiza mzigo mwingine.

Akihitimisha mjadala huo Mkuu wa Mkoa amesema Serikali ipo makini katika zoezi la usambazaji wa mbolea ili kuepusha uvushaji wa mbolea hiyo kwenda nje ya nchi kwa kuwa imeweka fedha nyingi za ruzuku.

Mwisho

Matangazo

  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2022_2023 SINGIDA RS July 01, 2022
  • MAJINA YA WALIOCHANGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA - 2023, MKOA WA SINGIDA December 14, 2022
  • TAARIFA YA MAPOKEZI YA FEDHA KWA KIPINDI CHA KUANZIA JULAI HADI OCTOBA, 2023 KWA AJILI YA UTEKELEZAJI WA SHUGHULI ZA MAENDELEO November 01, 2023
  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2021/2022 SINGIDA RS - GPN 2021 - 2022 July 01, 2021
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • HUDUMA ZA KIBINGWA ZAWAFIKIA WAGONJWA ZAIDI YA 3000 SINGIDA.

    May 09, 2025
  • IKUNGI YAPEPERUSHA BENDERA KWA MIRADI YA KIMKAKATI.

    May 08, 2025
  • DKT.MGANGA ASISITIZA MADAKTARI BINGWA KUTOA HUDUMA BORA

    May 05, 2025
  • WATUMISHI NA WAAJIRI HODARI MKOANI SINGIDA WAPOKEA TUZO

    May 02, 2025
  • Angalia Zote

Video

Mkoa wa Singida waja na Mikakati ya Kuboresha Elimu
Video zaidi

Viungio vya Haraka

  • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
  • Mwongozo wa Matumizi ya TEHAMA Serikalini
  • Fomu ya Maombi ya Kusafiri Nje ya Nchi
  • MPANGO WA MANUNUZI MKOA WA SINGIDA
  • KUONA AJIRA ZA WAALIMU WA SAYANSI NA MAFUNDI SANIFU

Tovuti Muhimu

  • UTUMISHI
  • TAMISEMI
  • IKULU
  • WIZARA YA ELIMU
  • NECTA
  • WIZARA YA AFYA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Ramani ya Mkoa

Wasiliana Nasi

    SINGIDA

    Anuani: P O BOX 5 SINGIDA

    Simu: 2502170, 2502089

    Simu: 2502170, 2502089

    Barua Pepe: info@singida.go.tz ras@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Usiri
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

Copyright ©2023 Singida Regional Commisioner' Office . All rights reserved.