• Wasiliana Nasi |
    • Malalamiko |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
    • Blog |
Singida Regional Website

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Tovuti ya Mkoa wa Singida

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na dhima
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Ikungi
      • HISTORIA
    • Iramba
    • Manyoni
    • Mkalama
    • Singida
  • Halmashauri
    • H/W Ikungi
    • H/W Iramba
    • H/W Itigi
    • H/W Manyoni
    • H/W Mkalama
    • H/W Singida
    • H/M Singida
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Viwanda na Biashara
    • Madini
  • Huduma Zetu
    • Afya
      • Madaktari Bingwa
      • Huduma za Tiba
      • Huduma za Kinga
      • Ustawi wa Jamii
      • Afya ya Mazingira
      • Lishe
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba Wa Huduma Kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
    • Investment Guide
  • Kituo Cha Habari
    • Picha
    • Video
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma

Jiungeni katika vikundi ili mkopesheke - DC Muragili

Posted on: January 28th, 2022

Wafanyabiashara wadogo Manispaa ya Singida wameshauriwa kujiunga katika vikundi vya wajasiriamali na kuvisajili ili waweze kukopesheka katika taasisi mbalimbali za fedha.

Ushauri huo umetolewa leo Januari 28, 2022 na Mkuu wa Wilaya ya Singida Mhandisi Paskasi Muragili wakati alipokutana na wafanyabiashara wadogo katika soko la wamachinga la Kata ya Majengo katika Manispaa hiyo alipokuwa akikabidhi fedha kiasi cha Tsh. 2,000,000 kwa niaba ya Mkuu wa mkoa huo .

Mhandisi Muragili amesema namna pekee ambayo vijana wataweza kupata mitaji kwa ajili ya kuendesha maisha yao ni kujiunga katika vikundi ili waweze kuaminiwa na kukopesheka.

Aidha DC Muragili amebainisha kwamba mabenki mbalimbali hapa Singida yakiwemo CRDB, NMB NBC na nyinginezo wameonesha utayari wa kuvikopesha vikundi ambavyo vimesajiliwa hivyo kuwataka vijana kujiunga ambapo Maafisa Maendeleo ya Jamii kusaidia utoaji wa miongozo mbalimbali kufanikisha zoezi hilo.

Mkuu wa Wilaya ya Singida Mhandisi Paskasi Muragili (mwenye suti) wakati alipokutana na wafanyabiashara wadogo katika soko la wamachinga la Kata ya Majengo katika Manispaa ya Singida. Wa kwanza kutoka kushoto ni Meya wa Manispaa ya Singida Yagi Maulid Kiaratu.

Amewakumbusha vijana wenye umri kati ya miaka 18 mpaka 35 kutumia fursa ya mikopo ya vijana asilimia nne(4%) inayotolewa na Halmashauri kwa kuwa ina mashart nafuu na haina riba.

Akitoa salamu za Mkuu wa Mkoa mbele ya wafanyabiashara hao (wamachinga) DC Paskasi amesema kiasi hicho cha fedha kimetolewa kwa ajili ya ununuzi wa vifaa vya usafi kama ambavyo alivyotoa ahadi hiyo alipokutana nao tarehe 06/11 mwaka jana.

Ununuzi wa vifaa hivyo ni sehemu ya utekelezaji wa maagizo ya Mkuu wa Mkoa ya kufanya usafi kila jumamosi  katika maeneo yanayowazunguka ili kuepuka magonjwa ya milipuko alibainisha DC Muragili.

Katika hatua nyingine Mhandisi Paskasi  akawakabidhi fedha Tsh. 1,000,000 (Milioni moja ) kupitia kwa mwenyekiti wa Vijana Mtaa wa Majengo  Saidi Hassani kama sehemu ya ahadi ya mkuu wa Mkoa juu ya uboreshaji wa eneo lao la uoshaji wa magari.

DC akatumia muda huo kuwaasa vijana wote kutumia fedha hizo kwa malengo mahususi ili ziweze kuleta chachu katika biashara zao, na zisaidie kuibua miradi mipya ya maendeleo.

Sambamba na hilo DC Muragili akakabidhi shilingi milioni mbili(2,000,000) wa diwani wa Unyianga kwa ajili ya ujenzi wa kituo cha afya Unyianga ikiwa ni muendelezo wa kukamilisha ahadi alizozitoa kwa wanachi.

Kwa upande wake Meya wa Manispaa ya Singida Yagi Maulid Kiaratu amemshukuru Mkuu wa Mkoa huo kwa kutekeleza ahadi zake katika vikundi vilivyopo Kata ya Majengo na Kituo cha Afya Unyianga.

Meya huyo amewasihi Maafisa Maendeleo ya jamii ngazi ya wilaya kuendelea kufanya kazi kwa ukaribu na wafanyabiashara hao ili kusaidia kutambua fursa ambazo zinawazunguka .

Kwa pamoja viongozi hao wakatoa wito kwa wananchi kushiriki kikamilifu katika zoezi la upandaji miti litakalozindiuliwa ki mkoa jumamosi tarehe 29.01.2022 katika kingo za ziwa Kindai ili kurejesha mazingira ya ukijani mkoani Singida.

Baada ya uzinduzi huo kila mwananchi atatakiwa kupanda miti katika maeneo wanayoishi na maeneo ya mipaka ya mashamba yao kwa nyakati tofauti aliendelea kueleza Dc Muragili.

DC Muragili akikabidhi shilingi milioni mbili (2,000,000) kwa Diwani wa Unyianga kwa ajili ya ujenzi wa kituo cha afya Unyianga ikiwa ni muendelezo wa kukamilisha ahadi alizozitoa Mkuu wa Mkoa wa Singida Dkt. Binilith Mahenge kwa wanachi.

Meya wa Manispaa ya Singida Yagi Maulid Kiaratu akizungumza kabla ya kumkaribisha mgeni rasmi Mheshimiwa Mkuu wa Wilaya ya Singida Mhandisi Paskasi Muragili  

Mtendaji wa Kata ya Majengo akisoma taarifa kwa Mheshimiwa Mkuu wa Wilaya ya Singida kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa huo wakati wa hafla ya utekelezaji wa ahadi ya Mkuu wa Mkoa kwa vijana 

Baadhi ya watendaji na vijana wa Kata ya Majengo wakati wa hafla ya utekelezaji wa ahadi ya Mkuu wa Mkoa wa Singida Dkt. Binilith Mahenge kwa vijana hao.

Mwisho

Matangazo

  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2022_2023 SINGIDA RS July 01, 2022
  • MAJINA YA WALIOCHANGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA - 2023, MKOA WA SINGIDA December 14, 2022
  • TAARIFA YA MAPOKEZI YA FEDHA KWA KIPINDI CHA KUANZIA JULAI HADI OCTOBA, 2023 KWA AJILI YA UTEKELEZAJI WA SHUGHULI ZA MAENDELEO November 01, 2023
  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2021/2022 SINGIDA RS - GPN 2021 - 2022 July 01, 2021
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • HUDUMA ZA KIBINGWA ZAWAFIKIA WAGONJWA ZAIDI YA 3000 SINGIDA.

    May 09, 2025
  • IKUNGI YAPEPERUSHA BENDERA KWA MIRADI YA KIMKAKATI.

    May 08, 2025
  • DKT.MGANGA ASISITIZA MADAKTARI BINGWA KUTOA HUDUMA BORA

    May 05, 2025
  • WATUMISHI NA WAAJIRI HODARI MKOANI SINGIDA WAPOKEA TUZO

    May 02, 2025
  • Angalia Zote

Video

Mkoa wa Singida waja na Mikakati ya Kuboresha Elimu
Video zaidi

Viungio vya Haraka

  • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
  • Mwongozo wa Matumizi ya TEHAMA Serikalini
  • Fomu ya Maombi ya Kusafiri Nje ya Nchi
  • MPANGO WA MANUNUZI MKOA WA SINGIDA
  • KUONA AJIRA ZA WAALIMU WA SAYANSI NA MAFUNDI SANIFU

Tovuti Muhimu

  • UTUMISHI
  • TAMISEMI
  • IKULU
  • WIZARA YA ELIMU
  • NECTA
  • WIZARA YA AFYA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Ramani ya Mkoa

Wasiliana Nasi

    SINGIDA

    Anuani: P O BOX 5 SINGIDA

    Simu: 2502170, 2502089

    Simu: 2502170, 2502089

    Barua Pepe: info@singida.go.tz ras@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Usiri
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

Copyright ©2023 Singida Regional Commisioner' Office . All rights reserved.