• Wasiliana Nasi |
    • Malalamiko |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
    • Blog |
Singida Regional Website

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Tovuti ya Mkoa wa Singida

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na dhima
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Ikungi
      • HISTORIA
    • Iramba
    • Manyoni
    • Mkalama
    • Singida
  • Halmashauri
    • H/W Ikungi
    • H/W Iramba
    • H/W Itigi
    • H/W Manyoni
    • H/W Mkalama
    • H/W Singida
    • H/M Singida
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Viwanda na Biashara
    • Madini
  • Huduma Zetu
    • Afya
      • Madaktari Bingwa
      • Huduma za Tiba
      • Huduma za Kinga
      • Ustawi wa Jamii
      • Afya ya Mazingira
      • Lishe
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba Wa Huduma Kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
    • Investment Guide
  • Kituo Cha Habari
    • Picha
    • Video
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma

Kazi ya Kiongozi ni kutatua changamoto za Wananchi - RC Mahenge

Posted on: May 31st, 2022

Wakuu wa Idara katika Halmashauri ya Wilaya ya Mkalama wametakiwa kufanya kazi kwa kushirikiana na kufuata taratibu za kazi ambazo ndizo zitakazoleta mafanikio ambapo wamekumbushwa kwamba  lengo la uwepo wao ni kuwaletea maendeleo wananchi husika na sio vinginevyo.

Kauli hiyo imetolewa leo na Mkuu wa Mkoa wa Singida Dkt. Binilith Mahenge alipokutana na kufanya kikako cha pamoja na viongozi mbalimbali wakiwemo wakuu wa Idara katika ukumbi wa  Halmashauri hiyo ambapo alielekeza Watumishi kufuata taratibu za utumishi katika utekelezaji wa majukumu yao ya kila siku na kufanya kazi kwa kushirikiana.

RC Mahenge amesema pamoja na kwamba Wilaya ya Mkalama inafanya kazi nzuri ya makusanyo ya mapato lakini bado kuna changamoto  zinazosabishwa na usimamizi usioridhisha hivyo kuwataka wakuu wa Idara kuhakikisha wanashirikiana ili kuondoa changamoto za miundombinu ya Barabara, Elimu, Afya, Amani na usalama pamoja na kuhakikisha maendeleo yanatamalaki Wilayani hapo.

Mkuu wa Mkoa wa Singida Dkt. Binilith Mahenge akizungumza na Watumishi wakati wa kikao hicho.

Hata hivyo Dkt. Mahenge amewapongeza Viongozi wa Wilaya hiyo kwa hatua ambazo wamezifikia katika kutatua changamoto ndogondogo za migogoro ya mipaka katika baadhi ya maeneo katika Kata ya Mwangezi  wanapoishi jamii ya wahazabe na kuwataka kufikia mufaka kwa njia ya majadiliano ili kuhakikisha Amani inaendelea kutawala maeneo hayo.

Awali akitoa taarifa ya moja ya eneo lenye changamoto ya migogoro wa Mipaka Diwani wa Kata ya Mwangeza ambaye pia ni Makamu Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Mkalama Bosco Charles Samweli amesema Kata yake imekuwa na changamoto ya migogoro ya mpaka baina ya watu jamii ya Wahazabe na wengine wa Mkoa wa Arusha na Manyara jambo ambalo halina Afya nzuri kwa Amani ya Kata hiyo.

Ameiomba Serikali kuendeleza juhudi zake za kutatua changamoto hiyo ambapo shughuli za maendeleo kwa jamii hizo zimesimama wakisubiri majadiliano yanayoendelea baina ya viongozi wa mikoa hiyo.

Aidha Diwani ameomba msaada wa haraka kwa wataalamu wa wanyamapori ili kusaidia kuondoa changamoto ya uvamizi unaofanywa na wanyama pori wakiwemo Tembo na Simba katika mashamba ya wanakijiji ambapo mashamba yao yamekuwa yakiharibiwa na Serikali ilishindwa kulipa fidia kwa wakulima hao.

Mkuu wa Wilaya ya Mkalama Sophia Kizigo akizungumza na Watumishi wakati wa kikao hicho.

Akitolea majibu changamoto hiyo Mkuu wa Wilaya ya Mkalama Sophia Kizigo amesema Serikali hailipi fidia kwa wakulima bali inalipa  kiasi kidogo cha kifuta machozi au pole kwa walikutwa na dhahama ya kuvamiwa na wanyama na kuharibiwa kwa mazao yao.

DC Kizigo amesema kwamba tayari mawasiliano yameshaanza kufanyika ili kusaidia kuwapangia kazi hiyo  wataalamu wa wanyamapori ili kukabiliana na changamoto hiyo huku Mkurugenzi wa Halmashauri hiyo akikiri kutengwa  eneo lenye ukubwa wa ekari 10 kwa ajili ya zoezi hilo.

Kikao hicho kilihudhuriwa na wakuu wa Idara na vitengo viongozi wa kamati ya ulinzi na usalama ya Wilaya pamoja na timu kutoka ofisi ya Mkuu wa Mkoa ambapo lengo la kikao hicho ilikuwa ni kuangalia changamoto zinazokabili Kata ya Mwangeza Wilayani hapo.

 Mwisho

Matangazo

  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2022_2023 SINGIDA RS July 01, 2022
  • MAJINA YA WALIOCHANGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA - 2023, MKOA WA SINGIDA December 14, 2022
  • TAARIFA YA MAPOKEZI YA FEDHA KWA KIPINDI CHA KUANZIA JULAI HADI OCTOBA, 2023 KWA AJILI YA UTEKELEZAJI WA SHUGHULI ZA MAENDELEO November 01, 2023
  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2021/2022 SINGIDA RS - GPN 2021 - 2022 July 01, 2021
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • DKT.MGANGA ASISITIZA MADAKTARI BINGWA KUTOA HUDUMA BORA

    May 05, 2025
  • WATUMISHI NA WAAJIRI HODARI MKOANI SINGIDA WAPOKEA TUZO

    May 02, 2025
  • KUELEKEA MEIMOSI,RC DENDEGO ATANGAZA FURSA ZA UWEKEZAJI

    April 25, 2025
  • MADAKTARI BINGWA WA DKT.SAMIA WABISHA HODI SINGIDA

    April 23, 2025
  • Angalia Zote

Video

Mkoa wa Singida waja na Mikakati ya Kuboresha Elimu
Video zaidi

Viungio vya Haraka

  • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
  • Mwongozo wa Matumizi ya TEHAMA Serikalini
  • Fomu ya Maombi ya Kusafiri Nje ya Nchi
  • MPANGO WA MANUNUZI MKOA WA SINGIDA
  • KUONA AJIRA ZA WAALIMU WA SAYANSI NA MAFUNDI SANIFU

Tovuti Muhimu

  • UTUMISHI
  • TAMISEMI
  • IKULU
  • WIZARA YA ELIMU
  • NECTA
  • WIZARA YA AFYA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Ramani ya Mkoa

Wasiliana Nasi

    SINGIDA

    Anuani: P O BOX 5 SINGIDA

    Simu: 2502170, 2502089

    Simu: 2502170, 2502089

    Barua Pepe: info@singida.go.tz ras@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Usiri
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

Copyright ©2023 Singida Regional Commisioner' Office . All rights reserved.