• Wasiliana Nasi |
    • Malalamiko |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
    • Blog |
Singida Regional Website

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Tovuti ya Mkoa wa Singida

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na dhima
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Ikungi
      • HISTORIA
    • Iramba
    • Manyoni
    • Mkalama
    • Singida
  • Halmashauri
    • H/W Ikungi
    • H/W Iramba
    • H/W Itigi
    • H/W Manyoni
    • H/W Mkalama
    • H/W Singida
    • H/M Singida
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Viwanda na Biashara
    • Madini
  • Huduma Zetu
    • Afya
      • Madaktari Bingwa
      • Huduma za Tiba
      • Huduma za Kinga
      • Ustawi wa Jamii
      • Afya ya Mazingira
      • Lishe
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba Wa Huduma Kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
    • Investment Guide
  • Kituo Cha Habari
    • Picha
    • Video
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma

KLINIKI YA SHERIA KUKATA KIU YA MASHAURI YA WANANCHI MKOANI SINGIDA.

Posted on: May 16th, 2025

Wanasheria wabobezi zaidi ya 40 kutoka Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali,Wizara ya Katiba na Sheria na wa Mkoa wa Singida wataweka kambi ya siku tano katika kliniki ya sheria bila malipo kwa lengo la kutoa ushauri wa kisheria kwa wananchi, watumishi wa umma na viongozi mkoani hapa.

Mkuu wa Mkoa wa Singida, Mhe.Halima Dendego, amezungumza hayo leo Mei 16,2025 na waandishi wa habari wakati  akitambulisha uzinduzi wa Kamati ya Ushauri wa Kisheria ngazi ya Mkoa ambayo itafuatiwa na uendeshaji wa kliniki ya sheria bila malipo kwa wananchi wote wa Mkoa wa Singida kuanzia Mei 19 hadi 23 mwaka huu.

"Namshukuru Mheshimiwa Rais Dkt.Samia Suluhu Hassan kwa kulinda, kukuza na kutetea haki za wananchi wanyonge na kupinga vitendo vya uvunjifu wa haki za kibinadamu,misingi ya utawala wa sheria, ukatili wa kijinsia na kuheshimu utawala wa sheria ambao ndio msingi wa maendeleo," amesema Mhe.Dendego.

Mhe.Dendego amesema Kamati za Ushauri wa Kisheria za Mikoa na Wilaya zimeanzishwa kwa mujibu wa sheria ya utekelezaji wa majukumu ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali sura ya 268 na mwongozo wa huduma za ushauri wa Kisheria katika ngazi ya Mkoa na Wilaya.

Amesema faida za kamati hizo za mikoa na wilaya ni kupunguza mashauri au migogoro dhidi ya serikali,huduma za ushauri wa kisheria ambazo zitakutanisha mawakili wa sheria wa taasisi mbalimbali na kuwasaidia wananchi wenye changamoto mbalimbali.

Mkuu wa Mkoa amesema kuwa  faida nyingine ni uwepo wa huduma ambao utawawezesha mawakili wa serikali kusimamia utawala wa sheria katika maeneo yao,kupunguza malalamiko ya kisheria kutoka kwa wananchi, kutoa elimu ya sheria kwa umma katika kushughulikia changamoto mbalimbali na kupunguza vitendo vya uonevu na vinavyovunja sheria na taratibu.

"Nitoe rai kwa wananchi wote kujitokeza kwa wingi siku ya uzinduzi pamoja na kuhudhuria kliniki ya kisheria kuanzia Mei 19 hadi 23 na wakati wote wa kliniki kutakuwa na Kamati ya Ushauri wa Kisheria ngazi ya mkoa,Mwanasheria Mkuu wa Serikali na Mawakili wa Serikali kutoka ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali," amesema Mhe.Dendego.

Naye Mkuu wa Kitengo cha Sheria Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Singida, Matrider Meckson, amesema siku ya uzinduzi kutakuwa na wanasheria wabobezi kutoka ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali,Wizara ya Katiba na Sheria na wa kutoka Mkoa wa Singida.

"Tumelenga kupunguza mashauri  kwasababu kuna malalamiko mengi na pia tunataka kuhakikisha tunapunguza mashauri yanayoenda mahakamani  pamoja na wananchi kuhakikisha wanapata haki zao," amesema.

Meckson alisema wanasheria hao wabobezi ambao watakuwa zaidi ya 41 watahakikisha shauri au malalamiko ya wananchi yanafuatiliwa hadi mwisho na ufumbuzi kupatikan hivyo wenye malalamiko mbalimbali ikiwemo ya ardhi,mirathi nakadhalika.


Matangazo

  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2022_2023 SINGIDA RS July 01, 2022
  • MAJINA YA WALIOCHANGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA - 2023, MKOA WA SINGIDA December 14, 2022
  • TAARIFA YA MAPOKEZI YA FEDHA KWA KIPINDI CHA KUANZIA JULAI HADI OCTOBA, 2023 KWA AJILI YA UTEKELEZAJI WA SHUGHULI ZA MAENDELEO November 01, 2023
  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2021/2022 SINGIDA RS - GPN 2021 - 2022 July 01, 2021
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • MIRADI WILAYANI ITIGI KUNUFAISHA MAELFU YA WANANCHI.

    May 21, 2025
  • KAMATI YA USHAURI NA KLINIKI YA SHERIA YAZINDULIWA SINGIDA

    May 19, 2025
  • MAGARI MAPYA WILAYANI,UTENDAJI KUIMARIKA!

    May 19, 2025
  • SERIKALI KUU YAMWAGA FEDHA ZA MIRADI MANISPAA YA SINGIDA

    May 16, 2025
  • Angalia Zote

Video

Mkoa wa Singida waja na Mikakati ya Kuboresha Elimu
Video zaidi

Viungio vya Haraka

  • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
  • Mwongozo wa Matumizi ya TEHAMA Serikalini
  • Fomu ya Maombi ya Kusafiri Nje ya Nchi
  • MPANGO WA MANUNUZI MKOA WA SINGIDA
  • KUONA AJIRA ZA WAALIMU WA SAYANSI NA MAFUNDI SANIFU

Tovuti Muhimu

  • UTUMISHI
  • TAMISEMI
  • IKULU
  • WIZARA YA ELIMU
  • NECTA
  • WIZARA YA AFYA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Ramani ya Mkoa

Wasiliana Nasi

    SINGIDA

    Anuani: P O BOX 5 SINGIDA

    Simu: 2502170, 2502089

    Simu: 2502170, 2502089

    Barua Pepe: info@singida.go.tz ras@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Usiri
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

Copyright ©2023 Singida Regional Commisioner' Office . All rights reserved.