• Wasiliana Nasi |
    • Malalamiko |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
    • Blog |
Singida Regional Website

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Tovuti ya Mkoa wa Singida

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na dhima
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Ikungi
      • HISTORIA
    • Iramba
    • Manyoni
    • Mkalama
    • Singida
  • Halmashauri
    • H/W Ikungi
    • H/W Iramba
    • H/W Itigi
    • H/W Manyoni
    • H/W Mkalama
    • H/W Singida
    • H/M Singida
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Viwanda na Biashara
    • Madini
  • Huduma Zetu
    • Afya
      • Madaktari Bingwa
      • Huduma za Tiba
      • Huduma za Kinga
      • Ustawi wa Jamii
      • Afya ya Mazingira
      • Lishe
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba Wa Huduma Kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
    • Investment Guide
  • Kituo Cha Habari
    • Picha
    • Video
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma

KOROSHO MKOANI SINGIDA KUWA ZAO LA KIBIASHARA NA LA KUDUMU.

Posted on: June 29th, 2017

  Halmashauri za Mkoa wa Singida zimetakiwa kusimamia taasisi za serikali zilizopo kwenye maeneo yao pamoja na wananchi wao wanapanda zao la Korosho ili kuhifadhi mazingira, kuongeza kipato na kutimiza azma ya kuwa zao la kudumu na la mda mrefu la kibiashara mkoani hapa.

Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru kitaifa Amour Hamad Amour ametoa maelekezo hayo wakati mwenge wa uhuru ukizindua upandaji wa zao la korosho kimkoa uliofanyika katika kijiji cha Kipumbuiko, Wilayani Ikungi ambapo wakimbiza mwenge kitaifa wameshiriki upandaji miche ya mikorosho.

Kabla ya kutoa maelekezo hayo Amour amekagua shamba la korosho la ukubwa wa ekari moja na miche 28 linalomilikiwa na shule ya msingi Kipumbuiko na kuelekeza kuwa upandaji mikorosho usiishie hapo bali kila taasisi yenye eneo inapaswa kupanda mikorosho ya kutosha.

“Leo tumezindua upandaji mikorosho kimkoa, sasa juhudi hizi zisiishie hapa, Mkurugenzi wa halmashauri ya Ikungi hakikisha kila taasisi inalima mikorosho ya kutosha ili lengo la kutunza mazingiza liweze kutimia kwa ufanisi” amesema na kuongeza kuwa

“Tunapoelekea kwenye Tanzania ya Viwanda tunapaswa kuongeza uzalishaji wa malighafi za kuhudumia viwanda vyetu, hivyo basi hamasisheni wananchi wapande mikorosho kwa wingi, hata mimi nimehamasika na lazima nitalima mikorosho”

Naye Mkimbiza Mwenge Kitaifa Fredrick Ndahani amesema zao la korosho limekuwa mkombozi wa uchumi kwa wananchi wa mikoa ya lindi na mtwara ambako wanaifananisha na dhahabu ya kijani, hivyo basi mkoa wa Singida unapaswa kusimamia zao hilo lenye manufaa makubwa.

Ndahani amesema korosho ni zao ambalo huweza kutumia maji kwa ufanisi kwakuwa inaweza kupandwa hata kipindi ambapo sio cha mvua nyingi na pia ni zao ambalo huweza kupandwa katika shamba ambalo lina mazao mengine.

Ameongeza kuwa wananchi Mkoani Singida wanapaswa kuchangamkia kilimo cha korosho kwakuwa mavuno yake ni endelevu huku akiwasisitiza kuwatumia na kuwapa ushirikiao  wataalamu wa taasisi zinazofanya tafiti na kutoa elimu ya kilimo cha Korosho.

Kwa upande wake mwalimu Mkuu wa shule ya msingi Kipumbuiko Mariam Makera amesema wanafunzi na wananchi wa kijiji hicho kwa kushirikiana na Wilaya ya Ikungi wameanzisha kilimo cha korosho shuleni hapo ili wananfunzi wajifunze kilimo hicho kwa vitendo na kuwahamasisha wazazi wao.

Makera amesema korosho zinazolimwa shambani hapo zimetumia teknolojia ya umwagiliaji maji kwa njia rahisi ya matone ambayo hutumia maji kwa ufanisi wa hali ya juu.

Zao la korosho Mkoani Singida limeanza kulimwa mwaka 1970 huku uendelezaji wake kwa Wilaya ya Ikungi ukianza mwaka 2013 ambapo hadi sasa mikorosho 17,000 imeshapandwa na lengo la upandaji mikorosho mingine kwa msimu wa mwaka 2017/2018 likiwa mikorosho laki tano.

Matangazo

  • TAARIFA KWA UMMA KUHUSU KILIMO CHA MASHAMBA YA PAMOJA YA KOROSHO, WILAYA YA MANYONI – SINGIDA May 02, 2022
  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2021/2022 SINGIDA RS - GPN 2021 - 2022 July 01, 2021
  • SINGIDA INVESTMENT GUIDE February 23, 2021
  • MAJINA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA 2022 - MKOA WA SINGIDA December 24, 2021
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • RC SERUKAMBA: TUTAJENGA HOJA HOSPITARI YA MAKIUNGU IPANDISHWE HADHI KUWA HOSPITALI YA RUFAA

    August 18, 2022
  • TOENI USHIRIKIANO KWA MAKARANI WA SENSA WAKATI WA KUHESABIWA.- RC SERUKAMBA

    August 17, 2022
  • RC Serukamba, amewataka Makarani na Wasimamizi wa SENSA mkoani hapa kutanguliza uzalendo katika zoezi la SENSA

    August 16, 2022
  • SERIKALI Mkoa wa Singida imetenga Sh.Milioni 342.8 kwa ajili ya kutengeneza shughuli za lishe ambapo ni sawa na Sh. 1,239 kwa kila mtoto wa chini ya miaka mitano

    August 16, 2022
  • Angalia Zote

Video

Mkoa wa Singida waja na Mikakati ya Kuboresha Elimu
Video zaidi

Viungio vya Haraka

  • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
  • Mwongozo wa Matumizi ya TEHAMA Serikalini
  • Fomu ya Maombi ya Kusafiri Nje ya Nchi
  • MPANGO WA MANUNUZI MKOA WA SINGIDA
  • KUONA AJIRA ZA WAALIMU WA SAYANSI NA MAFUNDI SANIFU

Tovuti Muhimu

  • UTUMISHI
  • TAMISEMI
  • IKULU
  • WIZARA YA ELIMU
  • NECTA
  • WIZARA YA AFYA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Ramani ya Mkoa

Wasiliana Nasi

    SINGIDA

    Anuani: P O BOX 5 SINGIDA

    Simu: 2502170, 2502089

    Simu: 2502170, 2502089

    Barua Pepe: info@singida.go.tz ras@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Usiri
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Singida. Haki Zote Zimehifadhiwa.