• Wasiliana Nasi |
    • Malalamiko |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
    • Blog |
Singida Regional Website

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Tovuti ya Mkoa wa Singida

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na dhima
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Ikungi
      • HISTORIA
    • Iramba
    • Manyoni
    • Mkalama
    • Singida
  • Halmashauri
    • H/W Ikungi
    • H/W Iramba
    • H/W Itigi
    • H/W Manyoni
    • H/W Mkalama
    • H/W Singida
    • H/M Singida
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Viwanda na Biashara
    • Madini
  • Huduma Zetu
    • Afya
      • Madaktari Bingwa
      • Huduma za Tiba
      • Huduma za Kinga
      • Ustawi wa Jamii
      • Afya ya Mazingira
      • Lishe
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba Wa Huduma Kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
    • Investment Guide
  • Kituo Cha Habari
    • Picha
    • Video
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma

Kumalizika kwa Ujenzi wa madarasa nchini nzima kutaongeza ufanisi katika matumizi ya huduma ya Mahakama mtandao

Posted on: February 2nd, 2022

Huduma ya Mahakama Mtandao itatekelezwa kwa ufanisi mkubwa nchi nzima kwa sababu Serikali imewekeza katika ujenzi wa miundombinu ya elimu ambayo ilionekana kuwa kikwazo katika utoaji na usimamizi wa haki na masuala ya kisheria. 

Hayo yamesemwa na Mkuu wa Mkoa wa Singida Dkt Binilith Mahenge leo Februari 2, 2022 wakati akitoa salamu kwa Mawakili mbalimbali na wananchi waliohudhuria kilele cha siku ya sheria iliyofanyika ki Mkoa katika viwanja vya Mahakama ya Hakimu Mkazi Mkoa Singida.

Dkt. Mahenge amesema kwamba Serikali imewekeza vyumba vya madarasa zaidi ya elifu 15 nchi nzima huku akiutaja mkoa wa Singida kwamba wamepata madarasa 632 ambapo Sekondari ni 330 na Msingi yakiwa 332 jambo ambalo limesaidia watoto wote kupata nafasi ya kwenda shule.

Aidha Rc Mahenge akaendelea kueleza kwamba kitendo cha watoto wote kwenda shule kitasababisha kiwango cha elimu kuongezeka jambo ambalo litasaidia kuongeza uelewa na kurahisisha matumizi ya huduma Mahakama mtandao.

Kwa sasa Serikali imeendelea kuviwezesha vikundi mbalimbali kujiajiri ikiwa ni pamoja na kuvipatia mikopo ya asilimia 10 ambapo vijana hao wataweza kumiliki mitaji na vifaa vya mawasiliano ambavyo huduma za kisheria za kimtandao zitapatikana.

 Naye Hakimu Mkazi wa Mahakama hiyo Ally Nzowa wakati akitoa hotuba yake ameshukuru Serikali kwa ujenzi na ukarabati wa Mahakama za Kisasa zenye mifumo ya teknolijia za kisasa sehemu mbalimbali hapa nchini ili ziendane na mazingira ya utoaji haki.

Amesema wanasheria wanajivunia uanzishwaji wa Mahakama zinazotembea ambapo zimesaidia utoaji wa huduma za kimahakama hasa katika mji wa Dar es salaam na Mwanza ambapo zaidi ya watu 1,500 wamehudumiwa.

Hata hivyo Mhe. Nzowa akaendelea kuiomba Serikali kuboresha miundombinu kama uwepo wa umeme wa uhakika, ili huduma hiyo iweze kutolewa maeneo mengi zaidi.

Akiendelea kuyataja mafanikio ya Mahakama Hakimu akasema kila hakimu amepatiwa kompiuta mpakato ambazo zinawasaidia kuchapa hukumu, kufanyia mikutano kwa njia ya video na kwamba uwepo wa huduma ya Mahakama mtandao pamoja na Mahakama inayotembea kumesaidia kupunguza gharama za uendeshaji wa Mahakama alifafanua Mhe. Nzowa.

Mkuu wa Ofisi ya Mashtaka wa Mkoa wa Singida Mhe. Juma Salige pamoja na shukrani akaiomba Serikali hasa kipindi hiki ambacho Mahakama zinafanya mabadiliko makubwa ya kiutendaji kuongezewa bajeti kwenye Mahakama, Polisi na Magereza kwa kuwa wanategemeana ili kuongeza ufanisi.

“Mahakama imekuwa na mchango mkubwa katika kukuza uchumi wa nchi kupitia utoaji wa haki na usimamizi wa sheria jambo ambalo likiratibiwa vizuri litaleta manufaa makubwa kwa nchi”. Alisema Juma Salige.

Awali akiwawakilisha Mawakili wa kujitegemea katika kilele cha maadhimisho hayo Wakili Peter Njingo akaiomba Serikali kuielimisha jamii kwa upana ili kurahisisha utoaji wa huduma za kisheria kwa kuwa wananchi wengi wamekuwa wakishindwa kuendeleza kesi zao kwa sababu ya ufahamu mdogo wa matumizi ya teknolojia za simu Janja.

Akiendelea na hotuba yake Wakili Peter akaishauri Serikali kuingiza mafunzo ya Mahakama mtandao katika mitaala ya vyuo ili Mawakili waweze kujifunza kabla hawajaingia makazini kwa kuwa changamoto ya matumizi ya Mahakama mtandao ni ya watu wote.

Hata hivyo wakili huyo akasisitiza Serikali ikutane na makampuni ya simu kama Tigo, Airtel, Hallotel Vodacom na TTCL waweze kukubaliana kupunguza gharama za mabando ya intaneti ili wananchi waweze kupata misaada ya kisheria kupitia mitando. .

Akimalizia hotuba yake Wakili huyo akaiomba Mahakama kuongeza idadi ya maafisa TEHAMA katika Mahakama ili kutoa msaada wa kiufundi mara zinapotokea changamoto za mifumo ili huduma ziweze kuendelea na malengo kufikiwa.

Wawakilishi wa wananchi na baadhi ya viongozi wa Dini katika siku ya kilele cha siku ya sheria ambayo ilikuwa na kauli mbiu ya “Zama za mapinduzi ya nne ya viwanda, safari ya maboresho kuelekea Mahakama ya mtandao”.wakaguswa na kutoa maoni yao ambapo Askofu wa Kanisa la Anglikana Mkoa wa Singida John Lupaa akahidi kutoa magodoro 50 kwa ajili ya wafungwa waliopo katika Gereza la Manyoni .

Askofu amesema alipata fursa ya kulitembelea na kujionea changamoto inayowakabili wafungwa hao hivyo kuiomba jamii  kutoa msaada wa kisheria na mali kwa kila anayeguswa.

Akiwawakilisha wananchi Bwana Saidi  Sombi ambaye alitumia Sanaa ya ushairi kupeleka ujumbe wake amebainisha kwamba matumizi ya TEHAMA katika mahakama yameongeza uwazi, uwajibikaji wa watumishi na imeleta unafuu kwa wananchi ambao walikuwa wakishindwa kufuatilia kesi zao kwa sababu ya umbali au kutokuwa na muda wa kutosha.


Viongozi Meza Kuu wakishiriki wimbo wa Taifa mara baada ya kuwasili uwanjani

Mkuu wa Wilaya ya Singida Mhandisi Paskasi Muragili akizungumza kabla ya kumkaribisha Mkuu wa Mkoa wa Singida

Meza Kuu ikiwa katika picha ya pamoja na viongozi wa Dini mkoa wa Singida

Matangazo

  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2022_2023 SINGIDA RS July 01, 2022
  • MAJINA YA WALIOCHANGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA - 2023, MKOA WA SINGIDA December 14, 2022
  • TAARIFA YA MAPOKEZI YA FEDHA KWA KIPINDI CHA KUANZIA JULAI HADI OCTOBA, 2023 KWA AJILI YA UTEKELEZAJI WA SHUGHULI ZA MAENDELEO November 01, 2023
  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2021/2022 SINGIDA RS - GPN 2021 - 2022 July 01, 2021
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • IKUNGI YAPEPERUSHA BENDERA KWA MIRADI YA KIMKAKATI.

    May 08, 2025
  • DKT.MGANGA ASISITIZA MADAKTARI BINGWA KUTOA HUDUMA BORA

    May 05, 2025
  • WATUMISHI NA WAAJIRI HODARI MKOANI SINGIDA WAPOKEA TUZO

    May 02, 2025
  • KUELEKEA MEIMOSI,RC DENDEGO ATANGAZA FURSA ZA UWEKEZAJI

    April 25, 2025
  • Angalia Zote

Video

Mkoa wa Singida waja na Mikakati ya Kuboresha Elimu
Video zaidi

Viungio vya Haraka

  • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
  • Mwongozo wa Matumizi ya TEHAMA Serikalini
  • Fomu ya Maombi ya Kusafiri Nje ya Nchi
  • MPANGO WA MANUNUZI MKOA WA SINGIDA
  • KUONA AJIRA ZA WAALIMU WA SAYANSI NA MAFUNDI SANIFU

Tovuti Muhimu

  • UTUMISHI
  • TAMISEMI
  • IKULU
  • WIZARA YA ELIMU
  • NECTA
  • WIZARA YA AFYA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Ramani ya Mkoa

Wasiliana Nasi

    SINGIDA

    Anuani: P O BOX 5 SINGIDA

    Simu: 2502170, 2502089

    Simu: 2502170, 2502089

    Barua Pepe: info@singida.go.tz ras@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Usiri
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

Copyright ©2023 Singida Regional Commisioner' Office . All rights reserved.