• Wasiliana Nasi |
    • Malalamiko |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
    • Blog |
Singida Regional Website

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Tovuti ya Mkoa wa Singida

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na dhima
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Ikungi
      • HISTORIA
    • Iramba
    • Manyoni
    • Mkalama
    • Singida
  • Halmashauri
    • H/W Ikungi
    • H/W Iramba
    • H/W Itigi
    • H/W Manyoni
    • H/W Mkalama
    • H/W Singida
    • H/M Singida
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Viwanda na Biashara
    • Madini
  • Huduma Zetu
    • Afya
      • Madaktari Bingwa
      • Huduma za Tiba
      • Huduma za Kinga
      • Ustawi wa Jamii
      • Afya ya Mazingira
      • Lishe
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba Wa Huduma Kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
    • Investment Guide
  • Kituo Cha Habari
    • Picha
    • Video
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma

MAADHIMISHO SIKU YA WANAWAKE KUWEKA HISTORIA MKOANI SINGIDA

Posted on: March 1st, 2025

Mkuu wa Mkoa wa Singida Mhe. Halima Dendego amesema kuelekea siku ya Mwanamke duniani kimkoa,wameazimia kufanya matendo ya huruma kwa kutembelea na kutoa msaada kwa watoto wenye mahitaji maalumu katika Chuo cha Maendeleo ya Wananchi FDC .

Mhe.Dendego amesema hayo leo ofisini kwake wakati akizungumzia maandalizi ya siku ya Mwanamke kimkoa ambayo yatafanyika tarehe 7/3/2025 katika uwanja wa Bombadia.

Akitoa ratiba ya matukio mbalimbali yatakayofanyika kuelekea kilele cha maadhimisho,Mkuu wa Mkoa amesema kuwa kuanzia leo tarehe Mosi,maadhimisho yameanza katika ngazi ya Vijiji, Kitongoji ,Mitaa,Kata, Tarafa na Halmashauri na kuanzia tarehe 5 Machi, maadhimisho yataanza kufanyika katika ngazi ya Mkoa ambapo shughuli mbalimbali zitafanyika.

Katika Bonanza la Machi 5, kutakuwa na michezo mbalimbali katika uwanja wa Bombadia ikiwemo mpira wa Pete, Ngoma za asili, Muziki wa kizazi kipya, lengo la burudani hizi ni uhakikisha ujumbe wa siku ya Mwanamke kwa mwaka huu unafika kwa umma .

lakini pia tarehe 6/3/2025 kutakuwa na kongamano la wanawake wote kutoka maeneo mbalimbali ya Mkoa wa Singida kuanzia ngazi ya kijiji mpaka Mkoa na jumla ya wanawake zaidi ya elfu moja(1000) watakuwepo katika kongamano hilo likisindikizwa na Mada Mbalimbali ambazo zitafundishwa na kujadiliwa kama vile Mwanamke na Uchumi, Nishati safi ya kupikia ,mashaka ya ukatili,Mwanamke na Kodi na uwezeshwaji wa Mwanamke kuwa Mama bora.

Tarehe 7/3/2025 itakuwa ndio kilele cha siku ya Mwanamke kimkoa wa ambapo sherehe hizo zitafanyika katika uwanja wa Bombadia zikitanguliwa na maandamano ya Wanawake wote,Burudani mbalimbali na zoezi la utoaji wa tuzo kwa Wanawake waliofanya vizuri katika maswala mbalimbali yanayogusa jamii.

Katika hatua nyingine kueekea mwanzo wa mwezi mtukufu wa Ramadhani, Mkuu wa Mkoa wa Singida amewaomba wafanyabiashara wasipandishe bei ya bidhaa katika kipindi hiki cha Mwezi Mtukufu wa Ramadhani pamoja na Kwaresma ili wawape nafasi ya waumini kupata unafuu wa kupata mahitaji yao katika kipindi hiki.

Siku ya mwanamke duniani inaadhimishwa tarehe 08/03 ya kila Mwaka na kwa Mwaka huu siku hiyo kitaifa itafanyika Mkoani Arusha, kwa Mkoa wa Singida itaadhimishwa tarehe 07.03.2025 katika uwanja wa Bombadia Manispaa ya Singida na Kauli mbiu ya Mwaka huu ni :

           "WANAWAKE NA WASICHANA 2025:TUIMARISHE HAKI, USAWA NA UWEZESHAJI"

Matangazo

  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2022_2023 SINGIDA RS July 01, 2022
  • MAJINA YA WALIOCHANGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA - 2023, MKOA WA SINGIDA December 14, 2022
  • TAARIFA YA MAPOKEZI YA FEDHA KWA KIPINDI CHA KUANZIA JULAI HADI OCTOBA, 2023 KWA AJILI YA UTEKELEZAJI WA SHUGHULI ZA MAENDELEO November 01, 2023
  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2021/2022 SINGIDA RS - GPN 2021 - 2022 July 01, 2021
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • DKT.MGANGA ASISITIZA MADAKTARI BINGWA KUTOA HUDUMA BORA

    May 05, 2025
  • WATUMISHI NA WAAJIRI HODARI MKOANI SINGIDA WAPOKEA TUZO

    May 02, 2025
  • KUELEKEA MEIMOSI,RC DENDEGO ATANGAZA FURSA ZA UWEKEZAJI

    April 25, 2025
  • MADAKTARI BINGWA WA DKT.SAMIA WABISHA HODI SINGIDA

    April 23, 2025
  • Angalia Zote

Video

Mkoa wa Singida waja na Mikakati ya Kuboresha Elimu
Video zaidi

Viungio vya Haraka

  • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
  • Mwongozo wa Matumizi ya TEHAMA Serikalini
  • Fomu ya Maombi ya Kusafiri Nje ya Nchi
  • MPANGO WA MANUNUZI MKOA WA SINGIDA
  • KUONA AJIRA ZA WAALIMU WA SAYANSI NA MAFUNDI SANIFU

Tovuti Muhimu

  • UTUMISHI
  • TAMISEMI
  • IKULU
  • WIZARA YA ELIMU
  • NECTA
  • WIZARA YA AFYA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Ramani ya Mkoa

Wasiliana Nasi

    SINGIDA

    Anuani: P O BOX 5 SINGIDA

    Simu: 2502170, 2502089

    Simu: 2502170, 2502089

    Barua Pepe: info@singida.go.tz ras@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Usiri
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

Copyright ©2023 Singida Regional Commisioner' Office . All rights reserved.