• Wasiliana Nasi |
    • Malalamiko |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
    • Blog |
Singida Regional Website

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Tovuti ya Mkoa wa Singida

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na dhima
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Ikungi
      • HISTORIA
    • Iramba
    • Manyoni
    • Mkalama
    • Singida
  • Halmashauri
    • H/W Ikungi
    • H/W Iramba
    • H/W Itigi
    • H/W Manyoni
    • H/W Mkalama
    • H/W Singida
    • H/M Singida
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Viwanda na Biashara
    • Madini
  • Huduma Zetu
    • Afya
      • Madaktari Bingwa
      • Huduma za Tiba
      • Huduma za Kinga
      • Ustawi wa Jamii
      • Afya ya Mazingira
      • Lishe
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba Wa Huduma Kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
    • Investment Guide
  • Kituo Cha Habari
    • Picha
    • Video
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma

MADAKTARI BINGWA WAWASILI SINGIDA KUTOA HUDUMA BORA KWA WANANCHI

Posted on: October 6th, 2025

Katibu Tawala wa Mkoa wa Singida, Dkt. Fatuma Mganga, amewataka Madaktari Bingwa waliowasili mkoani humo kuhakikisha wanatoa huduma bora, zenye heshima na utu kwa wananchi ili kuenzi taaluma yao na kuacha alama chanya katika jamii.

Akizungumza leo Oktoba 6, 2025, wakati akiwakaribisha Madaktari Bingwa wa magonjwa mbalimbali maarufu kama Madaktari wa Mama Samia, Dkt. Mganga amesema madaktari hao wamewasili Singida kwa ajili ya kutoa huduma za kibingwa katika Halmashauri zote saba za Mkoa huo kwa muda wa siku tano.

Amesema ni wajibu wa kila daktari kutumia ujuzi wake ipasavyo kwa moyo wa kujituma, upendo na ukarimu ili huduma watakazozitoa ziwe chachu ya matumaini kwa wananchi na kuacha kumbukumbu njema ya kazi yao.

 “Tumetumwa kufanya kazi hii, hivyo yatupasa tukatumike kwa bidii, upendo na ukarimu kama fursa ya kuleta kicheko na baraka kwa wananchi tunaokwenda kuwahudumia,” alisema Dkt. Mganga.

Ameongeza kuwa utoaji wa huduma bora ni wajibu wa kitaaluma unaopaswa kuambatana na ubinadamu na moyo wa kujitolea, hasa kwa madaktari bingwa wanaokwenda kugusa maisha ya wananchi moja kwa moja. Kadhalika, ametoa wito kwa madaktari hao kuonyesha ubingwa wao kwa vitendo kwa kutoa huduma za ubora wa hali ya juu zinazolenga kupunguza idadi ya vifo vya akina mama na watoto, hususan wale waliokuwa wakisafiri umbali mrefu kufuata huduma hizo katika hospitali kubwa za kitaifa kama Muhimbili.

Kwa upande wake, Mganga Mkuu wa Mkoa wa Singida, Dkt. Victorina Ludovick, amewahamasisha wananchi kujitokeza kwa wingi katika vituo vya kutolea huduma hizo za kibingwa ambazo sasa zimesogezwa karibu na maeneo yao.

“Huduma hizi ni za kipekee sana. Wapo wananchi wengi waliokuwa wakisafiri hadi Muhimbili au Bugando kwa ajili ya huduma kama hizi, sasa zimeletwa mlangoni mwao. Ni nafasi ya kipekee ambayo kila mwananchi anapaswa kuitumia,” alisema Dkt. Ludovick.

Ameeleza kuwa huduma zitakazotolewa ni pamoja na magonjwa ya wanawake, watoto, upasuaji, meno na kinywa, magonjwa ya ganzi na usingizi, pamoja na uvimbe, huku zaidi ya wananchi 5,000 wakitarajiwa kufikiwa katika awamu hii.

Mmoja wa Madaktari Bingwa waliowasili mkoani humo alisema kuwa timu yao imejiandaa kikamilifu kuhakikisha wananchi wa Singida wanapata huduma bora na za kibingwa kwa viwango vya juu.

“Tumewezeshwa vizuri na Serikali – tuna vifaa vya kisasa, dawa muhimu na timu kamili ya wataalamu wa fani mbalimbali. Tumejipanga kutoa huduma bora, zenye matokeo chanya kwa wananchi,” alisema mmoja wa madaktari hao.

Ameishukuru Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuendelea kuimarisha sekta ya afya kupitia mpango huu wa Madaktari Bingwa unaolenga kufikisha huduma bora kwa wananchi katika ngazi za mikoa na halmashauri.

Uwepo wa Madaktari Bingwa mkoani Singida unatarajiwa kuleta manufaa makubwa kwa wananchi, ikiwemo kupunguza gharama za kusafiri umbali mrefu kufuata huduma za kibingwa, kuimarisha afya ya jamii kwa kugundua na kutibu magonjwa mapema, kuongeza uelewa wa wananchi kuhusu afya kupitia elimu itakayotolewa sambamba na huduma, pamoja na kuongeza ujuzi kwa watumishi wa afya wa mikoa na halmashauri kupitia mafunzo ya vitendo kutoka kwa madaktari hao.

Huduma hizo za kibingwa zitaendelea kutolewa kwa muda wa siku tano katika vituo maalum vilivyopangwa kwenye halmashauri zote saba za Mkoa wa Singida, zikilenga kuboresha afya ya wananchi na kuunga mkono juhudi za Serikali katika kusogeza huduma bora za afya karibu na wananchi wote.

Matangazo

  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2022_2023 SINGIDA RS July 01, 2022
  • MAJINA YA WALIOCHANGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA - 2023, MKOA WA SINGIDA December 14, 2022
  • TAARIFA YA MAPOKEZI YA FEDHA KWA KIPINDI CHA KUANZIA JULAI HADI OCTOBA, 2023 KWA AJILI YA UTEKELEZAJI WA SHUGHULI ZA MAENDELEO November 01, 2023
  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2021/2022 SINGIDA RS - GPN 2021 - 2022 July 01, 2021
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • MABINGWA WA CECAFA WAKARIBISHWA NYUMBANI BAADA YA USHINDI MNONO

    October 05, 2025
  • MADAKTARI BINGWA WAWASILI SINGIDA KUTOA HUDUMA BORA KWA WANANCHI

    October 06, 2025
  • HALI YA HEWA YA MKOA WA SINGIDA YATAKIWA KUTUMIWA KAMA FURSA NA SIO KIKWAZO

    September 25, 2025
  • MRADI WA MABWAWA YA KUTIBU MAJITAKA KUKAMILIKA OKTOBA,WANANCHI KUNUFAIKA

    September 23, 2025
  • Angalia Zote

Video

Mkoa wa Singida waja na Mikakati ya Kuboresha Elimu
Video zaidi

Viungio vya Haraka

  • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
  • Mwongozo wa Matumizi ya TEHAMA Serikalini
  • Fomu ya Maombi ya Kusafiri Nje ya Nchi
  • MPANGO WA MANUNUZI MKOA WA SINGIDA
  • KUONA AJIRA ZA WAALIMU WA SAYANSI NA MAFUNDI SANIFU

Tovuti Muhimu

  • UTUMISHI
  • TAMISEMI
  • IKULU
  • WIZARA YA ELIMU
  • NECTA
  • WIZARA YA AFYA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Ramani ya Mkoa

Wasiliana Nasi

    SINGIDA

    Anuani: P O BOX 5 SINGIDA

    Simu: 2502170, 2502089

    Simu: 2502170, 2502089

    Barua Pepe: info@singida.go.tz ras@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Usiri
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

Copyright ©2023 Singida Regional Commisioner' Office . All rights reserved.