• Wasiliana Nasi |
    • Malalamiko |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
    • Blog |
Singida Regional Website

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Tovuti ya Mkoa wa Singida

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na dhima
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Ikungi
      • HISTORIA
    • Iramba
    • Manyoni
    • Mkalama
    • Singida
  • Halmashauri
    • H/W Ikungi
    • H/W Iramba
    • H/W Itigi
    • H/W Manyoni
    • H/W Mkalama
    • H/W Singida
    • H/M Singida
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Viwanda na Biashara
    • Madini
  • Huduma Zetu
    • Afya
      • Madaktari Bingwa
      • Huduma za Tiba
      • Huduma za Kinga
      • Ustawi wa Jamii
      • Afya ya Mazingira
      • Lishe
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba Wa Huduma Kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
    • Investment Guide
  • Kituo Cha Habari
    • Picha
    • Video
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma

RAIS DKT. JOHN MAGUFULI AWEKA JIWE LA MSINGI UJENZI WA DARAJA LA MTO SIBITI LINALOUNGANISHA MKOA WA SIMIYU NA SINGIDA NA KUMTAKA MKANDARASI KUHAKIKISHA ANAMALIZA KAZI YA UJENZI WA DARAJA MAPEMA

Posted on: September 10th, 2018

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Magufuli amemwagiza Mkandarasi wa Kampuni ya HAINAN kutoka CHINA kuhakikisha anafanya kazi usiku na mchana ili kukamilisha ujenzi wa daraja la mto SIBITI ambayo linaunganisha mikoa ya Singida na Simiyu ili kuondoa adha kubwa wanayopata wananchi hasa kipindi cha mvua.

Rais Magufuli ametoa agizo hilo mapema leo alipokuwa Mkoani Singida wakati anaweka jiwe la msingi katika ujenzi wa Daraja la mto Sibiti baada ya kutoridhika na maendeleo ya ujenzi wa daraja hilo ambalo limechukua zaidi ya miaka sita licha ya mkandarasi kulipwa zaidi ya asilimia 90 ya gharama za ujenzi wa daraja hilo ambalo ujenzi wake unagharimu shilingi za kitanzania bilioni 16.

Rais MAGUFULI pia amewataka watendaji wa Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano kumsimamia ipasavyo mkandarasi huyo ili aweze kukamilisha ujenzi huo kabla ya mwezi wa TATU mwakani na kama mkandarasi atashindwa kukamilisha kazi hiyo kwa muda ulipangwa basi atachukua hatua zaidi dhidi ya wahusika akiwemo mkandarasi huyo.

Kwa upande wake, Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Mhandisi Isack Kamwele amesema ujenzi wa daraja la Mto Sibiti utakuwa ni mkombozi mkubwa kwa Wananchi wa mikoa ya Singida na Simiyu katika uimarishaji wa shughuli za kiuchumi kwenda ukanda huo.

Naye Mkuu wa Mkoa wa Singida Dkt. Rehema Nchimbi kwaniaba ya wananchi wa Mkoa wa Singida amemshukuru Mheshimiwa Rais Dkt. John Magufuli pamoja na Serikali ya awamu ya Tano kwa kuifanyia mambo mengi ya kimaendeleo mkoani hapa."Serikali imetupatia jumla ya shilingi za kitanzania bilioni ishilini na nne katika masuala ya Elimu ya kuwezesha Elimu bure kwa Wananchi, ukarabati wa miundombinu ya shule, ujenzi wa hosteli na mikakati mingine ya Elimu Bure, hizi ni fedha nyingi na zimefanya mambo makubwa sana mkoani Singida." 

"Tumepokea pikipiki 136 kwa ajili ya waratibu wa elimu za Kata na tayari zimeshagawanywa na sehemu zingine zinaendelea kugawanywa. Pia tumepokea fedha za ujenzi wa vituo vya Afya ambavyo ni 10 pamoja na fedha za kutandaza nguzo za umeme vijijini. Hii ni Singida njema sana." Dkt. Nchimbi.

Aidha, Wananchi wa mikoa ya Singida na Simiyu wamemshukuru sana Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Magufuli kwa ujenzi wa daraja hilo  ambalo kwa kupitia Serikali ya Awamu ya Tano imeweza kutoa shilingi za kitanzania bilioni 16 ili Wananchi wake waweze kunufaika kwa miundombinu bora ya barabara ambapo kwa ujenzi huo wa daraja litasaidia kuongeza na kuimarisha uchumi. "Tunamshukuru Rais Magufuli kwa kuweka jiwe la msingi la daraja hili na hii inaonyesha jinsi gani Mheshimiwa Rais wa Awamu ya Tano, Dkt. John Magufuli anavyotekelea kwa vitendo ILANI YA CCM kwani daraja hili litakuwa mkombozi kwetu wananchi wa Singida na Simiyu pamoja na wananchi kutoka pande za Tanzania kwani hapa kuna shughuli nyingi sana za kibiashara hususani CHUMVI hupatikana kwa wingi sana na kwa bei rahisi" Wananchi Sitibi.


Matangazo

  • TAARIFA KWA UMMA KUHUSU KILIMO CHA MASHAMBA YA PAMOJA YA KOROSHO, WILAYA YA MANYONI – SINGIDA May 02, 2022
  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2021/2022 SINGIDA RS - GPN 2021 - 2022 July 01, 2021
  • SINGIDA INVESTMENT GUIDE February 23, 2021
  • MAJINA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA 2022 - MKOA WA SINGIDA December 24, 2021
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • Dkt. Mahenge Atangaza Fursa kwa Wawekezaji Mkoani Singida

    May 14, 2022
  • Madiwani Watakiwa kushiriki kikamilifu zoezi la uwekaji wa Anwani za Makazi na Posti Kodi Wilayani Manyoni

    May 11, 2022
  • Taasisi binafsi zatakiwa kuonesha ushirikiano katika uwekaji wa Anwani za Makazi Manispaa ya Singida.

    May 10, 2022
  • Watendaji wa Makiungu, Mungaa Watakiwa kufanya "Data Cleaning" Katika zoezi la uwekaji wa Anwani za Makazi.

    May 09, 2022
  • Angalia Zote

Video

Mkoa wa Singida waja na Mikakati ya Kuboresha Elimu
Video zaidi

Viungio vya Haraka

  • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
  • Mwongozo wa Matumizi ya TEHAMA Serikalini
  • Fomu ya Maombi ya Kusafiri Nje ya Nchi
  • MPANGO WA MANUNUZI MKOA WA SINGIDA
  • KUONA AJIRA ZA WAALIMU WA SAYANSI NA MAFUNDI SANIFU

Tovuti Muhimu

  • UTUMISHI
  • TAMISEMI
  • IKULU
  • WIZARA YA ELIMU
  • NECTA
  • WIZARA YA AFYA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Ramani ya Mkoa

Wasiliana Nasi

    SINGIDA

    Anuani: P O BOX 5 SINGIDA

    Simu: 2502170, 2502089

    Simu: 2502170, 2502089

    Barua Pepe: info@singida.go.tz ras@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Usiri
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Singida. Haki Zote Zimehifadhiwa.