• Wasiliana Nasi |
    • Malalamiko |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
    • Blog |
Singida Regional Website

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Tovuti ya Mkoa wa Singida

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na dhima
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Ikungi
      • HISTORIA
    • Iramba
    • Manyoni
    • Mkalama
    • Singida
  • Halmashauri
    • H/W Ikungi
    • H/W Iramba
    • H/W Itigi
    • H/W Manyoni
    • H/W Mkalama
    • H/W Singida
    • H/M Singida
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Viwanda na Biashara
    • Madini
  • Huduma Zetu
    • Afya
      • Madaktari Bingwa
      • Huduma za Tiba
      • Huduma za Kinga
      • Ustawi wa Jamii
      • Afya ya Mazingira
      • Lishe
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba Wa Huduma Kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
    • Investment Guide
  • Kituo Cha Habari
    • Picha
    • Video
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma

RAS Singida akemea ucheleweshaji wa malipo ya vibarua

Posted on: May 30th, 2023

Ucheleweshaji wa fedha na  malipo kidogo kwa vibarua na mafundi yanayolipwa  na wakandarasi katika  miradi ya ujenzi wa nyumba ya kuhifadhia maiti (Mochwari) pamoja na wodi ya wanawake na wodi ya wanaume zinazojengwa katika Hospitali ya Wilaya ya Manyoni mkoani Singida umechangia ucheleweshaji wa ukamilishwaji wa mradi huo jambo ambalo viongozi wameagiza kukomeshwa hali hiyo.

Akiongea baada ya ukaguzi wa majengo hayo na kusikiliza malalamiko ya baadhi ya vibarua na mafundi ambao walilalamikia kutolipwa fedha zao kwa wakati na kulipwa ujira mdogo, Katibu Tawala Mkoa wa Singida Dkt. Fatma Mganga leo amezitaka kamati za ujenzi kukutana na mkandarasi wa majengo hayo na kuwalipa madeni yao kwa vibarua na mafundi wanaofanya kazi hiyo pamoja na kukaa mezani na kukubaliana malipo mapya ili kuondoa migomo baridi ya vibarua hao.

Aidha RAS amesema kwamba hayupo tayari kuona fedha za Seriki zinarudi hazina mwisho wa mwaka wakati miradi ya maendeleo ya wananchi haijakamilika hivyo kumuelekeza Mganga Mkuu wa Wilaya hiyo  Furaha Mwakafwila  kukutana na Mkandarasi huyo na kuona kama inawezekana kuachia jengo moja kwa mafundi wengine ili kazi ziweze kukamilika kwa wakati.

"Kila fundi anatakiwa kuwalipa vibarua wake kwa wakati na stahili walizokubaliana tofauti na hivyo itakuwa ni sababu ya ucheleweshaji wa kazi, na tulishatoa maelekezo kwamba fundi mmoja jengo moja kama inawezekana Mkandandarasi ashauriwe awaachie mafundi wengine jengo moja"

Kwa upande wake Mganga Mkuu wa Wilaya Furaha Mwakafwila amemuahidi Katibu Tawala huyo kwamba watakutana na Makandarasi kujadili namna ya kuboresha hali ujenzi, malipo ya vibarua na kuhakisha kazi inakamilika ndani ya wakati.

Hata hivyo RAS alitembelea Mradi wa Ujenzi wa shule ya Eka iliyoko Kata ya Eka Wilayani Manyoni chini ya Mradi wa Boost unaogharimu jumla wa Milioni 493.4 wenye vyumba vya madarasa  14 na Awali viwili na jengo la Utawala ambapo amewataka watendaji wa vijiji na kata kuhamasisha wananchi  kuchangia nguvu kazi lengo likiwa fedha zilizotolewa zinatosheleza.

Hata hivyo RAS Dkt. Fatma ametoa maagizo kwa wasimamizi wa ujenzi wa miradi ya boost Mkoani hapo kuhakikisha mafundi wanakuwa na mipango kazi katika eneo la kazi itakayoonesha namna ya utekelezaji wa shughuli za kila siku tofauti na hivyo mafundi wataonekana wanafanya kazi kila siku lakini majengo hayaendelei.

Hata hivyo RAS amesema Serikali kwa kiasi kikubwa imetambua umuhimu na mchango wa mafundi wa mtaani ndio maana imeendelea kuwapa kazi hivyo kuwataka kutopoteza imani hiyo kwa kufanya kazi nzuri, kutofanya uharibifu wa vifaa vya ujenzi na kubakiza kazi kwa wakati na kwa ubora unaotakiwa.

Awali RAS amewaeleza walimu katika miradi hiyo kuhakikisha wanapanda miti ya kivuko na matunda  maeneo yanayowazunguka ikiwa ni pamoja na kuyapendezesha maeneo kwa kutengeneza bustani za maua.


Matangazo

  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2022_2023 SINGIDA RS July 01, 2022
  • MAJINA YA WALIOCHANGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA - 2023, MKOA WA SINGIDA December 14, 2022
  • TAARIFA YA MAPOKEZI YA FEDHA KWA KIPINDI CHA KUANZIA JULAI HADI OCTOBA, 2023 KWA AJILI YA UTEKELEZAJI WA SHUGHULI ZA MAENDELEO November 01, 2023
  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2021/2022 SINGIDA RS - GPN 2021 - 2022 July 01, 2021
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • IKUNGI YAPEPERUSHA BENDERA KWA MIRADI YA KIMKAKATI.

    May 08, 2025
  • DKT.MGANGA ASISITIZA MADAKTARI BINGWA KUTOA HUDUMA BORA

    May 05, 2025
  • WATUMISHI NA WAAJIRI HODARI MKOANI SINGIDA WAPOKEA TUZO

    May 02, 2025
  • KUELEKEA MEIMOSI,RC DENDEGO ATANGAZA FURSA ZA UWEKEZAJI

    April 25, 2025
  • Angalia Zote

Video

Mkoa wa Singida waja na Mikakati ya Kuboresha Elimu
Video zaidi

Viungio vya Haraka

  • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
  • Mwongozo wa Matumizi ya TEHAMA Serikalini
  • Fomu ya Maombi ya Kusafiri Nje ya Nchi
  • MPANGO WA MANUNUZI MKOA WA SINGIDA
  • KUONA AJIRA ZA WAALIMU WA SAYANSI NA MAFUNDI SANIFU

Tovuti Muhimu

  • UTUMISHI
  • TAMISEMI
  • IKULU
  • WIZARA YA ELIMU
  • NECTA
  • WIZARA YA AFYA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Ramani ya Mkoa

Wasiliana Nasi

    SINGIDA

    Anuani: P O BOX 5 SINGIDA

    Simu: 2502170, 2502089

    Simu: 2502170, 2502089

    Barua Pepe: info@singida.go.tz ras@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Usiri
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

Copyright ©2023 Singida Regional Commisioner' Office . All rights reserved.