• Wasiliana Nasi |
    • Malalamiko |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
    • Blog |
Singida Regional Website

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Tovuti ya Mkoa wa Singida

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na dhima
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Ikungi
      • HISTORIA
    • Iramba
    • Manyoni
    • Mkalama
    • Singida
  • Halmashauri
    • H/W Ikungi
    • H/W Iramba
    • H/W Itigi
    • H/W Manyoni
    • H/W Mkalama
    • H/W Singida
    • H/M Singida
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Viwanda na Biashara
    • Madini
  • Huduma Zetu
    • Afya
      • Madaktari Bingwa
      • Huduma za Tiba
      • Huduma za Kinga
      • Ustawi wa Jamii
      • Afya ya Mazingira
      • Lishe
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba Wa Huduma Kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
    • Investment Guide
  • Kituo Cha Habari
    • Picha
    • Video
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma

RC Dendego Akutana na Watendaji wa Halmashauri ya Iramba: Atoa Maagizo kwa Wakuu wa Idara na Kusisitiza Uwajibikaji.

Posted on: September 27th, 2024

Mkuu wa Mkoa wa Singida Mhe. Halima Dendego, mapema leo (Septemba 27, 2024) amekutana na Watendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Iramba lengo kuu likiwa ni kuboresha utendaji kazi wa watumishi katika halmashauri hiyo ili waweze kutekeleza majukumu yao kwa ufanisi.

Akizungumza kwenye kikao kazi kilichofanyia katika ukumbi wa mikutano wa Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Iramba, RC Dendego amewataka Wakuu wa Idara na Vitengo katika halmashauri hiyo kuhakikisha wanasimamia miradi yote ya maendeleo ili kukamilika kwa wakati, ubora na kwa thamani ya fedha pasipo kuzalisha madeni.

"Serikali inapoleta fedha za ujenzi wa mradi inakuwa imeshapiga mahesabu ya kukamilisha sasa ninashangaa iweje halmashauri nyingine mradi huohuo umekalimika kwa thamani ya fedha iliyoletwa nyie hamjakamilisha au umekamilika ila mmezalisha madeni, sitaki kusikia jambo hilo" RC Dendego

Mkuu huyo wa Mkoa amewasisitiza watendaji hao wa halmashauri kwa kila mkuu wa Idara kuweka mpango kazi wake kwa kufuata Ilani ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) inavyoelekeza kwa kuhakikisha kuwa yale yanayotakiwa na ilani hiyo yanatekelezwa kikamilifu.

Aidha, katika kikao kazi hicho RC Dendego, amewaelekeza maafisa elimu wa halmashauri hiyo kuhakikisha wanapandisha hali ya taaluma kwa kiwango cha juu na kukomesha utoro wa wanafunzi kwa kuwa elimu ni msingi wa maendeleo ya taifa.

Katibu Tawala Mkoa wa Singida Dkt. Fatuma Mganga, akisisitiza jambo kwenye kikao kazi hicho.

Katika hatua nyingine Mkuu wa Mkoa huyo amewahimiza watendaji hao kushirikiana kikamilifu katika ukusanyaji na usimamizi wa mapato ya halmashauri akisema bila mpango wa kifedha unaoeleweka haiwezekani kufanikisha malengo ya halmashauri.

Akizungumza na Idara ya Utumishi amesema inawajibu wa kusimamia haki za watumishi na kuhakikisha kuwa masuala ya kiutumishi yanashughulikiwa ipasavyo ikiwa ni pamoja na matumizi bora ya teknolojia katika kurahisisha shughuli za kiutumishi.

Hata hivyo,  RC Dendego, ametumia kikao hicho kuwataka Wakurugenzi wa Halmashauri mkoani humo kutowahamisha watumishi bila idhini ya Katibu Tawala wa Mkoa (RAS) ili kudhibiti uhaba wa watumishi na kuweka uwiano bora katika utoaji wa huduma.

Pia RC Dendego, amewaagiza wakaguzi wa ndani katika halmashauri hiyo kuwa macho na kutoruhusu dosari zozote kutokea bila kuchukua hatua akisema kuwa hataki kusikia kwamba kuna jambo limegundulika lakini halijaripotiwa au kushughulikiwa.

Kwaupande wa Idara ya Afya RC Dendego, amewaagiza wahudumu wa afya kuongeza uangalizi wa hali ya juu pindi wanapokuwa kazini hasa wakati wa kutembelea wodi kujua changamoto za wagonjwa ili kutoa huduma bora.

Katika hatua nyingine Mkuu wa Mkoa huyo alihitimisha kwa kuwaonya viongozi kuwa hataki kuona halmashauri inarudi nyuma katika utekelezaji wa majukumu na maendeleo hususan katika usimamizi wa miradi, elimu, mapato huku akiwataka walimu na maafisa taaluma kuhakikisha kuwa wana mipango inayotekelezeka kwa manufaa ya elimu.


Matangazo

  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2022_2023 SINGIDA RS July 01, 2022
  • MAJINA YA WALIOCHANGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA - 2023, MKOA WA SINGIDA December 14, 2022
  • TAARIFA YA MAPOKEZI YA FEDHA KWA KIPINDI CHA KUANZIA JULAI HADI OCTOBA, 2023 KWA AJILI YA UTEKELEZAJI WA SHUGHULI ZA MAENDELEO November 01, 2023
  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2021/2022 SINGIDA RS - GPN 2021 - 2022 July 01, 2021
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • DKT.MGANGA ASISITIZA MADAKTARI BINGWA KUTOA HUDUMA BORA

    May 05, 2025
  • WATUMISHI NA WAAJIRI HODARI MKOANI SINGIDA WAPOKEA TUZO

    May 02, 2025
  • KUELEKEA MEIMOSI,RC DENDEGO ATANGAZA FURSA ZA UWEKEZAJI

    April 25, 2025
  • MADAKTARI BINGWA WA DKT.SAMIA WABISHA HODI SINGIDA

    April 23, 2025
  • Angalia Zote

Video

Mkoa wa Singida waja na Mikakati ya Kuboresha Elimu
Video zaidi

Viungio vya Haraka

  • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
  • Mwongozo wa Matumizi ya TEHAMA Serikalini
  • Fomu ya Maombi ya Kusafiri Nje ya Nchi
  • MPANGO WA MANUNUZI MKOA WA SINGIDA
  • KUONA AJIRA ZA WAALIMU WA SAYANSI NA MAFUNDI SANIFU

Tovuti Muhimu

  • UTUMISHI
  • TAMISEMI
  • IKULU
  • WIZARA YA ELIMU
  • NECTA
  • WIZARA YA AFYA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Ramani ya Mkoa

Wasiliana Nasi

    SINGIDA

    Anuani: P O BOX 5 SINGIDA

    Simu: 2502170, 2502089

    Simu: 2502170, 2502089

    Barua Pepe: info@singida.go.tz ras@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Usiri
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

Copyright ©2023 Singida Regional Commisioner' Office . All rights reserved.