• Wasiliana Nasi |
    • Malalamiko |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
    • Blog |
Singida Regional Website

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Tovuti ya Mkoa wa Singida

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na dhima
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Ikungi
      • HISTORIA
    • Iramba
    • Manyoni
    • Mkalama
    • Singida
  • Halmashauri
    • H/W Ikungi
    • H/W Iramba
    • H/W Itigi
    • H/W Manyoni
    • H/W Mkalama
    • H/W Singida
    • H/M Singida
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Viwanda na Biashara
    • Madini
  • Huduma Zetu
    • Afya
      • Madaktari Bingwa
      • Huduma za Tiba
      • Huduma za Kinga
      • Ustawi wa Jamii
      • Afya ya Mazingira
      • Lishe
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba Wa Huduma Kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
    • Investment Guide
  • Kituo Cha Habari
    • Picha
    • Video
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma

RC Mahenge awataka wananchi kujitokeza kupanda miti kipindi hiki cha mvua.

Posted on: January 25th, 2022

Wananchi mkoani Singida wametakiwa kujitokeza kwa wingi katika zoezi la upandaji miti litakalofanyika kimkoa katika maeneo mbalimbali mkoani humo siku ya Jumamosi Januari 29, 2022 ili kuhifadhi na kuyalinda mazingira.

Wito huo umetolewa leo Januari 25, 2022 na Mkuu wa Mkoa huo Dkt. Binilith Mahenge wakati akikagua hali ya mazingira katika maeneo ya kuhifadhia taka ngumu yaliyopo Msufini, Nyuma ya Uwanja wa Liti, Standi ya Zamani, Stand Kuu ya Mabasi Misuna na Soko Kuu katika Manispaa ya Singida Mjini.

Akiongea na Wananchi hao Mkuu wa mkoa akawataka wananchi hao kujitokeza katika maeneo yao kupanda miti huku wengine wakiendelea na zoezi hilo katika maeneo ya kando ya Maziwa ya Singidani na Ziwa Kindai pamoja na kingo za Mito.

“Leo tumefanya ukaguzi wa usafi wa mazingira katika maeneo yetu ya Manispaa ya Singida lakini kubwa kuliko nitoe wito kwa Wananchi wote wa mkoa huu kujitokeza kwa wingi Siku ya Jumamosi ya tarehe 29/1/2022 kufanya usafi katika maeneo yetu yanayotuzunguka pamoja na kushiriki katika zoezi la upandaji miti katika kipindi hiki cha mvua” Alisema Dkt. Mahenge

Awali Magreth Mushi Mfanyabiashara wa Soko Kuu aliiomba Serikali kuwatenganishia eneo la kuhifadhia taka ngumu kati yao na wananchi wengine wanaoyazunguka maeneo hayo ili kuleta uwajibikaji, usimamizi na ufuatiliaji katika eneo hilo.

Amesema madampo hayo yasipofanyiwa usafi yanachafua hali ya hewa na nihatari kwa afya za wafanyabiashara na wateja wanoukuja kununua bidhaa zao.

Naye, Zaituni Ismail mmoja wa wafanyabiashara wa maeneo hayo akaiomba Serikali kuhakikisha taka hizo zinazolewa kila baada ya wiki moja ambapo alibainisha kwamba uwepo wa taka hizo kwa muda mrefu zinasababisha kukosekana kwa wateja hasa wa matunda na mbogamboga.

Baadhi ya wananchi waliojitokeza katika eneo la Dampo lililoko Soko Kuu kwaajili ya kumsikiliza Mkuu wa Mkoa wa Singida Dkt. Binilith Mahenge wakati wa ziara yake fupi ya kukagua usafi wa mazingira katika Manispaa ya Singida Mjini 


Matangazo

  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2022_2023 SINGIDA RS July 01, 2022
  • MAJINA YA WALIOCHANGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA - 2023, MKOA WA SINGIDA December 14, 2022
  • TAARIFA YA MAPOKEZI YA FEDHA KWA KIPINDI CHA KUANZIA JULAI HADI OCTOBA, 2023 KWA AJILI YA UTEKELEZAJI WA SHUGHULI ZA MAENDELEO November 01, 2023
  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2021/2022 SINGIDA RS - GPN 2021 - 2022 July 01, 2021
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • HUDUMA ZA KIBINGWA ZAWAFIKIA WAGONJWA ZAIDI YA 3000 SINGIDA.

    May 09, 2025
  • IKUNGI YAPEPERUSHA BENDERA KWA MIRADI YA KIMKAKATI.

    May 08, 2025
  • DKT.MGANGA ASISITIZA MADAKTARI BINGWA KUTOA HUDUMA BORA

    May 05, 2025
  • WATUMISHI NA WAAJIRI HODARI MKOANI SINGIDA WAPOKEA TUZO

    May 02, 2025
  • Angalia Zote

Video

Mkoa wa Singida waja na Mikakati ya Kuboresha Elimu
Video zaidi

Viungio vya Haraka

  • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
  • Mwongozo wa Matumizi ya TEHAMA Serikalini
  • Fomu ya Maombi ya Kusafiri Nje ya Nchi
  • MPANGO WA MANUNUZI MKOA WA SINGIDA
  • KUONA AJIRA ZA WAALIMU WA SAYANSI NA MAFUNDI SANIFU

Tovuti Muhimu

  • UTUMISHI
  • TAMISEMI
  • IKULU
  • WIZARA YA ELIMU
  • NECTA
  • WIZARA YA AFYA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Ramani ya Mkoa

Wasiliana Nasi

    SINGIDA

    Anuani: P O BOX 5 SINGIDA

    Simu: 2502170, 2502089

    Simu: 2502170, 2502089

    Barua Pepe: info@singida.go.tz ras@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Usiri
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

Copyright ©2023 Singida Regional Commisioner' Office . All rights reserved.