• Wasiliana Nasi |
    • Malalamiko |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
    • Blog |
Singida Regional Website

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Tovuti ya Mkoa wa Singida

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na dhima
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Ikungi
      • HISTORIA
    • Iramba
    • Manyoni
    • Mkalama
    • Singida
  • Halmashauri
    • H/W Ikungi
    • H/W Iramba
    • H/W Itigi
    • H/W Manyoni
    • H/W Mkalama
    • H/W Singida
    • H/M Singida
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Viwanda na Biashara
    • Madini
  • Huduma Zetu
    • Afya
      • Madaktari Bingwa
      • Huduma za Tiba
      • Huduma za Kinga
      • Ustawi wa Jamii
      • Afya ya Mazingira
      • Lishe
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba Wa Huduma Kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
    • Investment Guide
  • Kituo Cha Habari
    • Picha
    • Video
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma

RC Serukamba akabidhiwa madarasa mpya 29 na Ofisi 11 za Walimu Wilayani Ikungi, awapongeza Viongozi kwa ukamilishaji kwa wakati uliopangwa

Posted on: December 15th, 2022

Mkuu wa  Mkoa wa Singida, Peter Serukamba,amekabidhiwa madarasa mpya 29 na Ofisi 11 za Walimu zilizojengwa katika Wilayaya Ikungi na kusema kuanzia mwakani mkoa utaweka mkakati wa kuondoa matokeo yamtihani daraja la sifuri na nne kwa wanafunzi.

Akizungumza baada ya kukagua madarasa yaliyojengwa katika Shule zaSekondari Wilayani Ikungi, Mungaa na Issuna na kuzungumza na wananchi, RCSerukamba alisema Wilaya ya Ikungi imekuwa ya kwanza kati ya wilaya sita zamkoa huo kwa kutekeleza kwa wakati ujenzi wa vyumba vya madarasa.

Serukamba alisema Serikali imetoa fedha nyingi kwa ajili ya ujenziwa vyumba vya madarasa vitakayowawezesha wanafunzi kusoma katika mazingiramazuri hivyo halitakuwa jambo jema kwa wanafunzi kupata daraja la sifurikutokana na miundombinu bora na mazingira rafiki yanayowezesha upatikanaji waelimu bora kwa mwanafunzi na mwalimu kufundisha.

Alisema Mkoa wa Singida ulipewa na Serikali Kuu Sh. Bilioni 5.8kwa ajili ya kujenga madarasa mapya 290 lakini Mkoa uliamua kuweka mikakatiyake ambapo katika fedha hizo hizo mbali na kujenga madarasa hayo kiasi chafedha kingine kilitumika kujenga shule mpya saba za Sekondari kwa kushirikianana wananchi.

“Kuanzia mwakani nitakutana na walimu shule zote za Mkoa waSingida ili tujadialiane na kupanga mikakati ya namna ya kuondoa matokeo yamtihani ya ‘division zero na four’ kwa shule zote, “alisema RC Serukamba.

Serukamba alisema ili kuondokana na matokeo mabaya, walimuwatimize wajibu wao  vizuri wa kufundisha na wanafunzi nao wasome kwabidii kwani baada ya ujenzi wa madarasa haya hakutakuwa na kisingizo tena.

Alisema kati ya Wilaya zote za Mkoa wa Singida, Wilaya ya Ikungikatika ujenzi wa madarasa hayo iliweza ilijiongeza kwa kujenga ofisi 11 zawalimu ambazo hazikuwepo katika bajeti ya fedha zilizotolewa na Serikali.

Naye Mkuu wa Wiaya ya Ikungi, Jerry Muro, alisema ushirikiano waviongozi na wananchi katika Wilaya hiyo ndio umesaidia kufanikisha kukamilikakwa wakati ujenzi wa madarasa hayo.

Muro aliishukuru Serikali kwa kutoa kiasi cha Sh. Milioni 580 kwaajili ya ujenzi wa madarasa hayo na kwamba Serikali Wilayani humo itaendeleakusimamia na kutekeleza miradi yote ambayo Serikali imetoa fedha.

Naye Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Ikungi,Justice Kijazi alisema mwezi Septemba mwaka huu Halmashauri hiyo ilipokea kiasicha Sh. Milioni 580 kwa ajili ya ujenzi wa vyumba vya madarasa 29 katika shule16 za Sekondari.

Alisema baada ya kupokea fedha ziliingizwa kwenye akaunti ya shulehusika na ujenzi ukaanza ambapo  mbali na kujenga idadi hiyo ya madarasalakini pia madawati 1160, meza 1160 na viti 1160 yametengenezwa kwa ajili yamapokezi ya wanafunzi wa kidato cha kwanza 2023.

Mbunge wa Ikungi Mashariki Mheshimiwa Miraji Jumanne Mtaturu akizungumza na baadhi ya Wananchi wa Ikungi waliojitokeza kushuhudia makabidhiano ya vyumba vya madarasa wilayani humo.

Matangazo

  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2022_2023 SINGIDA RS July 01, 2022
  • MAJINA YA WALIOCHANGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA - 2023, MKOA WA SINGIDA December 14, 2022
  • TAARIFA YA MAPOKEZI YA FEDHA KWA KIPINDI CHA KUANZIA JULAI HADI OCTOBA, 2023 KWA AJILI YA UTEKELEZAJI WA SHUGHULI ZA MAENDELEO November 01, 2023
  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2021/2022 SINGIDA RS - GPN 2021 - 2022 July 01, 2021
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • HUDUMA ZA KIBINGWA ZAWAFIKIA WAGONJWA ZAIDI YA 3000 SINGIDA.

    May 09, 2025
  • IKUNGI YAPEPERUSHA BENDERA KWA MIRADI YA KIMKAKATI.

    May 08, 2025
  • DKT.MGANGA ASISITIZA MADAKTARI BINGWA KUTOA HUDUMA BORA

    May 05, 2025
  • WATUMISHI NA WAAJIRI HODARI MKOANI SINGIDA WAPOKEA TUZO

    May 02, 2025
  • Angalia Zote

Video

Mkoa wa Singida waja na Mikakati ya Kuboresha Elimu
Video zaidi

Viungio vya Haraka

  • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
  • Mwongozo wa Matumizi ya TEHAMA Serikalini
  • Fomu ya Maombi ya Kusafiri Nje ya Nchi
  • MPANGO WA MANUNUZI MKOA WA SINGIDA
  • KUONA AJIRA ZA WAALIMU WA SAYANSI NA MAFUNDI SANIFU

Tovuti Muhimu

  • UTUMISHI
  • TAMISEMI
  • IKULU
  • WIZARA YA ELIMU
  • NECTA
  • WIZARA YA AFYA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Ramani ya Mkoa

Wasiliana Nasi

    SINGIDA

    Anuani: P O BOX 5 SINGIDA

    Simu: 2502170, 2502089

    Simu: 2502170, 2502089

    Barua Pepe: info@singida.go.tz ras@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Usiri
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

Copyright ©2023 Singida Regional Commisioner' Office . All rights reserved.