• Wasiliana Nasi |
    • Malalamiko |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
    • Blog |
Singida Regional Website

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Tovuti ya Mkoa wa Singida

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na dhima
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Ikungi
      • HISTORIA
    • Iramba
    • Manyoni
    • Mkalama
    • Singida
  • Halmashauri
    • H/W Ikungi
    • H/W Iramba
    • H/W Itigi
    • H/W Manyoni
    • H/W Mkalama
    • H/W Singida
    • H/M Singida
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Viwanda na Biashara
    • Madini
  • Huduma Zetu
    • Afya
      • Madaktari Bingwa
      • Huduma za Tiba
      • Huduma za Kinga
      • Ustawi wa Jamii
      • Afya ya Mazingira
      • Lishe
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba Wa Huduma Kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
    • Investment Guide
  • Kituo Cha Habari
    • Picha
    • Video
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma

RC Serukamba apokea Mwenge wa Uhuru, asema utakagua miradi yenye thamani ya Bilioni 8.2

Posted on: August 9th, 2022

Mwenge wa Uhuru Mkoani Singida umejipanga kukagua miradi yenye thamani ya Bilioni 8.28 ikiwa ni jumla ya miradi 35 inayohusu Elimu, Afya, Utawala bora, Maji, Barabara na uwezeshaji wa vijana kiuchumi.

Akihutubia leo tarehe 09.08.2022 Mkuu wa Mkoa wa Singida Peter Serukamba  baada ya kupokea Mwenge wa Uhuru katika Kijiji cha Mseko kilichopo Wilaya ya Iramba  amesema kiasi hicho cha fedha kimejumisha Tsh.Milioni 84.203 ikiwa ni michango ya wananchi, Tsh.Milioni 173.29 ikiwa ni kutoka Halmashauri, Bilioni 6.449 kutoka Serikali Kuu na fedha kutoka kwa wahisani Sh.Bikioni 1.575.

Aidha amebainisha kwamba programu 18 zitazinduliwa na 11 zitawekewa jiwe la msingi ikiwa ni pamoja  na  programu 42 za Sensa, Rushwa, Malaria, Mapambano dhidi ya dawa za kulevya VVU na miradi ya Lishe.

RC Serukamba akaeleza kwamba katika kipindi cha awamu ya Sita Mkoa wa Singida umepokea jumla ya Tsh.Bilioni 270.371 kutoka Serikali Kuu, Serikali za Mitaa na kwa wadau wengine kwa ajili ya miradi ya maendeleo katika Sekta ya Afya Utawala bora Kilimo Uwezeshaji wa vijana Sekta ya Barabara Nishati Maji na Habari na Mawasimiano.

Amesema sekta ya Afya jumla ya Sh.Bilioni 28.4 zimetolewa kwa ajili ya ujenzi wa hospitali Nne (4), vituo vya Afya 15 na Ujenzi wa Zahanati utoaji wa chanjo na Ujenzi wa vyoo katika vituo vya kutolea huduma za Afya.

Aidha RC Serukamba  amesema miradi mingine ni ya sekta ya Kilimo ambapo wakulima walipatiwa mbegu za ruzuku ya Serikali yenye thamani ya Tsh. Bilioni 2.26 zilizotolewa kwa wakulima wa Mkoa huo.

Hata hivyo amesema jumla ya vikundi 409 vya wanawake, vijana na wenye ulemavu vimefaidika na mfuko wa Taifa wa TASAF na kugharimu Tsh. Bilioni 12.07

Kwa upande wake Sahili Nyanzabara Geraruma Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru kitaifa amezitaka kila Halmashauri kuhakikisha wanakuwa na nyaraka halisi zinazohusiana na miradi mbalimbali wakati wa ukaguzi.

Amesema kila Halmashauri inatakiwa kuonesha vielelezo vya namna ilivyo peleka fedha kwa vijana ikiwa ni pamoja na miradi iliyoanzishwa.

Amesema ni muhimu kuongeza usimamizi wa miradi ili iweze kuwasaidia wananchi kwa muda mrefu.

Matangazo

  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2022_2023 SINGIDA RS July 01, 2022
  • MAJINA YA WALIOCHANGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA - 2023, MKOA WA SINGIDA December 14, 2022
  • TAARIFA YA MAPOKEZI YA FEDHA KWA KIPINDI CHA KUANZIA JULAI HADI OCTOBA, 2023 KWA AJILI YA UTEKELEZAJI WA SHUGHULI ZA MAENDELEO November 01, 2023
  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2021/2022 SINGIDA RS - GPN 2021 - 2022 July 01, 2021
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • IKUNGI YAPEPERUSHA BENDERA KWA MIRADI YA KIMKAKATI.

    May 08, 2025
  • DKT.MGANGA ASISITIZA MADAKTARI BINGWA KUTOA HUDUMA BORA

    May 05, 2025
  • WATUMISHI NA WAAJIRI HODARI MKOANI SINGIDA WAPOKEA TUZO

    May 02, 2025
  • KUELEKEA MEIMOSI,RC DENDEGO ATANGAZA FURSA ZA UWEKEZAJI

    April 25, 2025
  • Angalia Zote

Video

Mkoa wa Singida waja na Mikakati ya Kuboresha Elimu
Video zaidi

Viungio vya Haraka

  • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
  • Mwongozo wa Matumizi ya TEHAMA Serikalini
  • Fomu ya Maombi ya Kusafiri Nje ya Nchi
  • MPANGO WA MANUNUZI MKOA WA SINGIDA
  • KUONA AJIRA ZA WAALIMU WA SAYANSI NA MAFUNDI SANIFU

Tovuti Muhimu

  • UTUMISHI
  • TAMISEMI
  • IKULU
  • WIZARA YA ELIMU
  • NECTA
  • WIZARA YA AFYA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Ramani ya Mkoa

Wasiliana Nasi

    SINGIDA

    Anuani: P O BOX 5 SINGIDA

    Simu: 2502170, 2502089

    Simu: 2502170, 2502089

    Barua Pepe: info@singida.go.tz ras@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Usiri
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

Copyright ©2023 Singida Regional Commisioner' Office . All rights reserved.