• Wasiliana Nasi |
    • Malalamiko |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
    • Blog |
Singida Regional Website

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Tovuti ya Mkoa wa Singida

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na dhima
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Ikungi
      • HISTORIA
    • Iramba
    • Manyoni
    • Mkalama
    • Singida
  • Halmashauri
    • H/W Ikungi
    • H/W Iramba
    • H/W Itigi
    • H/W Manyoni
    • H/W Mkalama
    • H/W Singida
    • H/M Singida
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Viwanda na Biashara
    • Madini
  • Huduma Zetu
    • Afya
      • Madaktari Bingwa
      • Huduma za Tiba
      • Huduma za Kinga
      • Ustawi wa Jamii
      • Afya ya Mazingira
      • Lishe
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba Wa Huduma Kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
    • Investment Guide
  • Kituo Cha Habari
    • Picha
    • Video
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma

RC SERUKAMBA ATAKA WAFANYABIASHARA KUZINGATIA MIONGOZO YA ULIPAJI KODI

Posted on: June 13th, 2023

MKUU wa Mkoa wa Singida, Peter Serukamba, amewataka wafanyabiashara mkoani hapa kuzingatia miongozo ya ulipaji kodi wanazostahili kulipa na utoaji wa stakabadhi za kieletroniki za EFD ili kukuza uchumi wa mtu mmoja na taifa kwa ujumla.

Akifungua mkutano wa Baraza la Biashara la Mkoa wa Singida jana, alisema Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) na Mamlaka za Serikali za Mitaa kuzingatia sheria inapotekeleza majukumu ya ukusanyaji kodi kwa wafanyabiashara.

Serukamba alisema Serikali imekuwa ikiboresha mazingira ya biashara kwa kuondoa tozo ambazo hazina tija ili kuongeza ukuaji wa biashara na uwekezaji hivyo wafanyabiashara waunge jitihada hizi za Serikali kwa kulipa kodi.

Alisema Serikali pia imekuwa ikichukua hatua mbalimbali kuhakikisha kuwa sekta za biashara na uwekezaji zinakuwa na kutoa mchango stahiki katika kukuza uchumi na pato la taifa kwa manufaa ya Watanzania.

Serukamba aliongeza kuwa ili kuhakikisha uboreshaji huu unakuwa na tija zaidi Serikali imeanzisha idara ya uwekezaji, viwanda na biashara katika Sekretarieti za mikoa na Mamlaka za Serikali za Mitaa ili kusimamia kwa karibu tasnia ya biashara nchini.

Alisema Mkoa wa Singida umebarikiwa kuwa na rasilimali nyingi hivyo sekta za umma na binafsi zinapaswa kufanya kazi kwa pamoja ili kuwaletea wananchi maendeleo na hivyo kukuza uchumi.

"Ndoto yangu ni kuifanya Singida kuwa kitovu cha biashara na uwekezaji nchini na chombo muhimu kitakachonisaidia kutimiza ndoto hii ni Baraza la Biashara la Mkoa hivyo tuweke mpango mkakati wa kufanya kazi ndani ya miaka mitatu kwa kutangaza shughuli za biashara na uwekezaji," alisema Serukamba.

Aliongeza kuwa Dunia kwa sasa inakabiliwa na mabadiliko makubwa ya teknolojia ambayo yanasababisha kukua kwa haraka kwa uchumi hivyo jitihada zinahitajika kujipanga kukabiliana nazo kwa kuimarisha mazingira wezeshi ya wafanyabiashara.

"Kasi hii ya ukuaji wa teknolojia imeendelea kuibua changamoto mbalimbali katika mazingira ya biashara ambazo zinahitaji utatuzi kwa njia ya majadiliano kuzipitia ufumbuzi changamoto zote zinazokabili ufanyaji wa biashara kwa kuzingatia miongozo iliyopo," alisema Serukamba.

Naye Mwenyekiti wa Chemba ya Wafanyabiashara Wenye Viwanda na Kilimo (TCCIA) Mkoa wa Singida, Kitila Katala, alisema sekta binafsi imekuwa ikikabiliwa na mamlaka nyingi za Udhibiti ambazo hudai tozo zaidi ya 18 na hivyo kuongeza mzigo mkubwa kwa wafanyabiashara.

Alisema Serikali iweke utaratibu kwamba tozo zote hizo zilipwe kwa mamlaka moja ili kupunguza mtafaruku na kuwepo majadiliano badala ya kutumia nguvu katika kutekeleza majukumu.

"Mfano hivi karibuni hapa Manispaa ya Singida wafanyabiashara waliofungiwa biashara zao kwa kudaiwa tozo ya huduma (service levy) bila hata kupatiwa muda wa kunieleza ili wakubaliane cha kulipa," alisema Katala.

Kuhusu mashine za kielekroniki za EFD alisema zina ukomo wa kutumia ambapo wafanyabiashara wamekuwa wakitumia fedha nyingi kuzifanyia ukarabati na kuiomba Serikali kama itawezekana mzigo wa kuzikarabati uwe unafanywa na Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA).

Kwa upande wake Afisa Biashara kutoka Mamlaka ya Maendeleo ya Biashara Tanzania (TanTrade), Herbert Hatibu, alisema wafanyabiashara wawe wanashirikiana na mamlaka hiyo katika kutangaza biashara zao kupitia maonyesho biashara ambayo yamekuwa yakiandakiwa na TanTrade.

Matangazo

  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2022_2023 SINGIDA RS July 01, 2022
  • MAJINA YA WALIOCHANGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA - 2023, MKOA WA SINGIDA December 14, 2022
  • TAARIFA YA MAPOKEZI YA FEDHA KWA KIPINDI CHA KUANZIA JULAI HADI OCTOBA, 2023 KWA AJILI YA UTEKELEZAJI WA SHUGHULI ZA MAENDELEO November 01, 2023
  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2021/2022 SINGIDA RS - GPN 2021 - 2022 July 01, 2021
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • "WAHITIMU MSIBWETEKE,JIENDELEZENI KATIKA FANI ILI MJIAJIRI"-DKT.MGANGA

    May 30, 2025
  • DKT.MGANGA:"WATUMISHI MSIKUBALI KUTUMIKA VIBAYA,KUWENI NA UTAMBULISHO MZURI"

    May 27, 2025
  • ANUANI ZA MAKAZI KUJA NA FURSA LUKUKI ZA MAENDELEO KWA WANANCHI

    May 26, 2025
  • WANAFUNZI NI SALAMA CHINI YA MRADI WA SHULE BORA .

    May 26, 2025
  • Angalia Zote

Video

Mkoa wa Singida waja na Mikakati ya Kuboresha Elimu
Video zaidi

Viungio vya Haraka

  • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
  • Mwongozo wa Matumizi ya TEHAMA Serikalini
  • Fomu ya Maombi ya Kusafiri Nje ya Nchi
  • MPANGO WA MANUNUZI MKOA WA SINGIDA
  • KUONA AJIRA ZA WAALIMU WA SAYANSI NA MAFUNDI SANIFU

Tovuti Muhimu

  • UTUMISHI
  • TAMISEMI
  • IKULU
  • WIZARA YA ELIMU
  • NECTA
  • WIZARA YA AFYA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Ramani ya Mkoa

Wasiliana Nasi

    SINGIDA

    Anuani: P O BOX 5 SINGIDA

    Simu: 2502170, 2502089

    Simu: 2502170, 2502089

    Barua Pepe: info@singida.go.tz ras@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Usiri
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

Copyright ©2023 Singida Regional Commisioner' Office . All rights reserved.