• Wasiliana Nasi |
    • Malalamiko |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
    • Blog |
Singida Regional Website

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Tovuti ya Mkoa wa Singida

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na dhima
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Ikungi
      • HISTORIA
    • Iramba
    • Manyoni
    • Mkalama
    • Singida
  • Halmashauri
    • H/W Ikungi
    • H/W Iramba
    • H/W Itigi
    • H/W Manyoni
    • H/W Mkalama
    • H/W Singida
    • H/M Singida
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Viwanda na Biashara
    • Madini
  • Huduma Zetu
    • Afya
      • Madaktari Bingwa
      • Huduma za Tiba
      • Huduma za Kinga
      • Ustawi wa Jamii
      • Afya ya Mazingira
      • Lishe
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba Wa Huduma Kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
    • Investment Guide
  • Kituo Cha Habari
    • Picha
    • Video
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma

RC SERUKAMBA ATOA AGIZO KWA MANISPAA, ENEO DAMPO LA MANGA KUJENGWA MAEGESHO YA MALORI

Posted on: December 13th, 2022

Mkuu wa Mkoa wa Singida, Peter Serukamba, ameiagiza Halmashauri ya Manispaa ya Singida kuharakisha utekelezaji wa kulibadilisha matumizi dampo la Manga lililopo kijiji cha Mtipa kandokando ya barabara kuu ya Singida-Mwanza kuwa eneo la maegesho ya malori na kujenga hoteli na migahawa.

Akizungumza baada ya kutembelea dampo hilo, alisema eneo hilo yatakapojengwa maegesho, hoteli na vituo vya mafuta kitakuwa chanzo kizuri cha mapato ya Manispaa ya Singida kwa kuwa magari yatatoa ushuru na watu watakaowekeza hapo watatoa kodi.

Aidha, Serukamba ameziagiza Wilaya zote kuanza mkakati wa kupanda miti kandokando ya barabara na kufanya usafi kila siku ya Jumamosi kuanzia mwakani ili kutunza mazingira na kupendezesha miji.

Naye Meya wa Manispaa ya Singida, Yagi Kiaratu, amesema maelekezo ya Mkuu wa Mkoa wa Singida yatazingatiwa na kwamba Manispaa ilikuwa imeshaanza kubadilisha matumizi ya dampo la Manga.

Amesema dampo hilo wakati linaanzishwa mji wa Singida ulikuwa haujapanuka lakini baada ya mji kupanuka hivyo limetafutwa eneo la Mwankonko nje kidogo ya mji ambalo limeanza kutumika kama dampo jipya.

"Mpango wa Manispaa  eneo lote la dampo la Manga litapimwa kujua ukubwa wake na baadaye itapitishwa michoro inayokidhi eneo hilo na baada ya hapo tutajenga hoteli, nyumba za kulala wageni, maegesho ya magari pamoja  na eneo la mama lishe ili wanaoegesha magari yao waweze kupata huduma," Kiaratu amesema.

Kiaratu amesema kwamba Manispaa ya Singida itashughulika na suala la ujenzi wa maegesho ya magari lakini huduma nyingine zitafanywa na wawekezaji watakaopewa eneo hilo kuwekeza.

Aliongeza kuwa sheria ndogo za Manispaa zilizopo zitahuishwa zianze kutumika haraka na atakayepatikana akitupa taka ovyo atakamatwa na kutozwa faini kati ya Sh. 50,000 hadi 300,000.

Meya alisema Manispaa itaanza kuvitumia vikundi kazi vilivyo kila mtaa kwa ajili kukamata watu wanaochafua mazingira ili wachukuliwe hatua kwa mujibu wa sheria.

MWISHO

Matangazo

  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2022_2023 SINGIDA RS July 01, 2022
  • MAJINA YA WALIOCHANGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA - 2023, MKOA WA SINGIDA December 14, 2022
  • TAARIFA YA MAPOKEZI YA FEDHA KWA KIPINDI CHA KUANZIA JULAI HADI OCTOBA, 2023 KWA AJILI YA UTEKELEZAJI WA SHUGHULI ZA MAENDELEO November 01, 2023
  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2021/2022 SINGIDA RS - GPN 2021 - 2022 July 01, 2021
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • DKT.MGANGA ASISITIZA MADAKTARI BINGWA KUTOA HUDUMA BORA

    May 05, 2025
  • WATUMISHI NA WAAJIRI HODARI MKOANI SINGIDA WAPOKEA TUZO

    May 02, 2025
  • KUELEKEA MEIMOSI,RC DENDEGO ATANGAZA FURSA ZA UWEKEZAJI

    April 25, 2025
  • MADAKTARI BINGWA WA DKT.SAMIA WABISHA HODI SINGIDA

    April 23, 2025
  • Angalia Zote

Video

Mkoa wa Singida waja na Mikakati ya Kuboresha Elimu
Video zaidi

Viungio vya Haraka

  • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
  • Mwongozo wa Matumizi ya TEHAMA Serikalini
  • Fomu ya Maombi ya Kusafiri Nje ya Nchi
  • MPANGO WA MANUNUZI MKOA WA SINGIDA
  • KUONA AJIRA ZA WAALIMU WA SAYANSI NA MAFUNDI SANIFU

Tovuti Muhimu

  • UTUMISHI
  • TAMISEMI
  • IKULU
  • WIZARA YA ELIMU
  • NECTA
  • WIZARA YA AFYA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Ramani ya Mkoa

Wasiliana Nasi

    SINGIDA

    Anuani: P O BOX 5 SINGIDA

    Simu: 2502170, 2502089

    Simu: 2502170, 2502089

    Barua Pepe: info@singida.go.tz ras@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Usiri
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

Copyright ©2023 Singida Regional Commisioner' Office . All rights reserved.