• Wasiliana Nasi |
    • Malalamiko |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
    • Blog |
Singida Regional Website

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Tovuti ya Mkoa wa Singida

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na dhima
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Ikungi
      • HISTORIA
    • Iramba
    • Manyoni
    • Mkalama
    • Singida
  • Halmashauri
    • H/W Ikungi
    • H/W Iramba
    • H/W Itigi
    • H/W Manyoni
    • H/W Mkalama
    • H/W Singida
    • H/M Singida
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Viwanda na Biashara
    • Madini
  • Huduma Zetu
    • Afya
      • Madaktari Bingwa
      • Huduma za Tiba
      • Huduma za Kinga
      • Ustawi wa Jamii
      • Afya ya Mazingira
      • Lishe
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba Wa Huduma Kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
    • Investment Guide
  • Kituo Cha Habari
    • Picha
    • Video
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma

RC SERUKAMBA: SINGIDA INAWEZA KUWA KINARA UKUSANYAJI MAPATO KILA MTU AKIWAJIBIKA

Posted on: September 5th, 2023

MKUU wa Mkoa wa Singida, Peter Serukamba amesema Mkoa huo unaweza kuwa kinara wa ukusanyaji wa mapato, uhifadhi wa mazingira na usimamizi wa miradi iwapo tu watendaji watafanya kazi kwa kujituma na kushirikiana badala ya kuyaachia baadhi ya makundi kufanya kazi hiyo.

Serukamba amesema hayo jana ( 4 Septemba, 2023)  wakati akizungumza na Wakurugenzi, Wakuu wa Wilaya, Wenyeviti wa Halmashauri na wataalam mbalimbali kutoka Halmashauri za Mkoa wa Singida katika kikao kazi kilichofanyika katika ofisi ya Mkuu wa Mkoa Singida.

Alisema  Halmashauri zinatakiwa kuimarisha ukusanyaji wa mapato na kuhakikisha mashine za kukusanya fedha (POSS) zisitumike feki.

Alisema kumekuwa na changamoto ya ukusanyaji wa mapato na matumizi ya POSS feki hivyo kuukosesha mkoa kupata mapato stahiki ambapo aliviomba vyombo vya dola ikiwamo na Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) kusaidia kufanya uchunguzi kwenye mageti ya ukaguzi wa mazao yanayosafirishwa.

'' Tukifanya kazi vizuri katika uhifadhi wa mazingira, ukusanyaji mapato, ukamilishaji wa miradi kwa wakati na kuwa timu moja, siku moja  tutakuwa namba moja kitaifa,'' alisema Serukamba.

Naye Katibu Tawala Mkoa wa Singida, Dkt. Fatuma Mganga akizungumza kwenye kikao hicho aliwaomba Wakurugenzi pindi wanapopokea fedha za miradi kabla ya kuanza kutekelezwa watoke ofisini na kwenda kujua bei za vifaa badala ya kuwaachia watu wa manunuzi pekee ambao wamekuwa na changamoto ya kuweka bei ya juu.

'' Miradi mingi imekuwa haikamiliki kutokana na fedha zilizotolewa na Serikali kumalizika kabla haijaisha na hiyo inasabishwa kununua vifaa kwa bei kubwa lakini Wakurugenzi wakitoka na timu yao watawakuta wauzaji wa vifaa hivyo kwa bei ya chini.'' alisema Dkt. Fatuma Mganga.

Mganga akitolea mfano alisema alipokuwa Mkurugenzi wa Halmashauri wakati wanataka kutegeneza milango waliwaomba watu wa manunuzi wawape bei yao ambapo walisema ni Sh.Milioni 72 na walipotoka kutafuta bei kwa watu wengine alikuwepo wa Sh.Milioni 50 na mwingine Sh.Milioni 48 na hivyo kumpa kazi hiyo aliyekuwa na bei ya chini ambaye alifanya kazi hiyo kwa viwango vya hali ya juu.

Katika hatua nyingine Mganga aliwaomba Wakurugenzi hao kujenga tabia ya kwenda kujifunza kwa wenzao ambao wanafanikiwa kukamilisha miradi ya maendeleo kwa wakati na kwa fedha zilezile walizopokea kama wao.

Alisema utakuta Serikali imetoa fedha kiwango sawa lakini katika ukamilishaji wa miradi kwa fedha hizo hizo Halmashauri zingine zinakamilisha miradi iwe ya ujenzi wa shule au kituo cha afya na halmashauri nyingine utakuta ujenzi wake upo hatua ya msingi.

Katika kikao hicho pamoja na mambo mengine Wakurugenzi na Wakuu wa Wilaya walitoa taarifa za ukusanyaji wa mapato pamoja na miradi mbalimbali inayotekelezwa kwenye Wilaya zao.

Matangazo

  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2022_2023 SINGIDA RS July 01, 2022
  • MAJINA YA WALIOCHANGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA - 2023, MKOA WA SINGIDA December 14, 2022
  • TAARIFA YA MAPOKEZI YA FEDHA KWA KIPINDI CHA KUANZIA JULAI HADI OCTOBA, 2023 KWA AJILI YA UTEKELEZAJI WA SHUGHULI ZA MAENDELEO November 01, 2023
  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2021/2022 SINGIDA RS - GPN 2021 - 2022 July 01, 2021
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • IKUNGI YAPEPERUSHA BENDERA KWA MIRADI YA KIMKAKATI.

    May 08, 2025
  • DKT.MGANGA ASISITIZA MADAKTARI BINGWA KUTOA HUDUMA BORA

    May 05, 2025
  • WATUMISHI NA WAAJIRI HODARI MKOANI SINGIDA WAPOKEA TUZO

    May 02, 2025
  • KUELEKEA MEIMOSI,RC DENDEGO ATANGAZA FURSA ZA UWEKEZAJI

    April 25, 2025
  • Angalia Zote

Video

Mkoa wa Singida waja na Mikakati ya Kuboresha Elimu
Video zaidi

Viungio vya Haraka

  • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
  • Mwongozo wa Matumizi ya TEHAMA Serikalini
  • Fomu ya Maombi ya Kusafiri Nje ya Nchi
  • MPANGO WA MANUNUZI MKOA WA SINGIDA
  • KUONA AJIRA ZA WAALIMU WA SAYANSI NA MAFUNDI SANIFU

Tovuti Muhimu

  • UTUMISHI
  • TAMISEMI
  • IKULU
  • WIZARA YA ELIMU
  • NECTA
  • WIZARA YA AFYA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Ramani ya Mkoa

Wasiliana Nasi

    SINGIDA

    Anuani: P O BOX 5 SINGIDA

    Simu: 2502170, 2502089

    Simu: 2502170, 2502089

    Barua Pepe: info@singida.go.tz ras@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Usiri
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

Copyright ©2023 Singida Regional Commisioner' Office . All rights reserved.