• Wasiliana Nasi |
    • Malalamiko |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
    • Blog |
Singida Regional Website

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Tovuti ya Mkoa wa Singida

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na dhima
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Ikungi
      • HISTORIA
    • Iramba
    • Manyoni
    • Mkalama
    • Singida
  • Halmashauri
    • H/W Ikungi
    • H/W Iramba
    • H/W Itigi
    • H/W Manyoni
    • H/W Mkalama
    • H/W Singida
    • H/M Singida
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Viwanda na Biashara
    • Madini
  • Huduma Zetu
    • Afya
      • Madaktari Bingwa
      • Huduma za Tiba
      • Huduma za Kinga
      • Ustawi wa Jamii
      • Afya ya Mazingira
      • Lishe
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba Wa Huduma Kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
    • Investment Guide
  • Kituo Cha Habari
    • Picha
    • Video
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma

RC SINGIDA AMWAKILISHA MAKAMU WA RAIS HARAMBEE UJENZI KANISA ZAIDI YA SH. MILIONI 137.3 ZILIPATIKANA

Posted on: July 28th, 2024

Makamu wa Rais Dk. Philip Isdor Mpango, amesema Serikali inatambua na kuthamini mchango wa  taasisi za dini katika kudumisha hali ya amani na utulivu likiwemo dhehebu la dini la Kanisa la Anglicana ambalo hutoa huduma za Injili na Utume kwa pamoja katika ngazi ya kitaifa pamoja na kuendelea kufanya miradi mbalimbali ya maendeleo hapa nchini.

Katika hotuba yake iliyosomwa mkoani Singida kwa niaba na Mkuu wa mkoa huo Mheshimiwa Halima Dendego, kupitia harambee ya ukamilishaji wa jengo la Kanisa la Parish ya Mtakatifu Paulo, Dayosisi ya Rift Valley mjini Singida, Makamu wa Rais amesema anatambua kazi kubwa inayofanywa na Kanisa la Anglican Tanzania hasa kwenye eneo la elimu kwa ajili ya kuleta maendeleo ya mwananchi mmoja mmoja kikanda na Taifa kwa ujumla.

"Taasisi za dini ni muhimu sana kwa maendeleo ya Taifa letu kazi hii kubwa inayoendelea kufanywa na taasisi hizi imekuwa ni muhimili na kiungo muhimu kati ya Serikali, wananchi na madhehebu kama hili hapa leo...niwaombe endeleeni na moyo huu huu kwa ajili ya faida ya watu wetu wa sasa na hata katika kizazi kijacho...," alibainisha Dk. Mpango.

Aidha Dk. Mpango alihimiza umuhimu wa kuvumiliana na kuendelea kudumisha hali ya amani ili kuzidi kujenga na kuimarisha utulivu hapa nchini ulioasisiwa na watangulizi wa Taifa hili akiwemo hayati Mwalimu Julius K. Nyerere na Sheikh Amani Abeid Karume.

Katika harambee hiyo kwa niaba ya Makamu wa Rais, Mkuu wa mkoa wa Singida Halima Dendego, aliwasilisha zaidi ya Sh. Milioni 50/-, zikiwa ni fedha taslimu alizoziwasilisha kwa uongozi wa Kanisa la Anglican Tanzania kwa Askofu wa Dayosisi ya Rift Valley Mchungaji John Lupaa, na akawashukuru wananchi na viongozi wote wa mkoa zikiwemo Halmashauri za Wilaya, Sekretarieti ya mkoa na wakuu wa Wilaya kwa kuunga mkono hadi kufanikisha zoezi hilo.

Mapema akisoma risala Katibu wa Kanisa hilo Baraka Mazengo, alisema kuwa tangu ujenzi wa jengo jipya la Kanisa uanze mwaka 2018 hadi sasa mradi huo umetumia zaidi ya Sh. Milioni 313.3/-, na harambee inalenga kukusanya takribani Sh. Milioni 646/-, kuweza kukamilisha kupauliwa kwa jengo hilo litakalokuwa na uwezo wa kuingiza waumini 1,800 kwa mara moja.

Mazengo alifafanua kuwa Kanisa linatarajia hadi kufikia mwishoni mwa mwezi Disemba mwaka huu mradi huo uwe umekamilika.

Kwa upande wake Askofu wa Dayosisi ya Rift Valley John Lupaa, amemshukuru Mheshimiwa Makamu wa Rais na Serikali ya Tanzania inayoongozwa na Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan, kuweza kuwaletea wananchi maendeleo kupitia sekta mbalimba kama vile afya, elimu, kilimo, maji na miundombinu ya barabara.

Kupitia harambee hiyo Askofu Lupaa, aliahidi Serikali kuwa fedha zote zilizopatikana zitatumika kwa uaminifu mkubwa katika mipango iliyokusudiwa kwa ajili ya kukamilisha mradi wa ujenzi wa jengo la Kanisa.

Kwenye harambee hiyo zaidi ya Sh. Milioni 137.3/- zilipatikana zikiwemo fedha taslimu na ahadi, kati ya Sh. Milioni 646/- zilizokusudiwa fedha zilizokusanywa zikiwemo fedha taslimu Sh. Milioni 56.9/- na ahadi Sh. Milioni 80.4/-.

MWISHO.

Matangazo

  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2022_2023 SINGIDA RS July 01, 2022
  • MAJINA YA WALIOCHANGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA - 2023, MKOA WA SINGIDA December 14, 2022
  • TAARIFA YA MAPOKEZI YA FEDHA KWA KIPINDI CHA KUANZIA JULAI HADI OCTOBA, 2023 KWA AJILI YA UTEKELEZAJI WA SHUGHULI ZA MAENDELEO November 01, 2023
  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2021/2022 SINGIDA RS - GPN 2021 - 2022 July 01, 2021
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • IKUNGI YAPEPERUSHA BENDERA KWA MIRADI YA KIMKAKATI.

    May 08, 2025
  • DKT.MGANGA ASISITIZA MADAKTARI BINGWA KUTOA HUDUMA BORA

    May 05, 2025
  • WATUMISHI NA WAAJIRI HODARI MKOANI SINGIDA WAPOKEA TUZO

    May 02, 2025
  • KUELEKEA MEIMOSI,RC DENDEGO ATANGAZA FURSA ZA UWEKEZAJI

    April 25, 2025
  • Angalia Zote

Video

Mkoa wa Singida waja na Mikakati ya Kuboresha Elimu
Video zaidi

Viungio vya Haraka

  • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
  • Mwongozo wa Matumizi ya TEHAMA Serikalini
  • Fomu ya Maombi ya Kusafiri Nje ya Nchi
  • MPANGO WA MANUNUZI MKOA WA SINGIDA
  • KUONA AJIRA ZA WAALIMU WA SAYANSI NA MAFUNDI SANIFU

Tovuti Muhimu

  • UTUMISHI
  • TAMISEMI
  • IKULU
  • WIZARA YA ELIMU
  • NECTA
  • WIZARA YA AFYA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Ramani ya Mkoa

Wasiliana Nasi

    SINGIDA

    Anuani: P O BOX 5 SINGIDA

    Simu: 2502170, 2502089

    Simu: 2502170, 2502089

    Barua Pepe: info@singida.go.tz ras@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Usiri
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

Copyright ©2023 Singida Regional Commisioner' Office . All rights reserved.