• Wasiliana Nasi |
    • Malalamiko |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
    • Blog |
Singida Regional Website

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Tovuti ya Mkoa wa Singida

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na dhima
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Ikungi
      • HISTORIA
    • Iramba
    • Manyoni
    • Mkalama
    • Singida
  • Halmashauri
    • H/W Ikungi
    • H/W Iramba
    • H/W Itigi
    • H/W Manyoni
    • H/W Mkalama
    • H/W Singida
    • H/M Singida
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Viwanda na Biashara
    • Madini
  • Huduma Zetu
    • Afya
      • Madaktari Bingwa
      • Huduma za Tiba
      • Huduma za Kinga
      • Ustawi wa Jamii
      • Afya ya Mazingira
      • Lishe
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba Wa Huduma Kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
    • Investment Guide
  • Kituo Cha Habari
    • Picha
    • Video
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma

RC Singida Atembelea miradi Itigi.

Posted on: September 23rd, 2021

Mkuu wa Mkoa wa Singida Dkt.Binilith Mahenge ameupongeza uongozi wa Hospitali ya St.Gaspar Itigi kutokana na huduma Bora za kibingwa wanazozitoa kwa wananchi wa Singida na Mikoa ya jirani.

Pongezi hizo amezitoa hivi karibuni alipofanya ziara Katika Wilaya ya Itigi Mkoani hapo Katika Hospitali ya St.Gaspar Itigi  na kutembelea Skimu ya Umwagiliaji ya Itagata iliyopo Kijiji Cha Itagata.

Aidha Dkt.Mahenge akijibu hoja maombi ya Mkurugenzi wa Hospitali hiyo yaliyosomwa na  Fr Justin Boniface RC amesema Serikali itaendelea kutoa ruzuku kwa wananchi wake Katika sekta ya afya ili waweze kuimarisha Maisha yao.

Amesema pamoja na huduma nzuri na vipimo vinavyopatikana Katika Hospitali hiyo ni vyema kila.mwanachi akapata bima ya afya iliyoboreshwa ili kupata unafuu Lindi wapatapo maradhi.

Ametoa wito kwa madaktari na viongozi hao kuhalikisha huduma hizo zinaendelea kuboreshwa kuongeza mashine nyengine ili kuondoa usumbufu kwa wagonjwa kuenda mikoa.mingine kwa ajili ya vipimo alisema Dkt.Mahenge.

Akiwa Hospitalinj hapo Mkuu wa Mkoa alitembelea miundombinu mbalimbali ya Hospitali hiyo pamoja na mashine ya vipimo mbalimbali


Aidha Mkurugenzi mtendaji wa Hospitali hiyo  Fr. Justin Bonifasi aliomba Serikali iwafutie deni  lenye thamani ya shilingi milioni 333,389,925 linalodaiwa na TRA ombi ambalo RC aliwambia walete ofsini kwake kwa maandishi ili aweze kuguatilia.

Mkurugenzi huyo amesema endapo watalazimika kulipia  deni hilo wata athirika kiuchumi na watakao umia zaidi ni wananchi zaidi.

Katika hatua nyingine  Dkt.Binilith Mahenge amewataka  Viongozi wa Wilaya ya Itigi Mkoani Singida  kuangalia upya  utaratibu wa kuyagawa mashamba kwa wakulima  katika Skimu ya Umwagiliaji ya Itagata Wilayani hapo ili iweze kuwa na Tija katika mkoa.

Maelezo hayo ameyatoa  baada ya kutembelea Skimu hiyo na  kubaini uwepo wa mashamba makubwa ambayo hayatumiki.

Amesema wapo watu waliohodhi mashamba hayo bila kuyatumia wakati maji yapo ya kutosha huku wakisingizia ubovu wa miundombinu ya Barabara na uwepo wa vichuguu.

Akiongea na wanakiji wa eneo hilo Dkt Mahenge ametaka kuitishwa haraka kwa Mkutano utakao husisha Wakulima wote wa Skimu  na Viongozi wa maeneo hayo ili watafakari namna ya kuyagawa mashamba hayo upya kwa wakulima ambao wana utayari.

Aidha amebainisha  kwamba Serikali imetoa zaidi ya bilioni 2.1kwa ajili ya utengenezaji wa Skimu hiyo lakini matokeo yake imekuwa ikitumiwa na watu wachache huku ikiendelea kuwa na tija ndogo.

RC Mahenge amewataka Viongozi wa Skimu hiyo kuhakisha msimu unaoanza wa kilimo mashamba yote ya Skimu hiyo yanatumika kulima kilimo cha kibiashara.

Mwisho

Matangazo

  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2022_2023 SINGIDA RS July 01, 2022
  • MAJINA YA WALIOCHANGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA - 2023, MKOA WA SINGIDA December 14, 2022
  • TAARIFA YA MAPOKEZI YA FEDHA KWA KIPINDI CHA KUANZIA JULAI HADI OCTOBA, 2023 KWA AJILI YA UTEKELEZAJI WA SHUGHULI ZA MAENDELEO November 01, 2023
  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2021/2022 SINGIDA RS - GPN 2021 - 2022 July 01, 2021
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • DKT.MGANGA ASISITIZA MADAKTARI BINGWA KUTOA HUDUMA BORA

    May 05, 2025
  • WATUMISHI NA WAAJIRI HODARI MKOANI SINGIDA WAPOKEA TUZO

    May 02, 2025
  • KUELEKEA MEIMOSI,RC DENDEGO ATANGAZA FURSA ZA UWEKEZAJI

    April 25, 2025
  • MADAKTARI BINGWA WA DKT.SAMIA WABISHA HODI SINGIDA

    April 23, 2025
  • Angalia Zote

Video

Mkoa wa Singida waja na Mikakati ya Kuboresha Elimu
Video zaidi

Viungio vya Haraka

  • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
  • Mwongozo wa Matumizi ya TEHAMA Serikalini
  • Fomu ya Maombi ya Kusafiri Nje ya Nchi
  • MPANGO WA MANUNUZI MKOA WA SINGIDA
  • KUONA AJIRA ZA WAALIMU WA SAYANSI NA MAFUNDI SANIFU

Tovuti Muhimu

  • UTUMISHI
  • TAMISEMI
  • IKULU
  • WIZARA YA ELIMU
  • NECTA
  • WIZARA YA AFYA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Ramani ya Mkoa

Wasiliana Nasi

    SINGIDA

    Anuani: P O BOX 5 SINGIDA

    Simu: 2502170, 2502089

    Simu: 2502170, 2502089

    Barua Pepe: info@singida.go.tz ras@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Usiri
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

Copyright ©2023 Singida Regional Commisioner' Office . All rights reserved.