• Wasiliana Nasi |
    • Malalamiko |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
    • Blog |
Singida Regional Website

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Tovuti ya Mkoa wa Singida

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na dhima
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Ikungi
      • HISTORIA
    • Iramba
    • Manyoni
    • Mkalama
    • Singida
  • Halmashauri
    • H/W Ikungi
    • H/W Iramba
    • H/W Itigi
    • H/W Manyoni
    • H/W Mkalama
    • H/W Singida
    • H/M Singida
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Viwanda na Biashara
    • Madini
  • Huduma Zetu
    • Afya
      • Madaktari Bingwa
      • Huduma za Tiba
      • Huduma za Kinga
      • Ustawi wa Jamii
      • Afya ya Mazingira
      • Lishe
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba Wa Huduma Kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
    • Investment Guide
  • Kituo Cha Habari
    • Picha
    • Video
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma

RC SINGIDA ATOA SIKU 7 MIRADI YA SEQUIP IWE IMEKAMILIKA

Posted on: September 18th, 2023

MKUU wa Mkoa wa Singida Peter Serukamba, ametoa siku saba (7) kwa halmashauri ya Wilaya ya Iramba, Mkalama, Singida Dc na Manispaa kuhakikisha Mradi wa Kuimarisha Elimu ya Sekondari (SEQUIP) inakamilika na kukabidhiwa ifikapo tarehe 25 Septemba mwaka huo.

Ametoa agizo hilo leo tarehe 18 Septemba, 2023 kwa Wakuu wa Wilaya na Wakurugenzi alipokuwa akifanya ziara ya kukagua ujenzi wa miradi hiyo ambayo inasimamiwa na Wakuu wa Wilaya na Wakurugenzi wa halmashauri husika.

Serukamba akizungumza na Watendaji hao amesema kuwa Mkandarasi ambaye anachelewesha kazi wakati vifaa vyote vipo anatakiwa kupunguziwa kazi na kupewa mtu mwingine ambaye anaonesha kuwa na juhudi za kufanya kazi.

"Haiwezekani kuna vifaa vyote ambavyo vinastahili kutumika kwenye ujenzi lakini Mkandarasi anasuasua na napenda kuwaelekeza kama kuna hiyo hali Mkandarasi mpunguzie kazi na apewe fundi mwingine”

"Hatuwezi kuona kazi zinalala kwa ajili ya mtu ambaye anafanya makusudi au kama mtu mmepaana naye mfano milioni sita lakini kazi inaenda taratibu basi mwambie kuwa utampa milioni tatu na nusu na pesa nyingine atapewa mkandarasi ambaye ataweza kuendana na kasi inayotakiwa, nataka shule hizi nikabidhiwe tarehe 25 Septemba, 2023” Ameelekeza Serukamba.

Katika hatua nyingine amewaonya Wakandarasi ambao watachezea fedha za Serikali kwa kutekeleza miradi chini ya kiwango na kusema kuwa Wakandarasi hao hawatavumiliwa wala kufumbiwa macho na badala yake hatua za kisheria zitachukuliwa dhidi yao.

Aidha Serukamba amesema Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk. Samia Suluhu Hassan amekuwa akitoa fedha nyingi kwa ajili ya maendeleo, hivyo hakuna atakaye kubali kuona fedha zinachezewa hivyo amesisitiza watendaji kuwa na nidhamu ya fedha na kutekeleza miradi ambayo itaonesha thamani ya fedha iliyotolewa kwa ajili ya maendeleo na si vinginevyo.

Wakati huo huo Wakuu wa Wilaya, Wakurugenzi wa halmashauri hizo pamoja na Wakandarasi wamesema kuwa watahakikisha miradi hiyo inakamilika kwa wakati na kukabidhiwa tarehe 25 Septemba 2023 kama Mkuu wa Mkoa wa Singida Peter Serukamba alivyoagiza.

Ziara ya Mkuu wa Mkoa wa Singida ya kukagua miradi ya Kuimarisha Elimu ya Sekondari (SEQUIP) itaendelea kesho tarehe 19 Septemba katika Wilaya ya Ikungi, Manyoni na halmashauri ya Wilaya Itigi wilayani Manyoni ikiwa ni kuhakiki miradi inayotekelezwa katika Mkoa huo inakamilika kwa wakati na kwa kiwango kinachotakiwa.

Matangazo

  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2022_2023 SINGIDA RS July 01, 2022
  • MAJINA YA WALIOCHANGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA - 2023, MKOA WA SINGIDA December 14, 2022
  • TAARIFA YA MAPOKEZI YA FEDHA KWA KIPINDI CHA KUANZIA JULAI HADI OCTOBA, 2023 KWA AJILI YA UTEKELEZAJI WA SHUGHULI ZA MAENDELEO November 01, 2023
  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2021/2022 SINGIDA RS - GPN 2021 - 2022 July 01, 2021
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • DKT.MGANGA ASISITIZA MADAKTARI BINGWA KUTOA HUDUMA BORA

    May 05, 2025
  • WATUMISHI NA WAAJIRI HODARI MKOANI SINGIDA WAPOKEA TUZO

    May 02, 2025
  • KUELEKEA MEIMOSI,RC DENDEGO ATANGAZA FURSA ZA UWEKEZAJI

    April 25, 2025
  • MADAKTARI BINGWA WA DKT.SAMIA WABISHA HODI SINGIDA

    April 23, 2025
  • Angalia Zote

Video

Mkoa wa Singida waja na Mikakati ya Kuboresha Elimu
Video zaidi

Viungio vya Haraka

  • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
  • Mwongozo wa Matumizi ya TEHAMA Serikalini
  • Fomu ya Maombi ya Kusafiri Nje ya Nchi
  • MPANGO WA MANUNUZI MKOA WA SINGIDA
  • KUONA AJIRA ZA WAALIMU WA SAYANSI NA MAFUNDI SANIFU

Tovuti Muhimu

  • UTUMISHI
  • TAMISEMI
  • IKULU
  • WIZARA YA ELIMU
  • NECTA
  • WIZARA YA AFYA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Ramani ya Mkoa

Wasiliana Nasi

    SINGIDA

    Anuani: P O BOX 5 SINGIDA

    Simu: 2502170, 2502089

    Simu: 2502170, 2502089

    Barua Pepe: info@singida.go.tz ras@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Usiri
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

Copyright ©2023 Singida Regional Commisioner' Office . All rights reserved.