• Wasiliana Nasi |
    • Malalamiko |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
    • Blog |
Singida Regional Website

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Tovuti ya Mkoa wa Singida

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na dhima
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Ikungi
      • HISTORIA
    • Iramba
    • Manyoni
    • Mkalama
    • Singida
  • Halmashauri
    • H/W Ikungi
    • H/W Iramba
    • H/W Itigi
    • H/W Manyoni
    • H/W Mkalama
    • H/W Singida
    • H/M Singida
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Viwanda na Biashara
    • Madini
  • Huduma Zetu
    • Afya
      • Madaktari Bingwa
      • Huduma za Tiba
      • Huduma za Kinga
      • Ustawi wa Jamii
      • Afya ya Mazingira
      • Lishe
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba Wa Huduma Kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
    • Investment Guide
  • Kituo Cha Habari
    • Picha
    • Video
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma

RC SINGIDA, NATAKA JUKWAA LA WANAWAKE LA MKOA WA SINGIDA KUWA IMARA KULIKO LOLOTE NCHINI KATIKA KUSAIDIA WANAWAKE KUONDOKANA NA UMASKINI.

Posted on: June 4th, 2024

Serikali ya mkoa wa Singida imewaagiza Maafisa Maendeleo wa Halmashauri Saba za mkoa huo kuhakikisha wanafanya tafiti mbalimbali ambazo zitasaidia wanawake wa mkoa huo ambao wanafikia Milioni Moja kuanzisha miradi ya kiuchumi itakayowasaidia kujikwamua na umaskini ikilinganishwa na hali ilivyo kwa sasa.

Mkuu wa mkoa wa Singida Halima Dendego ametoa kauli hiyo leo (4-Juni-2024) Mjini Singida wakati azindua Jukwaa la Uwezeshaji Wanawake la mkoa wa Singida kiuchumi.

Halima Dendego amesema jukwaa hilo linatakiwa kuwa na nguvu kuliko majukwaa yote nchini katika kuweka mipango na mikakati madhubuti ya kuwainua wanawake katika masuala mbalimbali ya kiuchumi na uongozi.

“Watoeini Wanawake kwenye mablanketi ya umaskini wasaidieni wainuke kwenye miradi ya kiuchumi wanayoifanya kwa sababu miradi yao mingi haileti matokeo chanya katika kubadilisha maisha ya wanawake, Amesisitiza Halima Dendego.

Amesema hatapenda kuona Jukwaa hiyo linakuwa legelege na kusisitiza kuwa wanawake wengi lazima wajiunge na jukwaa hilo lenye lengo kubwa la kuwasaidia wanawake kujiimarisha kiuchumi kwa sababu wapo wengi na uwezo wao.

Mkuu huyo wa mkoa wa Singida amesema ili kuona Majukwaa hayo ya wanawake yanafanya kazi bila kulala atakuwa anafanya tathimini ya utendaji kazi kila baada ya miezi Mitatu ili kujua maendeleo yao na kama kuna changamoto  zinazokwamisha maendeleo ya majukwaa hayo zitatuliwe haraka.

Halima Dendego pia amewahimiza Wanawake wa mkoa wa Singida kujitokeza kwa wingi bila woga katika kugombea nafasi mbalimbali katika uchaguzi wa Serikali za Mitaa utakaofanyika hivi karibuni kwa sababu uwezo wa kugombea na kushinda nafasi hizo wanazo kinachotakiwa kujiamini na kuthubutu.

Naye, Katibu Tawala wa mkoa wa Singida Dkt. Fatuma Mganga amewataka Maafisa Maendeleo ya jamii katika Halmashauri Saba za mkoa wa Singida wanakuwa bega kwa bega na wanawake katika kuwashauri na kuwapatia mbinu mbalimbali za kufanya biashara zenye tija ili kuondokana na umaskini wa kipato.

Dkt. Fatuma amesema biashara nyingi wanazofanya baadhi ya wanawake zinaonekana hazina tija hali ambayo inasababisha baadhi ya biashara zinazoanzishwa kufa kwa sababu hawana elimu ya ujasirimali na fedha ikiwemo namna ya kukopa kwenye Taasisi za Kifedha ambazo hazina riba kubwa.

Kwa upande wake, Katibu wa Jukwaa la Wanawake wa mkoa wa Singida akisoma taarifa ya maendeleo ya Jukwaa hilo ambalo kwa sasa linafanya kazi katika Halmashauri Tatu za Singida, Ikungi na Manispaa ya Singida kwa kuwezeshwa na Shirika la UN WOMEN ameomba Serikali kuendelea kuwasaidia wanawake katika elimu ya ujasiriamali, elimu ya fedha na uongozi ili waweze kufanya vizuri katika kujiinua kiuchumi katika biashara.

Nao, Wakuu wa Wilaya za Singida na Ikungi wamemwahidi Mkuu wa mkoa wa Singida kuwa watasimamia kikamilifu maagiza yake katika kuwasaidia wanawake wa Wilaya zao kuwa bora katika masuala ya kiuchumi ikilinganishwa na hali ilivyo sasa.

Mkuu wa Wilaya ya Singida Godwin Gondwe, akitoa neno la shukrani kwaniaba ya Mkuu wa Mkoa huo kwa wanachama wa Jukwaa la kuwezesha wanawake kiuchumi la mkoa wa Singida.

Matangazo

  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2022_2023 SINGIDA RS July 01, 2022
  • MAJINA YA WALIOCHANGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA - 2023, MKOA WA SINGIDA December 14, 2022
  • TAARIFA YA MAPOKEZI YA FEDHA KWA KIPINDI CHA KUANZIA JULAI HADI OCTOBA, 2023 KWA AJILI YA UTEKELEZAJI WA SHUGHULI ZA MAENDELEO November 01, 2023
  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2021/2022 SINGIDA RS - GPN 2021 - 2022 July 01, 2021
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • DKT.MGANGA ASISITIZA MADAKTARI BINGWA KUTOA HUDUMA BORA

    May 05, 2025
  • WATUMISHI NA WAAJIRI HODARI MKOANI SINGIDA WAPOKEA TUZO

    May 02, 2025
  • KUELEKEA MEIMOSI,RC DENDEGO ATANGAZA FURSA ZA UWEKEZAJI

    April 25, 2025
  • MADAKTARI BINGWA WA DKT.SAMIA WABISHA HODI SINGIDA

    April 23, 2025
  • Angalia Zote

Video

Mkoa wa Singida waja na Mikakati ya Kuboresha Elimu
Video zaidi

Viungio vya Haraka

  • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
  • Mwongozo wa Matumizi ya TEHAMA Serikalini
  • Fomu ya Maombi ya Kusafiri Nje ya Nchi
  • MPANGO WA MANUNUZI MKOA WA SINGIDA
  • KUONA AJIRA ZA WAALIMU WA SAYANSI NA MAFUNDI SANIFU

Tovuti Muhimu

  • UTUMISHI
  • TAMISEMI
  • IKULU
  • WIZARA YA ELIMU
  • NECTA
  • WIZARA YA AFYA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Ramani ya Mkoa

Wasiliana Nasi

    SINGIDA

    Anuani: P O BOX 5 SINGIDA

    Simu: 2502170, 2502089

    Simu: 2502170, 2502089

    Barua Pepe: info@singida.go.tz ras@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Usiri
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

Copyright ©2023 Singida Regional Commisioner' Office . All rights reserved.