• Wasiliana Nasi |
    • Malalamiko |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
    • Blog |
Singida Regional Website

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Tovuti ya Mkoa wa Singida

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na dhima
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Ikungi
      • HISTORIA
    • Iramba
    • Manyoni
    • Mkalama
    • Singida
  • Halmashauri
    • H/W Ikungi
    • H/W Iramba
    • H/W Itigi
    • H/W Manyoni
    • H/W Mkalama
    • H/W Singida
    • H/M Singida
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Viwanda na Biashara
    • Madini
  • Huduma Zetu
    • Afya
      • Madaktari Bingwa
      • Huduma za Tiba
      • Huduma za Kinga
      • Ustawi wa Jamii
      • Afya ya Mazingira
      • Lishe
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba Wa Huduma Kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
    • Investment Guide
  • Kituo Cha Habari
    • Picha
    • Video
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma

Serikali kuongeza nguvu matengenezo ya miradi ya TASAF Singida

Posted on: May 27th, 2022

Halmashauri za Mkoa wa Singida ambazo zinapata fedha za miradi ya TASAF zimetakiwa kuiendeleza miradi hiyo kwa kuzifanyia matengenezo na kuiongezea thamani ili iweze kuongeza mapato ya wanufaika na Serikali kwa ujumla.

Miradi hiyo ni kama malambo, Mabwawa na Barabara za kijamii.

Kauli hiyo imetolewa hivi karibuni na Mkuu wa Mkoa wa Singida Dkt. Binilith Mahenge alipotembelea Miradi inayotekelezwa kupitia Mfuko wa Maendeleo ya Jamii TASAF katika Wilaya ya Iramba mkoani hapo ambapo alitoa maagizo ya kuendelezwa kwa miradi hiyo kupitia Halmashauri husika ili iweze kuwa na manufaa zaidi kwa wanufaika.

Mkuu wa Mkoa wa Singida Dkt. Binilith Mahenge akizungumza na Wanufaika wa Miradi inayotekelezwa kupitia Mfuko wa Maendeleo ya Jamii TASAF katika Wilaya ya Iramba mkoani Singida Mei 26, 2022

Aidha akijibu maombi ya wananchi na wanufaika wa Mradi wa bwawa wilayani Iramba ambao waliomba Serikali kusaidia kuongeza kina na upana wa  bwawa hilo, RC Mahenge amemtaka Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Iramba isaidie matengenezo hayo huku akiwataka kununua vifaranga vya samaki vitakavyofugwa katika bwawa hilo ili liongeze kipato kwao na Serikali kwa ujumla.

Dk. Mahenge ameagiza Maafisa kilimo na mifugo kuhakikisha wanasimamia bwawa hilo ili liweze kuzalisha samaki na liweze kutumika katika Kilimo cha Umwagiliaji wa Mboga mboga na matunda katika eneo hilo.

Katika hatua nyinge RC Mahenge akikagua Ujenzi wa Barabara ya kijamii iliyojengwa na wananchi katika Kijiji cha Misigiri kilichopo kata ya Kiomboi akatumia muda huo kuwaagiza Wakala wa Barabara Vijijini na Mjini TARURA kuongeza kasi katika uwekaji wa madaraja madogo na makubwa katika barabara hiyo ili ziweze kupitika kwa nyakati zote.

Akimalizia ziara yake katika Kijiji cha new Kiomboi RC Mahenge amewataka wanufaika wa TASAF kutumia fedha wanazopata kwa malengo yaliopo ikiwa ni pamoja na kuanzisha miradi midogo midogo itakayosaidia kuendeleza maisha yao huku akiwataka Maafisa wa TASAF ngazi zote kuongeza juhudi za kuelimisha wananchi kuhusiana na mifumo mbalimbali ya mradi ili kupunguza malalamiko ya wananchi.

Katika taarifa yake DC wa Iramba Suleimani Mwenda amesema kwamba TASAF Wilayani hapo inatekelezwa katika vijiji 51 ikiwemo miradi ya uhaulishaji wa fedha, miradi ya muda mfupi kwa walengwa, kuweka akiba na kukuza uchumi wa Kaya kupitia vikundi pamoja na mradi wa Timiza malengo kwa wasichana balehe na wanawake vijana.

DC Suleimani amesema Halmashauri ya Iramba umepokea kiasi cha Sh. Bilioni 1.184 kwa ajili ya kuandaa Mpango wa manunuzi wa vifaa vya ajira za muda kwa walengwa na Mpango wa kunusuru Kaya maskini, malipo ya ruzuku ya uhaulishaji wa fedha kwa Kaya za walengwa na ruzuku ya ajira .

Aidha, DC huyo amebainisha kwamba  vijiji 45 vinatekeleza miradi ya uchimbaji wa malambo wakati vijiji vitano vikitekeleza miradi ya uchimbaji wa Barabara za  jamii na Kijiji kimoja kikitekeleza mradi wa Matenga Maji.

Awali akitoa taarifa  Mratibu wa TASAF Mkoa Patric Kasango amesema Mkoa umepokea jumla ya Tsh. Bilioni 10 kwa ajili ya miradi mbalimbali iliyopo katika Wilaya za Iramba Ikungi Mkalama Manyoni na Singida  ambapo Bilioni 6 kati ya fedha hizo zinatumika kama ruzuku katika masharti ya elimu na Afya.

Baadhi ya Wanufaika wa Miradi inayotekelezwa kupitia Mfuko wa Maendeleo ya Jamii TASAF waliojitokeza wakati wa ziara ya Mheshimiwa Mkuu wa Mkoa wa Singida Dkt. Binilith Mahenge Wilaya ya Iramba mkoani Singida

RC Mahenge akikagua moja ya Ujenzi wa Barabara ya kijamii iliyojengwa na wananchi katika Kijiji cha Misigiri kilichopo kata ya Kiomboi Wilaya ya Iramba mkoani Singida

Mkuu wa Wilaya ya Iramba Suleimani Mwenda (mwenye suti nyeusi) akisisiza jambo kwa watendaji juu ya usimamizi na utekelezaji wa miradi hiyo wilayani Iramba

Mwisho

Matangazo

  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2022_2023 SINGIDA RS July 01, 2022
  • MAJINA YA WALIOCHANGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA - 2023, MKOA WA SINGIDA December 14, 2022
  • TAARIFA YA MAPOKEZI YA FEDHA KWA KIPINDI CHA KUANZIA JULAI HADI OCTOBA, 2023 KWA AJILI YA UTEKELEZAJI WA SHUGHULI ZA MAENDELEO November 01, 2023
  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2021/2022 SINGIDA RS - GPN 2021 - 2022 July 01, 2021
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • IKUNGI YAPEPERUSHA BENDERA KWA MIRADI YA KIMKAKATI.

    May 08, 2025
  • DKT.MGANGA ASISITIZA MADAKTARI BINGWA KUTOA HUDUMA BORA

    May 05, 2025
  • WATUMISHI NA WAAJIRI HODARI MKOANI SINGIDA WAPOKEA TUZO

    May 02, 2025
  • KUELEKEA MEIMOSI,RC DENDEGO ATANGAZA FURSA ZA UWEKEZAJI

    April 25, 2025
  • Angalia Zote

Video

Mkoa wa Singida waja na Mikakati ya Kuboresha Elimu
Video zaidi

Viungio vya Haraka

  • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
  • Mwongozo wa Matumizi ya TEHAMA Serikalini
  • Fomu ya Maombi ya Kusafiri Nje ya Nchi
  • MPANGO WA MANUNUZI MKOA WA SINGIDA
  • KUONA AJIRA ZA WAALIMU WA SAYANSI NA MAFUNDI SANIFU

Tovuti Muhimu

  • UTUMISHI
  • TAMISEMI
  • IKULU
  • WIZARA YA ELIMU
  • NECTA
  • WIZARA YA AFYA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Ramani ya Mkoa

Wasiliana Nasi

    SINGIDA

    Anuani: P O BOX 5 SINGIDA

    Simu: 2502170, 2502089

    Simu: 2502170, 2502089

    Barua Pepe: info@singida.go.tz ras@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Usiri
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

Copyright ©2023 Singida Regional Commisioner' Office . All rights reserved.