• Wasiliana Nasi |
    • Malalamiko |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
    • Blog |
Singida Regional Website

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Tovuti ya Mkoa wa Singida

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na dhima
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Ikungi
      • HISTORIA
    • Iramba
    • Manyoni
    • Mkalama
    • Singida
  • Halmashauri
    • H/W Ikungi
    • H/W Iramba
    • H/W Itigi
    • H/W Manyoni
    • H/W Mkalama
    • H/W Singida
    • H/M Singida
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Viwanda na Biashara
    • Madini
  • Huduma Zetu
    • Afya
      • Madaktari Bingwa
      • Huduma za Tiba
      • Huduma za Kinga
      • Ustawi wa Jamii
      • Afya ya Mazingira
      • Lishe
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba Wa Huduma Kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
    • Investment Guide
  • Kituo Cha Habari
    • Picha
    • Video
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma

SERIKALI YA MKOA WA SINGIDA YAZINDUA SIKU MAALUM YA KUSHUGHULIKIA KERO ZA WANANCHI.

Posted on: June 6th, 2024

Mamia ya Wananchi wa Mkoa wa Singida wamemiminika katika Ofisi ya Mkuu wa mkoa huo kwa ajili ya kutoa kero mbalimbali zinazowakabili kwa muda mrefu ili ziweze kupatiwa ufumbuzi kufutia Mkuu wa mkoa wa Singida Mhe. Halima Dendego, kuzindua rasmi siku ya Alhamisi kuwa ni siku maalum ya kusikiliza na kushughulikia kero za wananchi wa mkoa huo na kuzitafutia ufumbuzi.

Akizindua Kliniki hiyo ya kushughulikia kero za wananchi leo (6-Juni-2024) zoezi ambalo linajumuisha Wakuu wa Mashirika na Taasisi zote za mkoa wa Singida, Mkuu huyo wa mkoa amesema zoezi hilo litafanyika katika Halmashauri zote Saba za mkoa wa Singida nia ni kuona wananchi wanaishi maisha ya furaha kwa kuwaondolewa kero zinazowakabili.

Halima Dendego, amesema Ofisi yake itakuwa inafanya zoezi hilo kwa mwezi mara Moja na watagawana na Katibu Tawala wa mkoa wa Singida Dkt. Fatuma Mganga, kwenda kwenye kila Halmashauri kwa ajili ya kusikiliza na kutatua kero za Wananchi kama Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan, alivyowaagiza.

“Tunapokaa hivi tukawasiliza na kutatua kero mbalimbali zinazowasumbua basi tutakuwa tumefanya jambo kubwa la kuwarejeshea wananchi furaha iliyopote kwa kuondoa kero zao zinazowasumbua kwa muda mrefu”, amesisitiza Halima Dendego.

Ameeleza kuwa katika maisha yetu ya kila siku mtu akiwa na manung’uniko, maumivu na malalamiko hata umpe zawadi yoyote nzuri hataifurahia lakini unapomtatulia kero inayomkabili basi unamrejeshea furaha yake.

Naye, Katibu Tawala wa mkoa wa Singida Dkta. Futuma Mganga amewahakikishia wananchi kuwa watakuwa bega kwa bega na Mkuu wa mkoa pamoja na Viongozi wengine wa Wilaya katika kuhakikisha kero za wananchi zinapatiwa majawabu haraka ili wananchi watumie muda wao kufanya kazi badala ya kila siku kuzunguka kwenye ofisi za umma kwa ajili ya kutafuta majawabu ya kero zinazowakabili.

Baadhi ya Wananchi wa mkoa wa Singida Elizabeth Machael, Hamisi Mneta na Hemed Mushihiri waliojitokeza kutoa kero zao wamempongeza Mkuu wa mkoa wa Singida Halima Dendego kwa kutenga siku maalum ya kusikiliza kero za wananchi na wamesema wanaimani kubwa kuwa kero walizotoa zitapatiwa majawabu kwa wakati na ya uhakika.


Matangazo

  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2022_2023 SINGIDA RS July 01, 2022
  • MAJINA YA WALIOCHANGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA - 2023, MKOA WA SINGIDA December 14, 2022
  • TAARIFA YA MAPOKEZI YA FEDHA KWA KIPINDI CHA KUANZIA JULAI HADI OCTOBA, 2023 KWA AJILI YA UTEKELEZAJI WA SHUGHULI ZA MAENDELEO November 01, 2023
  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2021/2022 SINGIDA RS - GPN 2021 - 2022 July 01, 2021
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • IKUNGI YAPEPERUSHA BENDERA KWA MIRADI YA KIMKAKATI.

    May 08, 2025
  • DKT.MGANGA ASISITIZA MADAKTARI BINGWA KUTOA HUDUMA BORA

    May 05, 2025
  • WATUMISHI NA WAAJIRI HODARI MKOANI SINGIDA WAPOKEA TUZO

    May 02, 2025
  • KUELEKEA MEIMOSI,RC DENDEGO ATANGAZA FURSA ZA UWEKEZAJI

    April 25, 2025
  • Angalia Zote

Video

Mkoa wa Singida waja na Mikakati ya Kuboresha Elimu
Video zaidi

Viungio vya Haraka

  • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
  • Mwongozo wa Matumizi ya TEHAMA Serikalini
  • Fomu ya Maombi ya Kusafiri Nje ya Nchi
  • MPANGO WA MANUNUZI MKOA WA SINGIDA
  • KUONA AJIRA ZA WAALIMU WA SAYANSI NA MAFUNDI SANIFU

Tovuti Muhimu

  • UTUMISHI
  • TAMISEMI
  • IKULU
  • WIZARA YA ELIMU
  • NECTA
  • WIZARA YA AFYA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Ramani ya Mkoa

Wasiliana Nasi

    SINGIDA

    Anuani: P O BOX 5 SINGIDA

    Simu: 2502170, 2502089

    Simu: 2502170, 2502089

    Barua Pepe: info@singida.go.tz ras@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Usiri
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

Copyright ©2023 Singida Regional Commisioner' Office . All rights reserved.