• Wasiliana Nasi |
    • Malalamiko |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
    • Blog |
Singida Regional Website

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Tovuti ya Mkoa wa Singida

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na dhima
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Ikungi
      • HISTORIA
    • Iramba
    • Manyoni
    • Mkalama
    • Singida
  • Halmashauri
    • H/W Ikungi
    • H/W Iramba
    • H/W Itigi
    • H/W Manyoni
    • H/W Mkalama
    • H/W Singida
    • H/M Singida
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Viwanda na Biashara
    • Madini
  • Huduma Zetu
    • Afya
      • Madaktari Bingwa
      • Huduma za Tiba
      • Huduma za Kinga
      • Ustawi wa Jamii
      • Afya ya Mazingira
      • Lishe
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba Wa Huduma Kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
    • Investment Guide
  • Kituo Cha Habari
    • Picha
    • Video
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma

SERIKALI YATUMIA ZAIDI YA SH. BILIONI 17.8 KUBORESHA MIUNDOMBINU ELIMU YA AWALI NA SHULE ZA MSINGI, SINGIDA

Posted on: September 5th, 2023

Mkoa wa Singida umepokea zaidi ya Sh. Bilioni 17.8, kutoka Serikali Kuu kwa mwaka wa fedha 2021/2022 na 2022/2023, kwa ajili ya ujenzi wa miundombinu mbalimbali ya elimu ya awali na shule za msingi ili kumwezesha mwanafunzi kupata elimu bora zaidi darasani.   

Hayo yamebainishwa leo na Mkuu wa Mkoa wa Singida, Peter Serukamba kwenye hotuba iliyosomwa kwa niaba yake na Mkuu wa Wilaya ya Mkalama, Moses Machali wakati wa uzinduzi rasmi wa Programu Jumuishi ya Malezi, Makuzi na Maendeleo ya awali ya mtoto (PJT-MMMAM-2021/22-2025/26), huku Serikali ikiyapongeza mashirika 19 kati ya 59 yaliyosajiliwa kwa kutekeleza moja kwa moja programu hiyo mkoani Singida.

Mashirika mengine 40 kati ya 59 ambayo makao makuu yake yapo mkoani Singida na mengine nje ya mkoa yanatekeleza kazi zake kupitia miradi mbalimbali ikiwemo afya, elimu, maji, ujenzi wa miundombinu, ulinzi na usalama, lishe na usafi wa mazingira.

Serukamba amefafanua kuwa, kati ya fedha hizo, Shilingi 6,925,704,502/24 zililetwa na Serikali kwa ajili ya ujenzi wa miundombinu ya elimu msingi kwa mwaka wa fedha 2021/2022 na kiasi kingine cha Shilingi 10,925,465,901/34, kimetumika kwa mwaka wa fedha 2022/2023.

Mkuu huyo wa mkoa alifafanua kuwa, ili kuhakikisha mtoto anakuwa kwenye utimilifu wake, Serikali ya awamu ya sita imewekeza katika kuboresha uhai wa mtoto kupitia utoaji wa huduma bure za afya kwa mama wajawazito na watoto chini ya miaka mitano.

Amefafanua kuwa, Serikali imewekeza katika elimu ya awali kwa kuwajengea uwezo walimu wa ufundishaji kutengeneza na kutumia zana malezi na makuzi kwa walimu 151 wa elimu ya awali, walimu wakuu 21 na maafisa elimu kata 21 kwa mwaka 2022/2023.

Awali akizindua Programu hiyo kwaniaba ya Mkuu wa Mkoa katika hafla iliyofanyika kwenye ukumbi wa mikutano Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, amesema kuwa, Programu hiyo ni kielelezo tosha cha Rais Samia Suluhu Hassan, katika kujali malezi, makuzi na maendeleo ya awali ya mtoto kwa ajili ya maendeleo ya Taifa.

Dkt. Fatuma Mganga akizungumza wakati wa uzinduzi huo.

“Mpango huu wa MMMAM umelenga kuwekeza mapema kwa mtoto kwa kuwa ukuaji unaanza wakati wa kutungwa mimba hadi miaka nane ambacho ni kipindi cha ukuaji zaidi. Programu hii imelenga kwenye maeneo makuu matano ambayo ni afya bora, lishe ya kutosha, malezi yenye mwitikio, ujifunzaji wa awali na ulinzi na usalama,”alifafanua

“Ni dhahiri kabisa, lishe bora katika jamii ni kichocheo cha maendeleo katika nyanja zote, ikiwemo afya, kilimo, elimu, biashara na uchumi…hivyo ni pale tu ambapo athari za lishe duni au utapiamlo zitakapodhibitiwa au kutokomezwa ndipo malengo ya maendeleo katika nyanja hizi yataweza kufikiwa kwa ufanisi,”alisema Serukamba.


Matangazo

  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2022_2023 SINGIDA RS July 01, 2022
  • MAJINA YA WALIOCHANGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA - 2023, MKOA WA SINGIDA December 14, 2022
  • TAARIFA YA MAPOKEZI YA FEDHA KWA KIPINDI CHA KUANZIA JULAI HADI OCTOBA, 2023 KWA AJILI YA UTEKELEZAJI WA SHUGHULI ZA MAENDELEO November 01, 2023
  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2021/2022 SINGIDA RS - GPN 2021 - 2022 July 01, 2021
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • HUDUMA ZA KIBINGWA ZAWAFIKIA WAGONJWA ZAIDI YA 3000 SINGIDA.

    May 09, 2025
  • IKUNGI YAPEPERUSHA BENDERA KWA MIRADI YA KIMKAKATI.

    May 08, 2025
  • DKT.MGANGA ASISITIZA MADAKTARI BINGWA KUTOA HUDUMA BORA

    May 05, 2025
  • WATUMISHI NA WAAJIRI HODARI MKOANI SINGIDA WAPOKEA TUZO

    May 02, 2025
  • Angalia Zote

Video

Mkoa wa Singida waja na Mikakati ya Kuboresha Elimu
Video zaidi

Viungio vya Haraka

  • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
  • Mwongozo wa Matumizi ya TEHAMA Serikalini
  • Fomu ya Maombi ya Kusafiri Nje ya Nchi
  • MPANGO WA MANUNUZI MKOA WA SINGIDA
  • KUONA AJIRA ZA WAALIMU WA SAYANSI NA MAFUNDI SANIFU

Tovuti Muhimu

  • UTUMISHI
  • TAMISEMI
  • IKULU
  • WIZARA YA ELIMU
  • NECTA
  • WIZARA YA AFYA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Ramani ya Mkoa

Wasiliana Nasi

    SINGIDA

    Anuani: P O BOX 5 SINGIDA

    Simu: 2502170, 2502089

    Simu: 2502170, 2502089

    Barua Pepe: info@singida.go.tz ras@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Usiri
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

Copyright ©2023 Singida Regional Commisioner' Office . All rights reserved.