• Wasiliana Nasi |
    • Malalamiko |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
    • Blog |
Singida Regional Website

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Tovuti ya Mkoa wa Singida

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na dhima
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Ikungi
      • HISTORIA
    • Iramba
    • Manyoni
    • Mkalama
    • Singida
  • Halmashauri
    • H/W Ikungi
    • H/W Iramba
    • H/W Itigi
    • H/W Manyoni
    • H/W Mkalama
    • H/W Singida
    • H/M Singida
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Viwanda na Biashara
    • Madini
  • Huduma Zetu
    • Afya
      • Madaktari Bingwa
      • Huduma za Tiba
      • Huduma za Kinga
      • Ustawi wa Jamii
      • Afya ya Mazingira
      • Lishe
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba Wa Huduma Kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
    • Investment Guide
  • Kituo Cha Habari
    • Picha
    • Video
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma

SERUKAMBA AAGIZA KUKAMILIKA KWA VYUMBA VYA MADARASA ILI YATUMIKE KWA WANAFUNZI IFIKAPO JANUARI 2024

Posted on: November 28th, 2023

Mkuu wa Mkoa wa Singida Peter Serukamba, amezitaka Halmashauri za Wilaya Mkoani Singida kukamilisha miradi ya maendeleo kwa wakati ikiwemo ya elimu ili wanafunzi wenye sifa ya elimu ya awali na msingi wapate nafasi na watakaofaulu waendelee na elimu ya Sekondari ifikapo Januari 2024.

Serukamba amesema hayo leo Novemba 28, 2023 alipoongea na Wazazi Walezi na Viongozi wa Halmashauri ya Wilaya ya Ikungi katika shule ya msingi Kintandaa muda mfupi baada ya kukagua miradi ya maendeleo kwenye kijiji cha Irisya, Msimii, Kipunda na Kintandaa ikiwa ni mwendelezo wa ziara ya kusikiliza na kutatua kero za wananchi katika kila kijiji Mkoani humo.

Mkuu huyo wa Mkoa alilazimika kutoa maelekezo hayo baada ya kujionea ujenzi wa vyumba vya madarasa ya shule ya msingi Kintandaa na ambayo yapo kwenye hatua mbalimbali za ujenzi wakati umebakia mwezi mmoja pekee wanafunzi waanze muhula mpya wa masomo kote nchini.

“Mkurugenzi, lijulishe baraza lako la Madiwani juu ya ujenzi wa vyumba vya madarasa…hakikisha mnakamilisha mapema kabla ya Disemba 31 mwaka huu, ili ifikapo mwezi wa kwanza mwakani, wanafunzi waweze kuyatumia katika masomo yao,”alisema Serukamba.

Aidha katika kituo cha afya Irisya, Serukamba, alimtaka Mwenyekiti wa Halmashauri hiyo, Alli Mwanga, kulielekeza Baraza la Madiwani liidhinishe fedha za kukamilisha miradi ya Zahanati na vituo vya afya ili wananchi waanze kunufaika na matunda ya Serikali yao ya awamu ya sita.

“Kwenye miradi hii yote, hakikisheni mnaisimamia vizuri na kuifuatilia mwanzo hadi mwisho, ili iweze kuendana na kasi, ubora, thamani ya fedha na kiwango kinachostahili, kwa lengo la kuleta tija kwa jamii yetu tunayoitumikia,” alisisitiza Serukamba.

Mapema katika mkutano huo Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Ikungi, Alli Mwanga, aliipogeza Serikali ya awamu ya sita inayoongozwa na Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan, kwa kuwaletea wananchi maendeleo kupitia miradi ya afya elimu maji na miundombinu ya barabara.

“Mheshimiwa Mkuu wa Mkoa, sisi wananchi wa Halmashauri ya Wilaya ya Ikungi, pamoja na mambo mengi ya maendeleo yanayoendelea hivi sasa, tunamshuru sana Rais wetu, Dkt. Samia Suluhu Hassan, kwa kutupatia fedha za kutosha kwa ajili ya miradi mbalimbali inayotekelezwa” alisema.

Mwenyekiti huyo, alitumia muda huo pia kuwaomba wananchi waendelee kumuunga mkono Rais, kutokana na kazi kubwa ya maendeleo anayoifanya lengo likiwa ni kwa ajili ya kuwajali Watanzania, na bila kuwabagua kwa misingi ya dini na kabila lake la asili.

Ziara hiyo ni mahususi kwa Mkuu huyo wa Mkoa, kutembelea vijiji vyote 441 vya Mkoa wa Singida, huku katika awamu ya kwanza akiwa amekamilisha kukutana na wananchi wa vijiji zaidi ya 61, kwa ajili ya kusikiliza na kutatua kero mbalimbali zinazoikabili jamii.

Matangazo

  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2022_2023 SINGIDA RS July 01, 2022
  • MAJINA YA WALIOCHANGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA - 2023, MKOA WA SINGIDA December 14, 2022
  • TAARIFA YA MAPOKEZI YA FEDHA KWA KIPINDI CHA KUANZIA JULAI HADI OCTOBA, 2023 KWA AJILI YA UTEKELEZAJI WA SHUGHULI ZA MAENDELEO November 01, 2023
  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2021/2022 SINGIDA RS - GPN 2021 - 2022 July 01, 2021
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • HUDUMA ZA KIBINGWA ZAWAFIKIA WAGONJWA ZAIDI YA 3000 SINGIDA.

    May 09, 2025
  • IKUNGI YAPEPERUSHA BENDERA KWA MIRADI YA KIMKAKATI.

    May 08, 2025
  • DKT.MGANGA ASISITIZA MADAKTARI BINGWA KUTOA HUDUMA BORA

    May 05, 2025
  • WATUMISHI NA WAAJIRI HODARI MKOANI SINGIDA WAPOKEA TUZO

    May 02, 2025
  • Angalia Zote

Video

Mkoa wa Singida waja na Mikakati ya Kuboresha Elimu
Video zaidi

Viungio vya Haraka

  • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
  • Mwongozo wa Matumizi ya TEHAMA Serikalini
  • Fomu ya Maombi ya Kusafiri Nje ya Nchi
  • MPANGO WA MANUNUZI MKOA WA SINGIDA
  • KUONA AJIRA ZA WAALIMU WA SAYANSI NA MAFUNDI SANIFU

Tovuti Muhimu

  • UTUMISHI
  • TAMISEMI
  • IKULU
  • WIZARA YA ELIMU
  • NECTA
  • WIZARA YA AFYA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Ramani ya Mkoa

Wasiliana Nasi

    SINGIDA

    Anuani: P O BOX 5 SINGIDA

    Simu: 2502170, 2502089

    Simu: 2502170, 2502089

    Barua Pepe: info@singida.go.tz ras@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Usiri
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

Copyright ©2023 Singida Regional Commisioner' Office . All rights reserved.