• Wasiliana Nasi |
    • Malalamiko |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
    • Blog |
Singida Regional Website

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Tovuti ya Mkoa wa Singida

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na dhima
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Ikungi
      • HISTORIA
    • Iramba
    • Manyoni
    • Mkalama
    • Singida
  • Halmashauri
    • H/W Ikungi
    • H/W Iramba
    • H/W Itigi
    • H/W Manyoni
    • H/W Mkalama
    • H/W Singida
    • H/M Singida
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Viwanda na Biashara
    • Madini
  • Huduma Zetu
    • Afya
      • Madaktari Bingwa
      • Huduma za Tiba
      • Huduma za Kinga
      • Ustawi wa Jamii
      • Afya ya Mazingira
      • Lishe
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba Wa Huduma Kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
    • Investment Guide
  • Kituo Cha Habari
    • Picha
    • Video
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma

"SINGIDA TUMEZIKATAA CHANGAMOTO ZA WANAWAKE"RC DENDEGO

Posted on: October 16th, 2024

Mkuu wa Mkoa wa Singida Mhe Halima Dendego amewaomba wanawake kujiandikisha katika daftari la wapiga kura kwa ajili ya kushiriki  uchaguzi wa serikali za mitaa unaotarajiwa kufanyika Novemba 27, 2024 na kugombea nafasi za uongozi ili wanawake kuwa na nafasi  ya kutoa maamuzi pale yanapojadiliwa maswala mbalimbali ya maendeleo.

Hayo yamesemwa hii leo tarehe 16 Octoba, 2024 katika maadhimisho ya kimataifa ya mwanamke wa kijijini yalioanzishwa kwa mara ya kwanza na baraza kuu la umoja wa mataifa mwaka 2007 kupitia azimio maalumu la kutambua jukumu na mchango wa wanawake wa Vijijini katika kuimarisha maendeleo ya Kilimo maendeleo ya vijiji kuboresha usalama wa chakula na kutokomeza umasikini ambayo yamefanyika ukumbi wa shule ya sekondari Ikungi.

Mkuu wa Mkoa amesema kuwa nafasi hizi za uongozi zimewekwa ili wanawake wapaze sauti katika yale ambayo yamekuwa ni kero na yanakwamisha maendeleo ya wanawake kiuchumi na nyanja zingine zote.

"Singida hususani Wilaya ya Ikungi tumeshaanza kuzikataa changamoto za wanawake tunasema tutakapolima tupewe nafasi ya maamuzi kipi kiuzwe na kipi kibaki kwa ajili ya chakula" amesema mkuu wa Mkoa

Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya ya Ikungi Mhe Thomas Apson ameongeza na kusema kuwa ipo haja pia wanawake kuwaheshimu waume zao ili kuondokana na migogoro ya mara kwa mara inayojitokeza na kupeleke mifarakano katika familia.

"Nimejifunza hilo kwenye mikutano yangu ya kusikiliza kero za wananchi inapofika saa 12 wanawake wanawahi nyumbani kuwapikia waume zao huu ni Utamaduni mzuri tusiige tamaduni mbaya" ameongeza Mkuu wa Wilaya.

Kaimu Mkurugenzi Mtendaji Halmashauri ya Wilaya ya Ikungi Ndg. Richard Rwehumbiza akisoma taarifa mbele ya Mgeni Rasmi kuwa maadhimisho haya hufanyika kila mwaka ili kuelimisha jamii kuhusu jitihada mbali mbali zinazofanyika na serikali na asasi mbalimbali kukuza uchumi na mshikamano wa wanawake nchini na duniani kote.

Naye Afisa Maendeleo ya jamii Bi Haika Massawe mara baada ya maada mbalimbali kujadiliwa juu ya mwanamke wa kijijini ametaja baadhi ya maazimio ambayo kwa kushirikiana na wanawake wa Wilaya ya Ikungi yatatekelezwa kubwa ikiwa ni pamoja na utoaji kwa wakati mikopo ya asilimia 10 za halmashauri na kufatilia utendaji wao wa kazi ili kurejesha mikopo hiyo kwa wakati na mengine ikiwa ni pamoja na kuweka mazingira wezeshi kutatua changamoto zao kama kugombea nafasi za uongozi na kujumuika katika kutoa maamuzi.

Matangazo

  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2022_2023 SINGIDA RS July 01, 2022
  • MAJINA YA WALIOCHANGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA - 2023, MKOA WA SINGIDA December 14, 2022
  • TAARIFA YA MAPOKEZI YA FEDHA KWA KIPINDI CHA KUANZIA JULAI HADI OCTOBA, 2023 KWA AJILI YA UTEKELEZAJI WA SHUGHULI ZA MAENDELEO November 01, 2023
  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2021/2022 SINGIDA RS - GPN 2021 - 2022 July 01, 2021
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • IKUNGI YAPEPERUSHA BENDERA KWA MIRADI YA KIMKAKATI.

    May 08, 2025
  • DKT.MGANGA ASISITIZA MADAKTARI BINGWA KUTOA HUDUMA BORA

    May 05, 2025
  • WATUMISHI NA WAAJIRI HODARI MKOANI SINGIDA WAPOKEA TUZO

    May 02, 2025
  • KUELEKEA MEIMOSI,RC DENDEGO ATANGAZA FURSA ZA UWEKEZAJI

    April 25, 2025
  • Angalia Zote

Video

Mkoa wa Singida waja na Mikakati ya Kuboresha Elimu
Video zaidi

Viungio vya Haraka

  • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
  • Mwongozo wa Matumizi ya TEHAMA Serikalini
  • Fomu ya Maombi ya Kusafiri Nje ya Nchi
  • MPANGO WA MANUNUZI MKOA WA SINGIDA
  • KUONA AJIRA ZA WAALIMU WA SAYANSI NA MAFUNDI SANIFU

Tovuti Muhimu

  • UTUMISHI
  • TAMISEMI
  • IKULU
  • WIZARA YA ELIMU
  • NECTA
  • WIZARA YA AFYA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Ramani ya Mkoa

Wasiliana Nasi

    SINGIDA

    Anuani: P O BOX 5 SINGIDA

    Simu: 2502170, 2502089

    Simu: 2502170, 2502089

    Barua Pepe: info@singida.go.tz ras@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Usiri
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

Copyright ©2023 Singida Regional Commisioner' Office . All rights reserved.