• Wasiliana Nasi |
    • Malalamiko |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
    • Blog |
Singida Regional Website

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Tovuti ya Mkoa wa Singida

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na dhima
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Ikungi
      • HISTORIA
    • Iramba
    • Manyoni
    • Mkalama
    • Singida
  • Halmashauri
    • H/W Ikungi
    • H/W Iramba
    • H/W Itigi
    • H/W Manyoni
    • H/W Mkalama
    • H/W Singida
    • H/M Singida
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Viwanda na Biashara
    • Madini
  • Huduma Zetu
    • Afya
      • Madaktari Bingwa
      • Huduma za Tiba
      • Huduma za Kinga
      • Ustawi wa Jamii
      • Afya ya Mazingira
      • Lishe
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba Wa Huduma Kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
    • Investment Guide
  • Kituo Cha Habari
    • Picha
    • Video
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma

MABINGWA WA CECAFA WAKARIBISHWA NYUMBANI BAADA YA USHINDI MNONO

Posted on: October 5th, 2025

Mkuu wa Mkoa wa Singida, Mhe. Halima Dendego, ameongoza maelfu ya wananchi wa mkoa huo katika mapokezi ya kihistoria ya timu ya Singida Black Stars baada ya kutwaa ubingwa wa mashindano ya CECAFA 2025, yaliyofanyika hivi karibuni.

Mapokezi hayo yamefanyika leo katika Uwanja wa Bombadia, Mjini Singida, na kuvutia maelfu ya mashabiki wa soka kutoka maeneo mbalimbali ya mkoa huo. Furaha, nderemo na vifijo vilitawala uwanjani huku mashabiki wakiwa wamepambwa kwa jezi, bendera na mabango yenye maneno ya pongezi kwa mabingwa hao wapya wa Afrika Mashariki na Kati.

Akizungumza katika hafla hiyo, Mhe. Dendego aliwapongeza wachezaji, benchi la ufundi na uongozi mzima wa Singida Black Stars kwa ushindi huo mkubwa, akisema umeiweka Singida kwenye ramani ya michezo kitaifa na kimataifa.

"Hakika timu yetu ya Singida Black Stars imebeba na kulitangaza vema jina la Mkoa. Mmetupa heshima kubwa kitaifa na kimataifa. Huu ni ushahidi kwamba Singida ni kituo kipya cha vipaji na ubora katika michezo,” alisema Mhe.Dendego kwa furaha.

Mkuu  wa mkoa alisema kombe la CECAFA lina heshima kubwa katika ukanda wa Afrika Mashariki na Kati, na ushindi huo ni ishara ya mwanzo wa enzi mpya ya mafanikio kwa timu hiyo.

“Hizi ni salamu kwa wengine kwamba Singida Black Stars tuna jambo letu. Safari hii ya makombe ndiyo inaanza, hatuishii hapa,” alisisitiza.

Aidha, Mhe. Dendego alimpongeza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, kwa juhudi zake za kuendeleza sekta ya michezo nchini, hususan kupitia ujenzi wa miundombinu na kuimarisha timu za taifa na klabu.

 “Kupitia uongozi wake, tumeshuhudia miradi mikubwa ya michezo ikikamilika na hamasa kubwa kwa wachezaji wetu kushinda kimataifa – hili ndilo tunaliita Goli la Mama,” alisema Mhe. Dendego.

Akizungumzia maendeleo ya miundombinu ya michezo mkoani Singida, Dendegu alisema ujenzi wa uwanja wa mpira wa Airtel ulioko Mtipa upo katika hatua za mwisho, na mechi ya kwanza inatarajiwa kuchezwa mwezi Novemba mwaka huu.

Aidha, aliwahimiza wakazi wa Singida kuchangamkia fursa za kiuchumi zitakazotokana na uwepo wa uwanja huo, hasa katika biashara ndogo ndogo, huduma za malazi, usafiri na utalii.

 “Nitoe rai kwa wawekezaji wa hoteli, wafanyabiashara na watoa huduma mbalimbali kuendelea kujipanga vema ili kunufaika na fursa hii. Uwanja huu ni baraka kwa uchumi wa Singida,” alisisitiza.

Katika hatua nyingine, Mkuu huyo wa Mkoa alitumia nafasi hiyo kuwakumbusha wananchi kujitokeza kwa wingi kupiga kura katika uchaguzi mkuu unaotarajiwa kufanyika Oktoba 29 mwaka huu, akisema ni wajibu wa kila Mtanzania kuchangia ustawi wa taifa kupitia sanduku la kura.

Sherehe hizo zilihitimishwa kwa burudani kutoka kwa wasanii wa ndani, maonyesho na gwaride maalum la wachezaji wa Singida Black Stars lililopamba moto uwanjani.

Ushindi huo wa CECAFA umeifanya Singida Black Stars kuandika historia mpya katika michezo ya Tanzania, na kuwa timu ya kwanza kutoka Singida kutwaa ubingwa wa kimataifa tangu kuanzishwa kwake.



Matangazo

  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2022_2023 SINGIDA RS July 01, 2022
  • MAJINA YA WALIOCHANGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA - 2023, MKOA WA SINGIDA December 14, 2022
  • TAARIFA YA MAPOKEZI YA FEDHA KWA KIPINDI CHA KUANZIA JULAI HADI OCTOBA, 2023 KWA AJILI YA UTEKELEZAJI WA SHUGHULI ZA MAENDELEO November 01, 2023
  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2021/2022 SINGIDA RS - GPN 2021 - 2022 July 01, 2021
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • MABINGWA WA CECAFA WAKARIBISHWA NYUMBANI BAADA YA USHINDI MNONO

    October 05, 2025
  • MADAKTARI BINGWA WAWASILI SINGIDA KUTOA HUDUMA BORA KWA WANANCHI

    October 06, 2025
  • HALI YA HEWA YA MKOA WA SINGIDA YATAKIWA KUTUMIWA KAMA FURSA NA SIO KIKWAZO

    September 25, 2025
  • MRADI WA MABWAWA YA KUTIBU MAJITAKA KUKAMILIKA OKTOBA,WANANCHI KUNUFAIKA

    September 23, 2025
  • Angalia Zote

Video

Mkoa wa Singida waja na Mikakati ya Kuboresha Elimu
Video zaidi

Viungio vya Haraka

  • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
  • Mwongozo wa Matumizi ya TEHAMA Serikalini
  • Fomu ya Maombi ya Kusafiri Nje ya Nchi
  • MPANGO WA MANUNUZI MKOA WA SINGIDA
  • KUONA AJIRA ZA WAALIMU WA SAYANSI NA MAFUNDI SANIFU

Tovuti Muhimu

  • UTUMISHI
  • TAMISEMI
  • IKULU
  • WIZARA YA ELIMU
  • NECTA
  • WIZARA YA AFYA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Ramani ya Mkoa

Wasiliana Nasi

    SINGIDA

    Anuani: P O BOX 5 SINGIDA

    Simu: 2502170, 2502089

    Simu: 2502170, 2502089

    Barua Pepe: info@singida.go.tz ras@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Usiri
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

Copyright ©2023 Singida Regional Commisioner' Office . All rights reserved.