• Wasiliana Nasi |
    • Malalamiko |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
    • Blog |
Singida Regional Website

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Tovuti ya Mkoa wa Singida

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na dhima
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Ikungi
      • HISTORIA
    • Iramba
    • Manyoni
    • Mkalama
    • Singida
  • Halmashauri
    • H/W Ikungi
    • H/W Iramba
    • H/W Itigi
    • H/W Manyoni
    • H/W Mkalama
    • H/W Singida
    • H/M Singida
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Viwanda na Biashara
    • Madini
  • Huduma Zetu
    • Afya
      • Madaktari Bingwa
      • Huduma za Tiba
      • Huduma za Kinga
      • Ustawi wa Jamii
      • Afya ya Mazingira
      • Lishe
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba Wa Huduma Kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
    • Investment Guide
  • Kituo Cha Habari
    • Picha
    • Video
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma

SINGIDA YAMUENZI MWALIMU NYERERE KWA KUSIMAMIA UBORA WA ELIMU.

Posted on: October 14th, 2017

  Mkuu wa Mkoa wa Singida Dkt Rehema Nchimbi leo amekagua miradi ya uboreshaji wa mazingira ya kujifunzia na Kufundishia katika shule nne za Msingi na sekondari, kama sehemu ya kumbukumbu ya Hayati baba wa Taifa la Tanzania Mwalimu Julius Kambarage Nyerere. 

Katika ziara yake Dkt Nchimbi ametumia muda mwingi kuwafundisha uzalendo kwa taifa, wanafunzi wa shule za Sekondari Ilongero na Mtinko pamoja na shule za Msingi Mtinko na Mwakichenche zote za Halmashauri ya Wilaya ya Singida.

Dkt Nchimbi amesema, wanafunzi hao watamuenzi mwalimu Nyerere na kudumisha uzalendo endapo watasoma kwa bidii ili taifa lipate wataalamu wa kutosha katika Nyanja mbalimbali watakaoweza kusaidia kukuza uchumi wa Tanzania.

“Mchango wa baba wa Taifa Mwalimu Nyerere kwa taifa letu ni mkubwa sana kwakuwa licha ya kutupatia uhuru pia ametukomboa katika umasikini, ujinga na maradhi, hivyo basi nawaasa muipende sana elimu ili na nyinyi muweze kuwa sehemu ya kulisaidia taifa”, ameeleza Dkt Nchimbi.

Ameongeza kuwa katika kuboresha elimu serikali ya awamu ya tano imetoa zaidi ya shilingi bilioni 1 Mkoani Singida kwa ajili ya ujenzi wa miundombinu ya kidato cha tano na sita pamoja na kujenga miundombinu ya wanafunzi wenye mahitaji maalumu kwa kipindi cha mwaka 2017/2018.

“Tunapomkumbuka Mwalimu Nyerere leo tuthamini mchango wa serikali yetu unaofanya kwa ajili ya kuboresha sekta mbalimbali, mfano katika sekta ya elimu shilingi 1,052, 200,000 zilizotolewa nimethibitisha zimefanya kazi nzuri, kazi kwenu walimu kufundisha kwa bidii na wanafunzi kukazana katika kusoma kwakuwa mazingira yameboreshwa sana”, amesisitiza Dkt Nchimbi.

Aidha Dkt Nchimbi amewapongeza wakuu wa shule na kamati za shule hizo kwa kuchagua mafundi wazawa ambao wametumia gharama nafuu na kujenga miradi hiyo kwa kiwango kizuri, huku akisisitiza wananchi wasijicheleweshee maendeleo kwa kungoja wataalamu kutoka nje ya nchi wakati mtanzania anaweza kufanya jambo hilo kwa ubora ule ule.

Naye Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Singida Rashidi Mandoa amesema serikali kuu kupitia program ya lipa kutokana na matokeo imetoa fedha hizo kwa ajili ya shule tatu za Sekondari na mbili za Msingi ili kuinua ubora wa elimu Wilayani hapo.

Mandoa amesema kupitia miradi hiyo inayotekelezwa katika sekondari za Mtinko, Ilongero na Mwanamwema Shein pamoja na shule za Msingi za Mtinko na Mwakichenche, wananchi wameongeza imani na matumaini makubwa kwa serikali yao.

Kwa Upande wake Kiongozi wa Wanafunzi wa Sekondari ya Ilongero Daudi William Kihanga amesema nafasi waliyonayo katika kumuenzi baba wa Taifa ni kusoma kwa bidii kwakuwa wana imani kuwa kila mwalimu anapenda mwanafunzi asome kwa bidii vivyo hivyo wakisoma kwa bidii watakuwa wanamuenzi baba wa Taifa.

Kihanga ameishukuru serikali kwa kuboresha miundombinu ya kujifunzia kwakuwa inawapa wanafunzi hamasa ya kusoma kwa bidii bila kikwazo chochote.

Matangazo

  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2022_2023 SINGIDA RS July 01, 2022
  • MAJINA YA WALIOCHANGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA - 2023, MKOA WA SINGIDA December 14, 2022
  • TAARIFA YA MAPOKEZI YA FEDHA KWA KIPINDI CHA KUANZIA JULAI HADI OCTOBA, 2023 KWA AJILI YA UTEKELEZAJI WA SHUGHULI ZA MAENDELEO November 01, 2023
  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2021/2022 SINGIDA RS - GPN 2021 - 2022 July 01, 2021
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • DKT.MGANGA ASISITIZA MADAKTARI BINGWA KUTOA HUDUMA BORA

    May 05, 2025
  • WATUMISHI NA WAAJIRI HODARI MKOANI SINGIDA WAPOKEA TUZO

    May 02, 2025
  • KUELEKEA MEIMOSI,RC DENDEGO ATANGAZA FURSA ZA UWEKEZAJI

    April 25, 2025
  • MADAKTARI BINGWA WA DKT.SAMIA WABISHA HODI SINGIDA

    April 23, 2025
  • Angalia Zote

Video

Mkoa wa Singida waja na Mikakati ya Kuboresha Elimu
Video zaidi

Viungio vya Haraka

  • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
  • Mwongozo wa Matumizi ya TEHAMA Serikalini
  • Fomu ya Maombi ya Kusafiri Nje ya Nchi
  • MPANGO WA MANUNUZI MKOA WA SINGIDA
  • KUONA AJIRA ZA WAALIMU WA SAYANSI NA MAFUNDI SANIFU

Tovuti Muhimu

  • UTUMISHI
  • TAMISEMI
  • IKULU
  • WIZARA YA ELIMU
  • NECTA
  • WIZARA YA AFYA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Ramani ya Mkoa

Wasiliana Nasi

    SINGIDA

    Anuani: P O BOX 5 SINGIDA

    Simu: 2502170, 2502089

    Simu: 2502170, 2502089

    Barua Pepe: info@singida.go.tz ras@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Usiri
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

Copyright ©2023 Singida Regional Commisioner' Office . All rights reserved.