• Wasiliana Nasi |
    • Malalamiko |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
    • Blog |
Singida Regional Website

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Tovuti ya Mkoa wa Singida

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na dhima
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Ikungi
      • HISTORIA
    • Iramba
    • Manyoni
    • Mkalama
    • Singida
  • Halmashauri
    • H/W Ikungi
    • H/W Iramba
    • H/W Itigi
    • H/W Manyoni
    • H/W Mkalama
    • H/W Singida
    • H/M Singida
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Viwanda na Biashara
    • Madini
  • Huduma Zetu
    • Afya
      • Madaktari Bingwa
      • Huduma za Tiba
      • Huduma za Kinga
      • Ustawi wa Jamii
      • Afya ya Mazingira
      • Lishe
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba Wa Huduma Kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
    • Investment Guide
  • Kituo Cha Habari
    • Picha
    • Video
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma

Tutapima udongo kabla ya kusambaza mbegu za alizeti RC Mahenge

Posted on: June 28th, 2022

Serikali imejipanga kupima na kutambua  Hali ya udogo kabla ya kusambaza mbegu za alizeti kwa wakulima wa Mkoa wa Singida ili kuondoa  changamoto iliyojitokeza katika msimu huu wa kilimo ambapo kwa bàadhi ya maeneo hazikuweza kutoa mazao yaliyokusudiwa.

Lengo la kupima udongo wa maeneo hayo ni kutambua aina ya mazao au mbegu zinazoweza kustawi  kwa kuwa imebainika  kwamba bàadhi ya mbegu za alizeti zimekuwa zikistawi zaidi katika bàadhi ya maeneo huku maeneo mengine  zikishindwa kustawi vizuri.

Akiongea wakati wa Mkutano wa hadhara uliofanyika katika Kijiji cha Kitukutu kata ya Kiomboi wilaya ya Iramba alipokuwa akisikiliza na kutatua Kero za Wananchi Mkuu wa Mkoa wa Singida Dkt. Binilith Mahenge amebainisha kwamba Serikali inaendelea na mpango wa kupima ardhi ili kubaini aina ya mazao yanayoweza kustawi pamoja na aina ya mbolea itakayopendekezwa kutumika maeneo husika.

 Pamoja na changamoto ilijitokeza kwa wakulima wa alizeti katika bàadhi ya maeneo ambapo mbegu aina ya  standard kushindwa kustawi vizuri RC Mahenge akawaeleza wananchi kwamba  Serikali iligawa mbegu za alizeti kwa wananchi zenye thamani ya Tsh. Bilion tatu lengo likiwa ni kuondoa umaskini kwa wananchi kwa kupitia kilimo lakini mbegu hazikuweza kustawi vizuri kama malengo yalivyokuwa.

Amesema Serikali inampango wa kupima udongo katika maeneo mbalimbali Mkoani hapo ili  kubaini aina ya udongo na aina ya mbegu zinazotakiwa kustawishwa ili kuondokana na changamoto ya kupanda mbegu ambazo hazitaweza kutoa mafanikio.

Akijibu swali la mwanakijiji Elizabeth Shalua ambapo alitaka kujua mpango wa Serikali kuhusu mbegu hizo za alizeti ambazo ulikuwa ni mkopo kutoka Wizara ya Kilimo ambao waliotakiwa kurejesha wakati wa mavuno  na kwa bahati mbaya wameshindwa kuvuna kutokana na mbegu hiyo kutoa Mashuke kidogo RC Mahenge akabainisha kwamba kwa sasa Serikali haitadai kwa kuwa wananchi tayari wameingia hasara.

Naye Emanueli Mitundu kutoka Kijiji cha Misigiri akatumia nafasi hiyo kuiomba Serikali kupunguza bei ya pembejeo ikiwemo mbolea ambayo imekuwa juu kiasi cha wakulima kushindwa kununua hivyo kuchangia kupata mazao hafifu.

Ziara hiyo ya Mkuu wa Mkoa imeendelea katika Kijiji cha Misigiri ambapo aliendelea kutatua Kero za Wananchi kuhusu upatikanaji wa maji, Umeme na Barabara huku akiwataka wananchi kutoa ushirikiano kwa Serikali katika kutatua Kero zinazowakabili.

Aidha ziara hiyo ya kusikiliza na kutatua Kero za Wananchi itaendelea katika Wilaya ya Mkalama katika Kijiji cha Iguguno katika Mkutano wa hadhara utakofanyika uwanja wa Ofisi ya Kijiji cha Iguguno kuanzia saa tano asubuhi.

Mwisho

Matangazo

  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2022_2023 SINGIDA RS July 01, 2022
  • MAJINA YA WALIOCHANGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA - 2023, MKOA WA SINGIDA December 14, 2022
  • TAARIFA YA MAPOKEZI YA FEDHA KWA KIPINDI CHA KUANZIA JULAI HADI OCTOBA, 2023 KWA AJILI YA UTEKELEZAJI WA SHUGHULI ZA MAENDELEO November 01, 2023
  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2021/2022 SINGIDA RS - GPN 2021 - 2022 July 01, 2021
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • DKT.MGANGA ASISITIZA MADAKTARI BINGWA KUTOA HUDUMA BORA

    May 05, 2025
  • WATUMISHI NA WAAJIRI HODARI MKOANI SINGIDA WAPOKEA TUZO

    May 02, 2025
  • KUELEKEA MEIMOSI,RC DENDEGO ATANGAZA FURSA ZA UWEKEZAJI

    April 25, 2025
  • MADAKTARI BINGWA WA DKT.SAMIA WABISHA HODI SINGIDA

    April 23, 2025
  • Angalia Zote

Video

Mkoa wa Singida waja na Mikakati ya Kuboresha Elimu
Video zaidi

Viungio vya Haraka

  • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
  • Mwongozo wa Matumizi ya TEHAMA Serikalini
  • Fomu ya Maombi ya Kusafiri Nje ya Nchi
  • MPANGO WA MANUNUZI MKOA WA SINGIDA
  • KUONA AJIRA ZA WAALIMU WA SAYANSI NA MAFUNDI SANIFU

Tovuti Muhimu

  • UTUMISHI
  • TAMISEMI
  • IKULU
  • WIZARA YA ELIMU
  • NECTA
  • WIZARA YA AFYA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Ramani ya Mkoa

Wasiliana Nasi

    SINGIDA

    Anuani: P O BOX 5 SINGIDA

    Simu: 2502170, 2502089

    Simu: 2502170, 2502089

    Barua Pepe: info@singida.go.tz ras@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Usiri
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

Copyright ©2023 Singida Regional Commisioner' Office . All rights reserved.