• Wasiliana Nasi |
    • Malalamiko |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
    • Blog |
Singida Regional Website

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Tovuti ya Mkoa wa Singida

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na dhima
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Ikungi
      • HISTORIA
    • Iramba
    • Manyoni
    • Mkalama
    • Singida
  • Halmashauri
    • H/W Ikungi
    • H/W Iramba
    • H/W Itigi
    • H/W Manyoni
    • H/W Mkalama
    • H/W Singida
    • H/M Singida
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Viwanda na Biashara
    • Madini
  • Huduma Zetu
    • Afya
      • Madaktari Bingwa
      • Huduma za Tiba
      • Huduma za Kinga
      • Ustawi wa Jamii
      • Afya ya Mazingira
      • Lishe
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba Wa Huduma Kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
    • Investment Guide
  • Kituo Cha Habari
    • Picha
    • Video
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma

VIJANA WAASWA KUTUMIA VYUO VYA UFUNDI STADI KUWAWEZESHA KUJIAJIRI

Posted on: February 26th, 2025

Wazazi wametakiwa kutumia fursa zilizopo katika Vyuo vya Ufundi Stadi (VETA) ili kuwajengea vijana wao uwezo wa kupata elimu ya ufundi inayowawezesha kujiajiri ambavyo Serikali, kupitia Wizara ya Elimu imeendelea kuongeza bajeti kwa vyuo hivyo, ikiwemo VETA, ili kuhakikisha vijana wanapata ujuzi wa vitendo utakaowasaidia kujitegemea.

                       Kauli hiyo imetolewa na Mkuu wa Wilaya ya Singida, Mhe. Godwin Gondwe, Februari 25,wakati wa uzinduzi wa maonesho ya Chuo cha Ufundi VETA Kanda ya Kati, kuelekea maadhimisho ya miaka 30 ya Mamlaka ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi (VETA) tangu kuanzishwa mwaka 1994.

Katika hotuba yake, Mhe. Gondwe ametoa wito kwa Mamlaka ya VETA Kanda ya Kati kushirikiana na viwanda mbalimbali katika Wilaya ya Singida ili kuwaongezea wanachuo ujuzi wa vitendo.

          Kwa upande wake, Mbunge wa Jimbo la Singida na Makamu Mwenyekiti wa Kamati ya Elimu, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Mhe. Musa Sima, amesema kuwa mpango wa kuwatambua na kuwasimamia vijana walioko mtaani wenye ujuzi wa ufundi binafsi na kuwapatia vyeti rasmi ni hatua muhimu kwa maendeleo yao.

Aidha, amesema kubwa Serikali imewataka wahitimu wa elimu ya juu kujiunga na VETA ili kujipatia ujuzi wa vitendo utakaowawezesha kujiajiri badala ya kutegemea ajira za ofisini pekee.

Akizungumzia kodi ya ukuzaji ujuzi (SDL) inayotozwa kwa waajiri kwa asilimia 6, Mhe. Sima amesisitiza kuwa ni muhimu kuhakikisha fedha hizo zinatumika kuboresha elimu na miundombinu ya VETA nchini.

Naye Mkurugenzi wa VETA Kanda ya Kati, Ramadhani Makata, amewahimiza wazazi na vijana kujitokeza kwa wingi kujiunga na vyuo vya VETA kwa lengo la kupata ujuzi utakaowawezesha kujiajiri na kuinua uchumi wao.

                "VETA ndiyo mkombozi wa taifa hili. Vijana wanapaswa kuitumia fursa hii kujiandaa kwa maisha bora kupitia elimu ya ufundi stadi," alisisitiza Makata 

Maadhimisho hayo yamefanyika katika viwanja vya Bombadia, Mjini Singida.


Matangazo

  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2022_2023 SINGIDA RS July 01, 2022
  • MAJINA YA WALIOCHANGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA - 2023, MKOA WA SINGIDA December 14, 2022
  • TAARIFA YA MAPOKEZI YA FEDHA KWA KIPINDI CHA KUANZIA JULAI HADI OCTOBA, 2023 KWA AJILI YA UTEKELEZAJI WA SHUGHULI ZA MAENDELEO November 01, 2023
  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2021/2022 SINGIDA RS - GPN 2021 - 2022 July 01, 2021
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • IKUNGI YAPEPERUSHA BENDERA KWA MIRADI YA KIMKAKATI.

    May 08, 2025
  • DKT.MGANGA ASISITIZA MADAKTARI BINGWA KUTOA HUDUMA BORA

    May 05, 2025
  • WATUMISHI NA WAAJIRI HODARI MKOANI SINGIDA WAPOKEA TUZO

    May 02, 2025
  • KUELEKEA MEIMOSI,RC DENDEGO ATANGAZA FURSA ZA UWEKEZAJI

    April 25, 2025
  • Angalia Zote

Video

Mkoa wa Singida waja na Mikakati ya Kuboresha Elimu
Video zaidi

Viungio vya Haraka

  • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
  • Mwongozo wa Matumizi ya TEHAMA Serikalini
  • Fomu ya Maombi ya Kusafiri Nje ya Nchi
  • MPANGO WA MANUNUZI MKOA WA SINGIDA
  • KUONA AJIRA ZA WAALIMU WA SAYANSI NA MAFUNDI SANIFU

Tovuti Muhimu

  • UTUMISHI
  • TAMISEMI
  • IKULU
  • WIZARA YA ELIMU
  • NECTA
  • WIZARA YA AFYA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Ramani ya Mkoa

Wasiliana Nasi

    SINGIDA

    Anuani: P O BOX 5 SINGIDA

    Simu: 2502170, 2502089

    Simu: 2502170, 2502089

    Barua Pepe: info@singida.go.tz ras@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Usiri
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

Copyright ©2023 Singida Regional Commisioner' Office . All rights reserved.