• Wasiliana Nasi |
    • Malalamiko |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
    • Blog |
Singida Regional Website

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Tovuti ya Mkoa wa Singida

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na dhima
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Ikungi
      • HISTORIA
    • Iramba
    • Manyoni
    • Mkalama
    • Singida
  • Halmashauri
    • H/W Ikungi
    • H/W Iramba
    • H/W Itigi
    • H/W Manyoni
    • H/W Mkalama
    • H/W Singida
    • H/M Singida
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Viwanda na Biashara
    • Madini
  • Huduma Zetu
    • Afya
      • Madaktari Bingwa
      • Huduma za Tiba
      • Huduma za Kinga
      • Ustawi wa Jamii
      • Afya ya Mazingira
      • Lishe
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba Wa Huduma Kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
    • Investment Guide
  • Kituo Cha Habari
    • Picha
    • Video
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma

HUDUMA ZA KIBINGWA ZAWAFIKIA WAGONJWA ZAIDI YA 3000 SINGIDA.

Posted on: May 9th, 2025

Timu ya Madaktari bingwa wa Mama Samia ambayo leo imeagwa rasmi Mkoani Singida,imefanikiwa kuwafikia na kuwahudumia wagonjwa  3,242 kupitia kambi ya kliniki tembezi iliyofanyika kwa siku tano katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Singida, Mandewa.

Katibu Tawala wa Mkoa wa Singida, Dkt. Fatuma Mganga, ameongoza hafla ya kufunga rasmi kambi hiyo leo Mei 9,2025 akisema kuwa amefurahishwa na mafanikio ya kambi hiyo aliyoitaja kuwa ni ya kupongezwa kwa tija kubwa iliyoonekana kwa wananchi waliopata huduma.

"Kwa maana hiyo basi, mimi sina budi kumshukuru Mungu kwa ajili yenu, na kwa kila mmoja aliyechangia katika zoezi hili.Tumewagusa wananchi, tumewagusa wana Singida, na Watanzania wenzetu ambao walitaabika kwa muda mrefu kwa kukosa huduma, lakini kupitia ninyi mmeweza kurudisha faraja na afya katika maisha yao."amesema Daktari Mganga

Pia Dkt. Mganga  amewapongeza madaktari wa Mkoa wa Singida kwa kutumia rasilimali zilizopo kuongeza pato la hospitali na huduma kwa wananchi.

Kwa upande wake, Kaimu Mganga Mkuu wa Mkoa wa Singida, Dkt.Shilla Mwashiuya, ametoa pongezi kwa madaktari bingwa kwa kazi nzuri tangu walipoanza kambi tarehe 5 Mei akisema kuwa mirejesho kutoka kwa wagonjwa mbali mbali waliopata huduma hizo ni mizuri sana kwani wamefurahibkuoata huduma bora na karibu kabisa na makazi yao hapa Mkoani Singida.

 " Wagonjwa waliopata huduma wameridhika na matibabu na kauli nzuri kutoka kwa madaktari. Kupona si dawa tu, bali hata kauli njema inachangia mgonjwa kupata faraja," amesema Dkt.Shilla

Mwenyekiti wa Madaktari Bingwa wa Dr. Samia, Dkt. Amani Malima, amtoa taarifa ya utekelezaji wa kazi hiyo amesema kuwa waliwahudumia wagonjwa 3,242 dhidi ya lengo la 3,000, na kufanikisha upasuaji kwa wagonjwa 82 bila mgonjwa yeyote kuhitaji rufaa.

 "Wagonjwa wetu wote tuliowafanyia upasuaji wametoka salama, na hakuna aliyelazimika kupelekwa hospitali nyingine. Hii ni dalili kwamba tumepunguza gharama kwa wananchi na tumevuka malengo yetu," alisema Dkt. Malima.

Aliendelea kusema kuwa kambi hiyo ni ya tatu kwa awamu ya kwanza Kanda ya Kati, baada ya Morogoro na Iringa, na kwamba wataelekea Dodoma na Njombe kwa awamu zinazofuata. Ameushukuru uongozi wa Mkoa wa Singida kwa mapokezi mazuri na ushirikiano uliowezesha zoezi hilo kufanyika kwa mafanikio.

Wananchi nao wameeleza kwa furaha  kuridhishwa na  huduma walizopata kutoka kwa madaktari bingwa waliowahudumia kwa upendo na juhudi kubwa.

"Madaktari wa Samia wanatoa huduma nzuri sana na wako vizuri. Nimefurahi sana kwa huduma zao na tunaomba awamu nyingine waje kututembelea tena."Mimi nimepata uponyaji mkubwa kwa sababu mwanangu amefanyiwa upasuaji hapa. Nawaomba madaktari hawa waendelee hivyo hivyo na wapande ngazi kwa kazi nzuri wanayoifanya."amesema Amina Mwanga

Kwa mafanikio haya, Mkoa wa Singida umejizatiti kuendelea kushirikiana na timu ya madaktari bingwa ili kuhakikisha huduma bora zinaendelea kuwafikia wananchi wengi zaidi katika awamu zijazo.

Matangazo

  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2022_2023 SINGIDA RS July 01, 2022
  • MAJINA YA WALIOCHANGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA - 2023, MKOA WA SINGIDA December 14, 2022
  • TAARIFA YA MAPOKEZI YA FEDHA KWA KIPINDI CHA KUANZIA JULAI HADI OCTOBA, 2023 KWA AJILI YA UTEKELEZAJI WA SHUGHULI ZA MAENDELEO November 01, 2023
  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2021/2022 SINGIDA RS - GPN 2021 - 2022 July 01, 2021
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • HUDUMA ZA KIBINGWA ZAWAFIKIA WAGONJWA ZAIDI YA 3000 SINGIDA.

    May 09, 2025
  • IKUNGI YAPEPERUSHA BENDERA KWA MIRADI YA KIMKAKATI.

    May 08, 2025
  • DKT.MGANGA ASISITIZA MADAKTARI BINGWA KUTOA HUDUMA BORA

    May 05, 2025
  • WATUMISHI NA WAAJIRI HODARI MKOANI SINGIDA WAPOKEA TUZO

    May 02, 2025
  • Angalia Zote

Video

Mkoa wa Singida waja na Mikakati ya Kuboresha Elimu
Video zaidi

Viungio vya Haraka

  • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
  • Mwongozo wa Matumizi ya TEHAMA Serikalini
  • Fomu ya Maombi ya Kusafiri Nje ya Nchi
  • MPANGO WA MANUNUZI MKOA WA SINGIDA
  • KUONA AJIRA ZA WAALIMU WA SAYANSI NA MAFUNDI SANIFU

Tovuti Muhimu

  • UTUMISHI
  • TAMISEMI
  • IKULU
  • WIZARA YA ELIMU
  • NECTA
  • WIZARA YA AFYA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Ramani ya Mkoa

Wasiliana Nasi

    SINGIDA

    Anuani: P O BOX 5 SINGIDA

    Simu: 2502170, 2502089

    Simu: 2502170, 2502089

    Barua Pepe: info@singida.go.tz ras@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Usiri
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

Copyright ©2023 Singida Regional Commisioner' Office . All rights reserved.