• Wasiliana Nasi |
    • Malalamiko |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
    • Blog |
Singida Regional Website

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Tovuti ya Mkoa wa Singida

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na dhima
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Ikungi
      • HISTORIA
    • Iramba
    • Manyoni
    • Mkalama
    • Singida
  • Halmashauri
    • H/W Ikungi
    • H/W Iramba
    • H/W Itigi
    • H/W Manyoni
    • H/W Mkalama
    • H/W Singida
    • H/M Singida
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Viwanda na Biashara
    • Madini
  • Huduma Zetu
    • Afya
      • Madaktari Bingwa
      • Huduma za Tiba
      • Huduma za Kinga
      • Ustawi wa Jamii
      • Afya ya Mazingira
      • Lishe
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba Wa Huduma Kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
    • Investment Guide
  • Kituo Cha Habari
    • Picha
    • Video
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma

*WAJASIRIAMALI WADOGO WADOGO KUNUFAIKA NA VITAMBULISHO VYA KIDIJITALI.

Posted on: December 5th, 2024

Mkuu wa Wilaya ya Singida Godwin Gondwe leo Disemba 05,2024 amemuwakilisha Mkuu wa Mkoa wa Singida Halima Dendego katika uzinduzi wa zoezi la ugawaji wa vitambulisho vya kidijitali kwa wajasiriamali wadogo wadogo mkoani Singida ambao umefanyika katika Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Singida.

Uzinduzi huo umehudhuriwa  na viongozi na wawakilishi mbalimbali akiwemo Katibu Tawala Msaidizi sehemu ya viwanda na biashara, Maafisa maendeleo ya jamii kutoka ngazi za Mkoa na  halmashauri ambao ni waratibu wa dawati la wafanyabiashara ndogo ndogo,Viongozi wa Wafanyabiashara ndogo ndogo(wajasiriamali) na wawakilishi kadhaa wa wafanyabiashara ndogo ndogo.

Akizungumza wakati wa hafla hiyo Mkuu wa Wilaya  amesema ni wakati sasa wa wajasiriamali kwenda kunufaika na fursa mbali mbali kutokana na kupata vitambulisho hivyo huku akitoa agizo Kwa waratibu wa zoezi hilo wilaya zote  kuongeza kasi ya kuandikisha wajasiriamali hao ili wengi waweze kunufaika.

“Shughuli ya uzinduzi na ugawaji wa vitambulisho vya kidigitali kwa ajili ya Wafanyabiashara ndogondogo katika Mkoa wa Singida umetokana na changamoto ya muda mrefu ya kutaka kuwatambua wafanyabiashara ndogondogo nchini kwa idadi yao na umuhimu wa kuweka utaratibu mzuri wa kuwaratibu ili waweze kukua katika shughuli zao za kiuchumi na kijamii Kwa lengo la  kuwainua wafanyabiashara hao kiuchumi na kijamii pamoja na utayari wa kuhakikisha kuwa changamoto zao zinapatiwa ufumbuzi na wataalam kwa wakati”. Amesema DC Gondwe.

Awali,Katibu Tawala Msaidizi sehemu ya viwanda na biashara,Bi.Donatila Vedasto ameainisha makundi ya Wafanyabiashara ndogondogo,

"Wafanyabiashara ndogondogo nchini tunazingatia biashara zote halali zinazofanywa na wafanyabiashara hao ambazo zinatambuliwa na Mamlaka. Aidha, wafanyabiashara ndogondogo wanajumuisha machinga, mama na baba lishe, madereva wa bodaboda na bajaji, wasusi, vinyozi, wakulima wa bustani ndogondogo na wauzaji wa vyakula kama vile matunda na mbogamboga. Kwa ujumla sekta hii inachangia kwa kiwango kikubwa kutoa ajira kwa vijana wanaohitimu katika ngazi mbalimbali za elimu na taaluma hapa nchini”. Alisema Bi.Donatila

Wema Yona mfanyabiashara ambaye amepata kitambulisho siku ya Leo,amesema anategemea kupata fursa nyingi zaidi kupitia vitambulisho hivyo vya wafanyabiashara ndogo ndogo ikiwemo fursa za kupata mikopo ambazo walikua hawazipati ,akisema kuwa sasa watafanya kazi kwa kujiamini zaidi huku akitoa wito kwa wajasiriamali wote kupata vitambulisho hivyo ili kuwa karibu na fursa.

Pia,ameomba ushirikiano wa kutosha kutoka kwa viongozi uendelee ili kuweza kuzitatua changamoto zitakazojitokeza kwa lengo la kukuza uchumi wa wajasiriamali mmoja mmoja na Singida kwa ujumla kwa kuongeza mapato kutokana na kulipa kodi.

Mpaka sasa takribani wajasiriamali  894 wameshasajiliwa na kupata vitambulisho hivyo Mkoani Singida.



Matangazo

  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2022_2023 SINGIDA RS July 01, 2022
  • MAJINA YA WALIOCHANGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA - 2023, MKOA WA SINGIDA December 14, 2022
  • TAARIFA YA MAPOKEZI YA FEDHA KWA KIPINDI CHA KUANZIA JULAI HADI OCTOBA, 2023 KWA AJILI YA UTEKELEZAJI WA SHUGHULI ZA MAENDELEO November 01, 2023
  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2021/2022 SINGIDA RS - GPN 2021 - 2022 July 01, 2021
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • HUDUMA ZA KIBINGWA ZAWAFIKIA WAGONJWA ZAIDI YA 3000 SINGIDA.

    May 09, 2025
  • IKUNGI YAPEPERUSHA BENDERA KWA MIRADI YA KIMKAKATI.

    May 08, 2025
  • DKT.MGANGA ASISITIZA MADAKTARI BINGWA KUTOA HUDUMA BORA

    May 05, 2025
  • WATUMISHI NA WAAJIRI HODARI MKOANI SINGIDA WAPOKEA TUZO

    May 02, 2025
  • Angalia Zote

Video

Mkoa wa Singida waja na Mikakati ya Kuboresha Elimu
Video zaidi

Viungio vya Haraka

  • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
  • Mwongozo wa Matumizi ya TEHAMA Serikalini
  • Fomu ya Maombi ya Kusafiri Nje ya Nchi
  • MPANGO WA MANUNUZI MKOA WA SINGIDA
  • KUONA AJIRA ZA WAALIMU WA SAYANSI NA MAFUNDI SANIFU

Tovuti Muhimu

  • UTUMISHI
  • TAMISEMI
  • IKULU
  • WIZARA YA ELIMU
  • NECTA
  • WIZARA YA AFYA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Ramani ya Mkoa

Wasiliana Nasi

    SINGIDA

    Anuani: P O BOX 5 SINGIDA

    Simu: 2502170, 2502089

    Simu: 2502170, 2502089

    Barua Pepe: info@singida.go.tz ras@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Usiri
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

Copyright ©2023 Singida Regional Commisioner' Office . All rights reserved.