• Wasiliana Nasi |
    • Malalamiko |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
    • Blog |
Singida Regional Website

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Tovuti ya Mkoa wa Singida

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na dhima
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Ikungi
      • HISTORIA
    • Iramba
    • Manyoni
    • Mkalama
    • Singida
  • Halmashauri
    • H/W Ikungi
    • H/W Iramba
    • H/W Itigi
    • H/W Manyoni
    • H/W Mkalama
    • H/W Singida
    • H/M Singida
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Viwanda na Biashara
    • Madini
  • Huduma Zetu
    • Afya
      • Madaktari Bingwa
      • Huduma za Tiba
      • Huduma za Kinga
      • Ustawi wa Jamii
      • Afya ya Mazingira
      • Lishe
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba Wa Huduma Kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
    • Investment Guide
  • Kituo Cha Habari
    • Picha
    • Video
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma

*WAKULIMA NA WAFANYABIASHARA SINGIDA, WAHIMIZWA KUTUMIA MFUMO WA STAKABADHI ZA GHALA KWA TIJA*

Posted on: September 6th, 2024

Serikali ya Mkoa wa Singida imewataka wakulima na wafanyabiashara kuendelea kutumia mfumo wa stakabadhi za ghala kwa tija kubwa ili kuwaepusha na walanguzi wa mazao ya biashara na kuimarisha biashara yao.

Akizungumza na Waandishi wa habari, tarehe (6 Septemba, 2024), Mkuu wa Mkoa wa Singida, Mheshimiwa Halima Dendego, amesema kuwa mfumo huu umeanza kutekelezwa rasmi katika msimu wa 2024/2025 mkoani humo.

Aidha ameeleza kuwa utekelezaji wa mfumo huo unafuatia maagizo yaliyotolewa na serikali kupitia mwongozo wa biashara ya mazao kama dengu, mbaazi, na ufuta, ambao umetolewa chini ya usimamizi wa Mamlaka ya Udhibiti wa Nafaka na Mazao Mchanganyiko (COPRA), Tume ya Ushirika, Bodi ya Usimamizi wa Stakabadhi za Ghala na Soko la Bidhaa kupitia toleo la tatu la mwaka 2024.

Mkuu wa Mkoa pia alibainisha kuwa mwongozo huu mpya unalenga kudhibiti biashara ya mazao na kuwahakikishia wakulima na wafanyabiashara masoko ya uhakika ndani na nje ya nchi. Kupitia mfumo huu, wakulima watapata bei nzuri kwa mazao yao ikilinganishwa na miaka iliyopita, na hivyo kuongeza mapato yao.

Amefafanua kuwa, bei ya zao la dengu ambayo ilikuwa inauzwa kati ya TZS 900 hadi 1300 kwa kilo katika msimu wa 2023/2024, sasa inauzwa kati ya TZS 1,670 hadi 2,060 kwa kilo katika msimu wa 2024/2025 kupitia mfumo wa stakabadhi za ghala.

Faida nyingine za mfumo huu ni pamoja na ongezeko la mapato kwa halmashauri, udhibiti wa utoroshaji wa mazao, na kutoa uhakika wa takwimu kwa serikali. Mfumo huu pia umewezesha upatikanaji rahisi wa mikopo kwa wakulima na kuongeza masoko ya uhakika ya ndani na nje ya nchi.

Hata hivyo, amesema, ubora wa mazao umeimarika kwa kiasi kikubwa kutokana na mfumo huu ambao unazingatia taratibu na viwango bora vya usafirishaji na uhifadhi wa mazao, pia mfumo wa stakabadhi za ghala umeleta mapinduzi makubwa katika biashara ya mazao mkoani Singida.

Serikali ya Mkoa wa Singida inaendelea kushirikiana na wadau wote muhimu ili kuhakikisha mfumo huu unatekelezwa kikamilifu na kuleta matokeo chanya kwa wakulima na wafanyabiashara. Hii ni hatua muhimu katika kukuza uchumi wa mkoa na taifa kwa ujumla kupitia sekta ya kilimo, ambayo inabaki kuwa uti wa mgongo wa uchumi wa Tanzania.

Matangazo

  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2022_2023 SINGIDA RS July 01, 2022
  • MAJINA YA WALIOCHANGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA - 2023, MKOA WA SINGIDA December 14, 2022
  • TAARIFA YA MAPOKEZI YA FEDHA KWA KIPINDI CHA KUANZIA JULAI HADI OCTOBA, 2023 KWA AJILI YA UTEKELEZAJI WA SHUGHULI ZA MAENDELEO November 01, 2023
  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2021/2022 SINGIDA RS - GPN 2021 - 2022 July 01, 2021
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • IKUNGI YAPEPERUSHA BENDERA KWA MIRADI YA KIMKAKATI.

    May 08, 2025
  • DKT.MGANGA ASISITIZA MADAKTARI BINGWA KUTOA HUDUMA BORA

    May 05, 2025
  • WATUMISHI NA WAAJIRI HODARI MKOANI SINGIDA WAPOKEA TUZO

    May 02, 2025
  • KUELEKEA MEIMOSI,RC DENDEGO ATANGAZA FURSA ZA UWEKEZAJI

    April 25, 2025
  • Angalia Zote

Video

Mkoa wa Singida waja na Mikakati ya Kuboresha Elimu
Video zaidi

Viungio vya Haraka

  • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
  • Mwongozo wa Matumizi ya TEHAMA Serikalini
  • Fomu ya Maombi ya Kusafiri Nje ya Nchi
  • MPANGO WA MANUNUZI MKOA WA SINGIDA
  • KUONA AJIRA ZA WAALIMU WA SAYANSI NA MAFUNDI SANIFU

Tovuti Muhimu

  • UTUMISHI
  • TAMISEMI
  • IKULU
  • WIZARA YA ELIMU
  • NECTA
  • WIZARA YA AFYA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Ramani ya Mkoa

Wasiliana Nasi

    SINGIDA

    Anuani: P O BOX 5 SINGIDA

    Simu: 2502170, 2502089

    Simu: 2502170, 2502089

    Barua Pepe: info@singida.go.tz ras@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Usiri
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

Copyright ©2023 Singida Regional Commisioner' Office . All rights reserved.