• Wasiliana Nasi |
    • Malalamiko |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
    • Blog |
Singida Regional Website

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Tovuti ya Mkoa wa Singida

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na dhima
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Ikungi
      • HISTORIA
    • Iramba
    • Manyoni
    • Mkalama
    • Singida
  • Halmashauri
    • H/W Ikungi
    • H/W Iramba
    • H/W Itigi
    • H/W Manyoni
    • H/W Mkalama
    • H/W Singida
    • H/M Singida
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Viwanda na Biashara
    • Madini
  • Huduma Zetu
    • Afya
      • Madaktari Bingwa
      • Huduma za Tiba
      • Huduma za Kinga
      • Ustawi wa Jamii
      • Afya ya Mazingira
      • Lishe
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba Wa Huduma Kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
    • Investment Guide
  • Kituo Cha Habari
    • Picha
    • Video
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma

Waliomkataa Mwenyekiti wa Kijiji wakutana na Serukamba

Posted on: November 2nd, 2022

Wananchi wa Kijiji cha Choda Kata ya Mkiwa Wilayani Ikungi Mkoa wa Singida hivi karibuni wameeleza nia yao ya kumkataa Mwenyekiti wa Kijiji hicho kwa tuhuma mbalimbali zikiwemo za kutofanya mikutano ya kuzungumzia maendeleo ya Kijiji chao.

Maelezo hayo wameyatoa mbele ya Mkuu wa Mkoa huo Peter Serukamba wakimuomba kuingilia kati mgogoro huo wa uongozi ambao umekuwa wa muda mrefu.

Akiwa katika mkutano huo wa hadhara wananchi hao walieleza kutoridhishwa na uongozi wa kijiiji kwa kuwa hauitishi mikutano na kutowasomea wananchi mapato na matumizi ya Kijiji chao.

Kutokana na malalamiko hayo RC Serukamba alihoji Halmashauri ya Kijiji hicho kuhusiana na tuhuma hizo ambapo Mwenyekiti wa Kijiji hicho alieleza kwamba wapo wananchi ambao kutokana na itikadi zao hawajitokezi kwenye mikutano inapoitishwa hivyo kukosa uelewa wa kutosha kuhusiana na mapato na matumizi ya Kijiji hicho.

Aidha baadhi ya wananchi walipoulizwa kama waliowahi kuhudhuria mikutano iliyoishwa na Halmashauri hiyo pamoja na viongozi mbalimbali wa vijiji walieleza kwamba hawakuhudhuria.

Akizungumza na viongozi hao Rc Serukamba amesema kwa mujibu wa maelezo aliyoyapata kutoka kwa viongozi wa Halmashauri ya Kijiji, pamoja na viongozi wa CCM wa tawi na Kata amebaini tuhuma zinazotolewa dhidi ya Mwenyekiti wa Kijiji hicho hazina mashiko ya kumuondoa katika nafasi yake.

Awali Mkuu wa Wilaya ya Ikungi Mhe. Jerry Muro akitoa taarifa ya jinsi walivyoshughulikia mgogoro huo amesema walilazimika kufanya vikao vitatu vya kutatua changamoto hiyo ambapo katika kikao cha mwisho mwezi October Dc. Muro aliwataka kufuata utaratibu endapo wanaona tuhuma za kumtoa Mwenyekiti wa Kijiji zina ukweli jambo ambalo baadhi ya viongozi hawakufanya hivyo.

RC Serukamba mbali na kupongeza jitihada za awali za Wilaya katika kutatua mgogoro huo amewataka wajumbe wa Halmashauri ya Kijiji na viongozi wa CCM tawi kufanya kazi na Mwenyekiti huyo na kumpa ushirikiano ili atekeleze majukumu yake ipasavyo na kuwaonya baadhi ya wajumbe kuacha kuweka maslahi yao binafsi.

Matangazo

  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2022_2023 SINGIDA RS July 01, 2022
  • MAJINA YA WALIOCHANGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA - 2023, MKOA WA SINGIDA December 14, 2022
  • TAARIFA YA MAPOKEZI YA FEDHA KWA KIPINDI CHA KUANZIA JULAI HADI OCTOBA, 2023 KWA AJILI YA UTEKELEZAJI WA SHUGHULI ZA MAENDELEO November 01, 2023
  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2021/2022 SINGIDA RS - GPN 2021 - 2022 July 01, 2021
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • IKUNGI YAPEPERUSHA BENDERA KWA MIRADI YA KIMKAKATI.

    May 08, 2025
  • DKT.MGANGA ASISITIZA MADAKTARI BINGWA KUTOA HUDUMA BORA

    May 05, 2025
  • WATUMISHI NA WAAJIRI HODARI MKOANI SINGIDA WAPOKEA TUZO

    May 02, 2025
  • KUELEKEA MEIMOSI,RC DENDEGO ATANGAZA FURSA ZA UWEKEZAJI

    April 25, 2025
  • Angalia Zote

Video

Mkoa wa Singida waja na Mikakati ya Kuboresha Elimu
Video zaidi

Viungio vya Haraka

  • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
  • Mwongozo wa Matumizi ya TEHAMA Serikalini
  • Fomu ya Maombi ya Kusafiri Nje ya Nchi
  • MPANGO WA MANUNUZI MKOA WA SINGIDA
  • KUONA AJIRA ZA WAALIMU WA SAYANSI NA MAFUNDI SANIFU

Tovuti Muhimu

  • UTUMISHI
  • TAMISEMI
  • IKULU
  • WIZARA YA ELIMU
  • NECTA
  • WIZARA YA AFYA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Ramani ya Mkoa

Wasiliana Nasi

    SINGIDA

    Anuani: P O BOX 5 SINGIDA

    Simu: 2502170, 2502089

    Simu: 2502170, 2502089

    Barua Pepe: info@singida.go.tz ras@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Usiri
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

Copyright ©2023 Singida Regional Commisioner' Office . All rights reserved.