• Wasiliana Nasi |
    • Malalamiko |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
    • Blog |
Singida Regional Website

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Tovuti ya Mkoa wa Singida

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na dhima
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Ikungi
      • HISTORIA
    • Iramba
    • Manyoni
    • Mkalama
    • Singida
  • Halmashauri
    • H/W Ikungi
    • H/W Iramba
    • H/W Itigi
    • H/W Manyoni
    • H/W Mkalama
    • H/W Singida
    • H/M Singida
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Viwanda na Biashara
    • Madini
  • Huduma Zetu
    • Afya
      • Madaktari Bingwa
      • Huduma za Tiba
      • Huduma za Kinga
      • Ustawi wa Jamii
      • Afya ya Mazingira
      • Lishe
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba Wa Huduma Kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
    • Investment Guide
  • Kituo Cha Habari
    • Picha
    • Video
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma

WANAWAKE 3,000 KUSHIRIKI TAMASHA LA SERIKALI ZA MITAA SINGIDA

Posted on: October 7th, 2024

Mkoa wa Singida umeandaa tamasha kubwa litakalo washirikisha wanawake zaidi ya 3,000 kutoka wilaya zote za mkoa huu lililobeba jina la Wanawake na Uchaguzi wa Serikali za Mitaa.

Mkuu wa Mkoa wa Singida, Halima Dendego, akizungumza leo (Oktoba 7, 2024) na waandishi wa habari, amesema tamasha hilo litafanyika Oktoba 10, mwaka huu kwenye viwanja vya Bombadia vilivyopo Manispaa ya Singida.

Amesema Spika wa Bunge mstaafu ambaye pia ni Kamisaa wa Sensa nchini, Anne Makinda, atakuwa mgeni rasmi katika tamasha hilo ambalo lengo lake ni kuwahamashisha wanawake  kushiriki katika uchahuzi wa serikali za mitaa unaotarajia kufanyika Novemba 27, 2024.

"Serikali yetu bora na sikivu chini ya uongozi wa Rais Dk.Samia Suluhu Hassan, imeweka taratibu mbalimbali za kuhakikisha kuwa kila mwananchi anapata taarifa sahihi za uchaguzi na anahamasishwa ili aweze kushiriki katika uchaguzi na hivyo kutimiza haki yao ya kikatiba, hivyo tamasha hili ni moja ya mipango ya mkoa katika kuwafikia wananchi wengi hasa makundi maalum ya wanawake,vijana na watu wenye ulemavu," amesema Dendego.


Dendego amesema tamasha hilo ni fursa kubwa na ya kipekee kwa wanawake wa Mkoa wa Singida kushiriki pamoja na mama Anne Makinda ambaye ni kiongozi mbobezi ili waweze kupata ladha sahihi ya wanawake na uongozi na matumizi ya takwimu katika kufanya maamuzi na utekelezaji wa mipango ya maendeleo.


"Kongamano letu litahusisha wanawake takribani 3,000 kutoka wilaya zote tano za Mkoa wa Singida na kubwa zaidi wanawake hawa vinara wanatoka kwenye ngazi za chini kabisa kwa maana ya vijiji mitaa na kata," amesema Dendego.


Ameongeza kuwa lengo la kuwakutanisha wanawake hao ni kuwahabarisha na kuwahamasisha kushiriki uchaguzi wa serikali za mitaa,uchaguzi ambao unatoa viongozi watakaosimamia maisha yao ya kila siku.


"Pamoja na tamasha hili,bado kuna mikutano mbalimbali inaendelea mabonanza ya michezo yanaendelea na ziara za viongozi nazo zinaendelea, lengo ni kiwafikia wananchi walio wengi na hasa maeneo ya pembezoni na kuwaleta pamoja kwenye jambo hili kubwa katika nchi yetu," amesema Dendego.


Aidha, amesema tamasha hili mbali na kuwaleta pamoja wanawake vinara litaanbatana na taarifa fupi za maendeleo na uzinduzi wa mpango wa matumizi ya nishati safi ya kupikia na litasindikizwa na burudani kutoka kwa wasanii mahiri.

"Tamasha hili la wanawakenwa Mkoa wa Singida linalobeba kauli mbiu Serikali za Mitaa,Sauti ya wananchi jitokeze kushiriki uchaguzi si la kukosa,atakuwepo msanii Msaga Sumu na singeli Isha Mashauzi na miondoko ya pwani na mwanamama mshereheshaji Angela Bondo," amesema Dendego

"Nawakumbusha wanawake wa Mkoa wa Singida,tamasha hili tumeliandaa pamoja na tushiriki pamoja kuliheshimisha na kujiheshimisha,hivyo mjitokeze kwa wingi sana ili tamasha lipendeze ikiwa ni moja ya safari ya kuwaunganisha wanawake katika mambo muhimu yanayogusa maisha yao," amesema Dendego.

Kwa mujibu wa sensa ya watu na makazi ya mwaka 2022 Mooa wa Singida unakadiriwa kuwa na watu 2,008,058 na nusu ya hao zaidi ya milioni moja watashiriki kwenye uchaguzi kutokana na kukidhi vigezo.

Matangazo

  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2022_2023 SINGIDA RS July 01, 2022
  • MAJINA YA WALIOCHANGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA - 2023, MKOA WA SINGIDA December 14, 2022
  • TAARIFA YA MAPOKEZI YA FEDHA KWA KIPINDI CHA KUANZIA JULAI HADI OCTOBA, 2023 KWA AJILI YA UTEKELEZAJI WA SHUGHULI ZA MAENDELEO November 01, 2023
  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2021/2022 SINGIDA RS - GPN 2021 - 2022 July 01, 2021
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • IKUNGI YAPEPERUSHA BENDERA KWA MIRADI YA KIMKAKATI.

    May 08, 2025
  • DKT.MGANGA ASISITIZA MADAKTARI BINGWA KUTOA HUDUMA BORA

    May 05, 2025
  • WATUMISHI NA WAAJIRI HODARI MKOANI SINGIDA WAPOKEA TUZO

    May 02, 2025
  • KUELEKEA MEIMOSI,RC DENDEGO ATANGAZA FURSA ZA UWEKEZAJI

    April 25, 2025
  • Angalia Zote

Video

Mkoa wa Singida waja na Mikakati ya Kuboresha Elimu
Video zaidi

Viungio vya Haraka

  • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
  • Mwongozo wa Matumizi ya TEHAMA Serikalini
  • Fomu ya Maombi ya Kusafiri Nje ya Nchi
  • MPANGO WA MANUNUZI MKOA WA SINGIDA
  • KUONA AJIRA ZA WAALIMU WA SAYANSI NA MAFUNDI SANIFU

Tovuti Muhimu

  • UTUMISHI
  • TAMISEMI
  • IKULU
  • WIZARA YA ELIMU
  • NECTA
  • WIZARA YA AFYA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Ramani ya Mkoa

Wasiliana Nasi

    SINGIDA

    Anuani: P O BOX 5 SINGIDA

    Simu: 2502170, 2502089

    Simu: 2502170, 2502089

    Barua Pepe: info@singida.go.tz ras@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Usiri
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

Copyright ©2023 Singida Regional Commisioner' Office . All rights reserved.