• Wasiliana Nasi |
    • Malalamiko |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
    • Blog |
Singida Regional Website

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Tovuti ya Mkoa wa Singida

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na dhima
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Ikungi
      • HISTORIA
    • Iramba
    • Manyoni
    • Mkalama
    • Singida
  • Halmashauri
    • H/W Ikungi
    • H/W Iramba
    • H/W Itigi
    • H/W Manyoni
    • H/W Mkalama
    • H/W Singida
    • H/M Singida
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Viwanda na Biashara
    • Madini
  • Huduma Zetu
    • Afya
      • Madaktari Bingwa
      • Huduma za Tiba
      • Huduma za Kinga
      • Ustawi wa Jamii
      • Afya ya Mazingira
      • Lishe
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba Wa Huduma Kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
    • Investment Guide
  • Kituo Cha Habari
    • Picha
    • Video
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma

Watoto 363,315 chini ya umri wa miaka mitano kupatiwa chanjo ya Polio Mkoani Singida.

Posted on: August 26th, 2022

Mkoa wa Singida unatarajia kutoa chanjo ya matone dhidi ya Ugonjwa wa Polio kwa watoto 363,315 wenye umri chini ya miaka mitano ili kujikinga na maradhi hayo.

Kauli hiyo imetolewa leo na Mkuu wa Mkoa wa Singida Peter Serukamba katika kikao cha uhamasishaji wa Kampeni ya utoaji wa chanjo ya matone dhidi ya Ugonjwa wa Polio kikao kilichofanyika katika ukumbi wa mikutano wa Ofisi hiyo.

Mkuu wa Mkoa wa Singida Peter Serukamba akizungumza na viongozi wa Dini mbalimbali na Wadau wa Afya katika kikao cha uhamasishaji wa Kampeni ya utoaji wa chanjo ya matone dhidi ya Ugonjwa wa Polio kikao kilichofanyika katika ukumbi wa mikutano wa Ofisi hiyo.

RC Serukamba amesema Halmashauri zote za Mkoa huo zitashiriki katika utoaji wa chanjo hizo ambapo Wilaya ya Iramba inatarajiwa kuwafikia watoto wasiopungua 56,360 Wilaya ya Singida inatarajia kuwafikia watoto 58,197 Manyoni 45,416 Manispaa 39,841 na Wilaya ya Ikungi watoto 77,638

Wilaya nyingine ni Mkalama ambapo inatakiwa kuwafikia watoto 51,658 na Itigi ambayo jumla ya watoto 34,205 watakaopata chanjo ya matone ya Polio alieleza RC Serukamba.

Aidha Serukamba amesema kauli mbiu ya Kampeni hiyo ni "Kila tone la chanjo ya Polio litawekwa, Tanzania salama dhidi ya Ugonjwa wa kupooza" ambapo kupitia kampeni hiyo inategemewa watoto wote wenye umri wa chini ya miaka mitano watapatiwa.

Hata hivyo RC Serukamba amesisitiza kwamba katika maandalizi hayo wataalamu wa afya wataendesha zoezi hilo katika vituo vya kutolea huduma ya  afya na kwa kutumia njia ya mkoba na kwamba kampeni hiyo itaendeshwa nyumba kwa nyumba, mtoto kwa mtoto ili kuwafikia wote.

Hata hivyo Mkuu wa Mkoa ametoa wito kwa wakuu wa Wilaya kupitia kamati za Afya ya msingi za Halmashauri kusimamia utoaji wa huduma ya chanjo kwenye vituo vya kutolea huduma za Afya na zitakazotolewa kwa njia ya mkoba ili kuwafikia watoto kwa asilimia 100.

RC Serukamba amewataka Wakurugenzi wa Halmashauri kuweka mikakati mbalimbali ya kuhakikisha watoto wote waliokosa chanjo ya awamu ya kwanza na pili wahakakishe wanapata awamu hii.

Akimalizia hotuba yake Mkuu wa Mkoa huyo akawataka wananchi kuhakikisha wanajitokeza kushiriki katika kampeni hiyo na kuwapeleka watoto wao kupata chanjo kwa ajili ya maisha yao.

Kwa upande wake Mratibu wa chanjo hiyo ki mkoa Habibu Mwinorya amesema kampeni hiyo inaanza tarehe 28 Agosti, 2022 wakati uchanjaji utanza tarehe 1 Septemba, 2022.

Habibu amebainisha kwamba chanjo kiasi cha dozi 350,000 zimekwisha sambazwa katika Halmashauri zote Saba za Mkoa wa Singida na mpaka sasa zimekwisha pelekwa katika vituo vyote vya kutolea huduma.

Mganga Mkuu wa Mkoa wa Singida Victorin Ludovick akizungumzakabla ya kumkaribisha Mkuu wa Mkoa wa Singida.

Mratibu wa chanjo hiyo ki mkoa Habibu Mwinorya akizungumza wakati wa kikao hicho.

Kikao cha kampeni ya chanjo kikiendelea

Matangazo

  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2022_2023 SINGIDA RS July 01, 2022
  • MAJINA YA WALIOCHANGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA - 2023, MKOA WA SINGIDA December 14, 2022
  • TAARIFA YA MAPOKEZI YA FEDHA KWA KIPINDI CHA KUANZIA JULAI HADI OCTOBA, 2023 KWA AJILI YA UTEKELEZAJI WA SHUGHULI ZA MAENDELEO November 01, 2023
  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2021/2022 SINGIDA RS - GPN 2021 - 2022 July 01, 2021
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • HUDUMA ZA KIBINGWA ZAWAFIKIA WAGONJWA ZAIDI YA 3000 SINGIDA.

    May 09, 2025
  • IKUNGI YAPEPERUSHA BENDERA KWA MIRADI YA KIMKAKATI.

    May 08, 2025
  • DKT.MGANGA ASISITIZA MADAKTARI BINGWA KUTOA HUDUMA BORA

    May 05, 2025
  • WATUMISHI NA WAAJIRI HODARI MKOANI SINGIDA WAPOKEA TUZO

    May 02, 2025
  • Angalia Zote

Video

Mkoa wa Singida waja na Mikakati ya Kuboresha Elimu
Video zaidi

Viungio vya Haraka

  • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
  • Mwongozo wa Matumizi ya TEHAMA Serikalini
  • Fomu ya Maombi ya Kusafiri Nje ya Nchi
  • MPANGO WA MANUNUZI MKOA WA SINGIDA
  • KUONA AJIRA ZA WAALIMU WA SAYANSI NA MAFUNDI SANIFU

Tovuti Muhimu

  • UTUMISHI
  • TAMISEMI
  • IKULU
  • WIZARA YA ELIMU
  • NECTA
  • WIZARA YA AFYA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Ramani ya Mkoa

Wasiliana Nasi

    SINGIDA

    Anuani: P O BOX 5 SINGIDA

    Simu: 2502170, 2502089

    Simu: 2502170, 2502089

    Barua Pepe: info@singida.go.tz ras@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Usiri
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

Copyright ©2023 Singida Regional Commisioner' Office . All rights reserved.